Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Wananchi wa kijiji cha Ngelenge wilaya ya Ludewa mkoani Njombe wamelazimika kuifunga ofisi ya mwenyekiti wa kijiji chao Bwana Thomas Mkinga wakimtuhumu kuwa anahujumu uchumi wa kijiji huku wakimtaka ajiuzulu kwenye nafasi yake.
Frolence Haule ni mmoja wa wananchi wa kijiji hicho ambapo amesema mwenyekiti amekuwa akikusanya pesa za ushuru na kufanyia matumizi binafsi na wanapohitaji mikutano kwa ajili ya taarifa ya mapato na matumizi amekuwa akikataa kuitisha huku Avelina Mbonde akieleza kuwa hawahitaji kuongozwa tena na mwenyekiti huyo.
Mkinga alipoulizwa juu ya tuhuma hizohakuweza kuzungumza chochote akidai mpaka atakapopata kibali kutoka ngazi za juu.
Victoria Mwanziva ni mkuu wa wilaya ya Ludewa amesema wanaendelea kufanya uchunguzi juu ya jambo hilo sambamba na kusuruhisha mgogoro huo ili wananchi waendelee kupata huduma kupitia ofisi hizo.
"Niwaase viongozi wa ngazi zote kupeuka migogoro na wananchi na zinapotokea kesi mbalimbali watatue kwa wakati ili kutoathiri utendaji kazi na utoaji wa huduma"amesema DC Mwanziva
Frolence Haule ni mmoja wa wananchi wa kijiji hicho ambapo amesema mwenyekiti amekuwa akikusanya pesa za ushuru na kufanyia matumizi binafsi na wanapohitaji mikutano kwa ajili ya taarifa ya mapato na matumizi amekuwa akikataa kuitisha huku Avelina Mbonde akieleza kuwa hawahitaji kuongozwa tena na mwenyekiti huyo.
Mkinga alipoulizwa juu ya tuhuma hizohakuweza kuzungumza chochote akidai mpaka atakapopata kibali kutoka ngazi za juu.
Victoria Mwanziva ni mkuu wa wilaya ya Ludewa amesema wanaendelea kufanya uchunguzi juu ya jambo hilo sambamba na kusuruhisha mgogoro huo ili wananchi waendelee kupata huduma kupitia ofisi hizo.
"Niwaase viongozi wa ngazi zote kupeuka migogoro na wananchi na zinapotokea kesi mbalimbali watatue kwa wakati ili kutoathiri utendaji kazi na utoaji wa huduma"amesema DC Mwanziva