Njombe: Mfungwa apora Bunduki kwa Askari na kumpiga kaka yake kwa kushindwa kumtoa Gerezani na kuuza mashamba ya familia

Njombe: Mfungwa apora Bunduki kwa Askari na kumpiga kaka yake kwa kushindwa kumtoa Gerezani na kuuza mashamba ya familia

Kuna wale wazazi wanaozaa watoto wa uzeeni, anakuwa na watoto wakubwa anaenda kuchukua dogodogo na kuanza kufyatua vijukuu, wapo wengi tu hasa maeneo ya vijijini. Sasa automatically huo utakuwa mzigo wa watoto wakubwa maana mara nyingi wazee wa dizani hiyo huwa hawana mwelekeo wowote.
Inawezekana hao ni mtu na kaka yake lakini sio baba mmoja, wanatumia jina la ukoo ( mfano mmoja ni mtoto wa baba mkubwa, na mwingine ni mtoto wa baba mdogo)
 
aisee 61 kwa 24 mtu na kaka ake mimi na 24 baba angu ana 58
 
Huyo askari mpaka anaporwa hiyo silaha yeye alikuwa kalewa au
...Si ajabu alikuwa kasinzia, kama tunavyowaonaga askari wa Lindo wakiwa wamesinzia huku wakiwa wameshika Silaha! Ni hatari tupu....
 
Kijana, Isaack Kawogo(24) aliyempora Askari magereza silaha aina ya SMG Usigani mkoani Iringa ameuawa kwa kupigwa risasi na Polisi baada ya kumjeruhi kaka yake, Andres Kawogo(61) akimtuhumu kuuza mashamba na kushindwa kumtoa gerezani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Hamis Issah amesema tukio hilo limetokea Novemba 20, huko maeneo ya Chaugingi mjini Njombe.

Amesema Kawongo aliiba silaha na kuitumia kufanya uhalifu ambapo alifanya matukio kadhaa Mkoani Iringa ikiwemo kumshambulia Askari kwa panga hali iliyosababisha wafungwa wengine kutoroka.

“Hii ni silaha ambayo askari magereza wanaitumia katika ulinzi wa wafungwa hao sasa huyu kwakuwa ni mhalifu akawa anaitumia katika kufanya uhalifu,” Kamanda Issah.

Amesema silaha hiyo ilikuwa na risasi kumi lakini mpaka inakamatwa na askari ilikuwa imebakiwa na risasi mbili pekee huku risasi nane zikitumika kufanya ualifu maeneo tofauti ikiwemo tukio hilo lilotokea Mkoani Njombe la kumjeruhi kaka yake.

Amesema licha ya juhudi kufanyika za kutaka kuokoa maisha yake ili alieleze Jeshi la Polisi namna alivyoondoka na silaha lakini ilishindikana kwa kuwa umauti ulimfika.

” Ukimnyang’a askari silaha namna pekee ya kuipa hiyo silaha ni kwa kutumia silaha hivyo wanapaswa kuwa makini,” Kamanda Issah
....Aliiba silaha halafu akamshambulia Askari na Panga...???
 
Askal mmoja analinda magerezaa 10 hatari hii
 
Walitulia hawa Wahehe, Wabena, na Wakinga mpaka mbwa walijazana mjini. Tuone sasa mambo yatakuwaje baada ya hili tukio maana hawa jamaa wana tabia ya kushindana vituko, kila mmoja anataka kabila lake lijulikane kuwa ni la hasara au wapenda vituko. Leo kaja huyu jamaa kuua, kesho atakuja msela mwingine kutaka kumzidi mwenzake kwa tukio jingine, utasikia tu mtu kafila kifaranga cha kuku hadharani au amakutwa kajinyonga baada ya kurudi nyumbani bila kukuta chai na viazi vitamu. Jamani Wahehe, Wabena na Wakinga, mnakosea wapi nyie watu?.
 
Back
Top Bottom