Njombe: Lori na Coaster vyagongana

Ilivyoonekana lori lilihama lane likaifuata coaster na kuichota mpaka imegeukia ilikotoka
Usingizi wa madereva, yanatembea usiku kucha, madereva wana mchepuko njia nzima, balaa balaa tu haya malory
 
Nimeona link ya video inayoonesha chanzo cha ajali, dereva wa coaster ndio alikuwa mzembe[emoji116][emoji116][emoji116]

https://www.facebook.com/
Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app

dah, inaonekana hilo lori lilikuwa na dash Camera au sijaelewa hii....

Dereva wa Coaster inaonekana kaovertake kifalafala hapo kwa kutoa nzima nzima, na inaokana hizo coaster zilikuwa kwenye ligi na zote zilikuwa kwenye safari moja na ushabiki ulikuwa mwingi barabarani kwa abiria kuwachochea madereva.....Traffic wanapaswa kufanya proper investigation itakayostate kila kitu na kutoa recommendation sahihi kuzuia haya mausenge...
 
Nategema kuona watu NIT kitengo cha road transport and traffic management wawe wanaandika papers za mara kwa mara namna ya kuondoa ajali hizi na kushauri serikali kadili wawezavyo..

Wahitimu wetu wa vyuo vikuu wanahitajika kuandika papers sana juu ya maisha ya kawaida tunayoishi na madhira tunayopitia labda tunaweza kupata suluhisho kupitia maarifa yao maana hili suala tukiliachia keshi la Polisi kila uchwao tutaisha...
 
Specialised Hauliers, hawa jamaa nikiwa safari ndefu napishana nao kwa adabu sana.

Na kama kumuovertake simpiti mpaka nihakikishe nimepigia honi za kutosha na kumwashia full light
njingi ni left hand
 
Utoaji wa Leseni kiholela uachwe na watu wafuate utaratibu kwenye utoaji wa leseni za udereva...

Hizi leseni za madereva wa magari ya abiria na mizigo ziwe na kitengo maalum kwenye utoaji wake na ziwe renewed kila miaka miwili... Madereva makosa yote ya kizembe wanyang'anywe leseni na kupigwa kabisa ban yakutogusa magari..

Tuwe na utaratibu wa kuwapima Afya madereva wa malori na magari ya abiria kabla ya kuwapa magari.....Afya kama Afya + afya ya akili....
 
Nimeona link ya video inayoonesha chanzo cha ajali, dereva wa coaster ndio alikuwa mzembe[emoji116][emoji116][emoji116]

https://www.facebook.com/
Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
Tazama zipo coaster mbili, coaster ya mbele alitoka nje ya lane ikaenda porini kujinusuru, hiyo ya pili ikavaana na lori, hayo mabasi yalikuwa kama manne kwenye msafara mmoja
 
Hizi leseni za madereva wa magari ya abiria na mizigo ziwe na kitengo maalum kwenye utoaji wake na ziwe renewed kila miaka miwili... Madereva makosa yote ya kizembe wanyang'anywe leseni na kupigwa kabisa ban yakutogusa magari..
Hao watoa leseni wanakuambia kadi haiendeshi gari, tatizo ni tabia
 
Dereva wa Coaster inaonekana kaovertake kifalafala hapo kwa kutoa nzima nzima,
Tazama zipo coaster mbili zilikuwa kwenye msafara mmoja coaster iliyotangulia ilikoswakoswa ikaingia porini, hiyo ya pili ndiyo ikapigwa na lori, hiyo sehemu barabara ina mawimbi sana
 
Ilivyoonekana lori lilihama lane likaifuata coaster na kuichota mpaka imegeukia ilikotoka
Tunarudi pale pale njia zetu bado finyu sana tena single way hizi zapaswa kuwa njia za mitaa siyo za kupita magari yanayosafiri kms nyingi
 
Ajali haina mipaka, hata kwenda sokoni tu chochote kinaweza tokea
Sio kweli.
Mbona tangu mwaka 2022 uanze, nishaenda sokoni zaidi ya mara 200 na sijawahi pata ajali yoyote.

Sasa assume ningesafiri mara 200 kutoka Dar kwenda Katesh Manyara kwa mwaka mzima. Si ningekua ⚰️ leo!
 
Sio kweli.
Mbona tangu mwaka 2022 uanze, nishaenda sokoni zaidi ya mara 200 na sijawahi pata ajali yoyote.

Sasa assume ningesafiri mara 200 kutoka Dar kwenda Katesh Manyara kwa mwaka mzima. Si ningekua ⚰️ leo!
Hiyo ni hofu ndio maana nikakupa tu mfano wa safari ya hapo hapo, kwa nini hujaziacha kwa kuhofia ajali
 
Wenye Mungu ingieni kwenye maombi.

Damu ya Watanzania inamwagika sana.

Mungu awarehenu wapendwa wetu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…