mwanateknolojia
JF-Expert Member
- Nov 17, 2014
- 1,026
- 1,749
Hata kisikizo kinaweza kusemwa kilikutwa kwenye gari.Hivi katika ulimwengu wa sasa kuna mkanda wa mtu specific kweli. Mbona wamasai wanatutengenezea mikanda inayofanana. Lisiwe shinikizo la kale kazee kakijana ka juz
Mkanda ulimdondoka!? Amini usiamini.Sasa hapo unachobiisha ni nin mkuu?
Rais wao Chadema angeamuru wote wangekamatwa, bahati mbaya hawana rais.Watawakamata lakini sheria haitawafunga! Aliuwawa Mawazo hakuna mwanaCCM aliyekamatwa hata mmoja! Alishambuliwa mwanasheria mkuu wa CHADEMA Tundu Lissu, hakuna mwanaCCM aliyekamatwa hata mmoja! Alitekwa na kutoweka msaidizi wa Mbowe, hadi leo hakuna mwanaccm aliyekamatwa hata mmoja! Alishambuliwa na kuvunjwa mguu Mwenyekiti taifa wa CHADEMA Freeman Mbowe, lakn mpaka leo hakuna aliyetuhumiwa hata mmoja achilia mbali kukamatwa! Hivyo kama kweli waliokamatwa kwa tukio hilo ndio hasa wahusika, basi nashawishika kusema kumbe wahalifu huwa wanajulikana lakini kukamatwa inategemea unavaa khaki au kijani! Therefore Penye CHADEMA weka CCM, penye CCM weka CHADEMA!
Ili mgombea wa CCM apite bila kupingwa mbinu inayotumika ngazi zote toka tupate Uhuru tumeona Fomu ya kutia nia ya kugombea inachapishwa moja tu ili kusiwe na mpinzani na hivi mgombea mmoja anahojiwa badala ya kuwa kwenye kampeni kama mpinzani wake. Kila mbinu chafu inatumika ili wagombea hovyo wa Chama hicho wapite kwa kishindo ili wadanganye ulimwengu kuwa wanakubalika wanasitahili kuongoza nchi milele. Hizi mbinu zinatumika dhidi ya Chama kimoja tu cha CHADEMA kati ya Vyama 19 vilivyosajiliwa kwa sababu ndo chenye wanachama mahili na wakati wa Uchaguzi ndo kinawapatia ushindani mkali kutishia kuendelea kwao kuongoza. Kuna matukio mengi ya kijinai yamejiri Awamu hii kama vile watu kutekwa, kupotea, kuuawa, kujeruhi kwa risasi na maiti kuokotwa bila Polisi kujihusisha kwa namna yoyote ile hata tu kuonyesha wapo na wanajali lakini kuokotwa maiti ya mwanachama wa Chama Tawala wagombea wanne wa Upinzani wamekamatwa. Hata kwa sisi tusiyo Polisi haingii akilini wauaji wakijua watakuwa watuhumiwa namba moja wanavua mkanda wa marehemu na kuuacha ndani ya gari yao iliyotumika kwenye mauaji. Kama watu wanabambikiziwa kesi itashangaza kama watu hawawezi kubambikiziwa ushahidi (exhibit)!Umbambike kesi diwani ili iweje?
Wewe ni lipumbavu kabisa. Did you understand my writing? Pumbavu kazi kukurupuka tu. Mbweha mkubwa!.Mbinu mpya zikoje hebu tufahamishe, lazima mchezee kichapo cha kisheria huu ujinga wenue wa kujifanya mko juu ya sheria. Kisanga kikitokea unavuna mwenyewe, tunawaambia acheni ushabiki wa kijinga wa kujifanya mko juu ya sheria. Leo boss wenu lISSU anafundishwa namna ya kuheshimu sheria za nchi, akitoka huko atakuwa amepata digree ya uaminifu. Jinga kabisa
CHADEMA ikichukua nchi oktoba 28 italifuta jeshi la polisi , huu ujinga wa kuwanunua wagombea udiwani ulipangwa na kwamba wakikataa watapewa kesi yoyote , na hii imevuja tangu wiki 2 zilizopita eti leo ndio inatekelezwa ! Poor Polisi
Kasaidie kwa ushahidi. Na huo ndio Uzalendo na Uraia mwema maana inaonekana unajua mengi kweli hili.Polisi fanyeni kazi yenu ila hapo Kuna walakini huyo kada wa CCM alikuwa anang'ata huku then anapuliza kule sasa kwa kawaida ya CCM wakishakujua kuwa wewe ni msaliti lazima wakuuwe ila hapo ukatengenezwa ushahid fake wa kufanya mawasiliano kabla ya mauwaji kufanyika na ikiwa nikiwasiliana na hao makada wa CDM logic ndogo ni kwamba pengne alitekwa halaf wakasema ili tusikuuwe tunaomba umpgie fulani na Fulani waje sehem fulan ko kivyovyote vile akifa mawasiliano yataonesha mtu wa kuwasiliana nae then huyo ndo mtuhumiwa namba moja hii Kama imetengenezwa haya kuhc mkanda wauwaji wanaweza wakaweka mkanda kwenye gari then wakatoa taarifa kwa polis ko kila kitu kinawezekana
Hongeren vyombo vya ulinzi na usalama wa raia. Mkumbuke kuwakamata na wale waliomuua Daud Mwangosi. Kazi yenu ni njema sanaNi mauaji ya yule kijana wa CCM kule Njombe.
Wagombea udiwani wawili na Katibu mwenezi wa kata wote wa CHADEMA na dalali wa mbao wamekamatwa kwa kuhusishwa na mauaji ya mwanafunzi wa chuo kikuu na kada wa CCM yaliyotokea huko Njombe.
Pamoja na wao pia gari la mtuhumiwa mmojawapo limekamatwa na kukutwa baadhi ya vitu vya marehemu vikiwa ndani yake.
=======
RPC wa Njombe, Hamis Issa amesema,gari namba T457 DAB Toyota Gaiya ya George Sanga mgombea udiwani kata ya Ramadhani(CHADEMA)ilitumiwa wakati wa utekelezaji wa mauaji ya Kada wa CCM Emmanuel Mlelwa kutokana na kukutwa mkanda wa kiunoni wa marehemu baada ya gari hiyo kushikiliwa
Jeshi la polisi mkoani Njombe limesema mpaka sasa wanashikiliwa watu wanne wakiwemo makada watatu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa tuhuma za mauaji ya Emmanuel Mlelwa mwanafunzi wa chuo cha Tumaini Iringa ambaye ni mwenyekiti wa wanafunzi wa vyuo na vyuo vikuu (UVCCM) mkoa wa Iringa.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe Hamis Issa akizungumza na vyombo vya habari,amesema jeshi hilo limewashikilia watu hao kutokana na upelelezi wa awali wa mawasiliano yake.
“Jeshi la polisi lilianza upelelezi na tukajua mtu wa mwisho aliyekuwa anaongea naye ni mtu mmoja anaitwa Tadei Mwanyika,huyu ni mgombea udiwani kupitia kata ya Utalingolo,tulimkamata na hakuwa na maneno mengi yeye anasema kweli nilikuwa na Marehemu”alisema kamanda Issa
Aidha amesema mtu wa pili kutambuliwa ni George Sanga mgombea wa Udiwani kupitia Chadema kata ya Ramadhani ambaye gari yake ilitumika kuwabeba watu hao akiwemo marehemu Emmanuel Mlelwa.
Vile vile amesema mtuhumiwa mwingine aliyeshikiliwa ni Optatus Mkwera katibu mwenezi wa kata ya Ramadhani wa Chadema ambaye kwa mujibu wa maelezo yake ameeleza tukio zima lilivyokuwa.
“Huyu naye alihusika kushiriki mauaji kwa mujibu wa maelezo yake”alisema Kamanda
Mtuhumiwa wa nne ni Gudluck Mfuse anayejishughulisha na udalali wa magari yanayobeba mbao na viazi ambapo kamanda wa polisi amesema tukio hilo anaamini lilikuwa limepangwa na jeshi hilo linaendelea na upepelezi dhidi ya mtandao huo ili haki itendeke.
Hata hivyo kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe Hamis Issa amesema gari namba T457 DAB Toyota Gaiya inayomilikiwa na George Sanga mgombea wa udiwani kata ya Ramadhani ndio inayotuhumiwa kutumiwa wakati wa utekelezaji wa mauaji ya Kada huyo wa CCM kutokana na kukutwa mkanda wa kiunoni wa marehemu baada ya gari hiyo kushikiliwa.
Mkuu wa mkoa wa Njombe mhandisi Marwa Rubirya amesema mwili wa marehemu Emmanuel, ulikutwa eneo la bwawa la maji kibena na alipotea tangu tarehe 20 mwezi wa 9 huku akiwa ni miongoni mwa vijana walioko kwenye timu ya kampeni ya mgombea wa Ubunge jimbo la Njombe mjini.
“Kwa mara ya mwisho simu yake ilikuwa hewani tarehe 20 tangu hapo hakupatikana lakini kwa kuwashirikisha ndugu wa marehemu ilibainika mwili uliokuwepo hospitali ni wa Emmanuel Mlelwa na ushahidi wa awali unaonyesha ndugu Emmnuel ameuawa kikatili katika mazingira ya kisiasa”alisema Marwa Rubirya
Hata hivyo uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kupitia kwa mwenyekiti wake Rose Mayemba wameliomba jeshi la polisi kuweka wazi juu ya taarifa za wagombea wao bila kuharibu uchunguzi wao.
“Tunaliomba jeshi la polisi kama kuna mambo inafuatilia ni vema sisi na wao kuwe na taarifa za wazi kama wamehusika na mauaji watuambie lakini kitendo cha kuficha taarifa sahihi hatuwezi kuishi kwa namna hiyo kwa kuwa wale ni wagombea”alisema Rose Mayemba.
Sawa sawa mkuu.....Omba yasikukute wewe au ndudu yako. Kumbuka maendeleo yana vyama lkn udikteta hauna chama wala mtu. Kawaulize kina nape, makamba, membe, mangula, na kinana watakwambia na kukusaidia ww buku 7 ili akili zikufungukeTuweke jina alilotaja.
Halafu anaongea na vyombo vya habari, kwanini asiende polisi?
Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Hatimaye. Utawala wa kuanzia 2015 ulikuwa wa kibabe sana kusema kweliKaachiwa huru