Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakati zoezi la uchukuaji fomu za kugombea uenyekiti na ujumbe wa serikali za mitaa likiendelea nchini, wakazi wa Mtaa wa Kambarage mjini Njombe wameomba kampeni za kistaarabu zisizo na lugha za matusi pindi zitakapoanza.
Wananchi hao wamesisitiza umuhimu wa kampeni zenye kujenga umoja na maendeleo kwa ajili ya ustawi wa mtaa wao.
Mgombea wa nafasi ya uenyekiti kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Emmanuel Kayombo, pamoja na wajumbe wake, walichukua fomu huku wakiwa na matumaini ya kuchaguliwa ili kusaidia kutatua changamoto mbalimbali, hususan usimamizi wa miradi ya maendeleo na masuala ya kifedha.
Soma pia: RC Njombe awaongoza Wananchi kujiandikisha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
Kwa upande wake, Nicodemus Funi, ambaye ni msimamizi msaidizi wa uchaguzi katika mtaa huo, alieleza kuwa hadi sasa ni vyama viwili tu, CCM na CHADEMA, ambavyo vimechukua fomu za kugombea.
Wanachama wa CHADEMA waliomsindikiza mgombea wao katika zoezi hilo wameonyesha imani kubwa kwake, wakiamini kuwa atachangia kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi wa Kambarage.
Source: Uplands FM
Wananchi hao wamesisitiza umuhimu wa kampeni zenye kujenga umoja na maendeleo kwa ajili ya ustawi wa mtaa wao.
Mgombea wa nafasi ya uenyekiti kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Emmanuel Kayombo, pamoja na wajumbe wake, walichukua fomu huku wakiwa na matumaini ya kuchaguliwa ili kusaidia kutatua changamoto mbalimbali, hususan usimamizi wa miradi ya maendeleo na masuala ya kifedha.
Soma pia: RC Njombe awaongoza Wananchi kujiandikisha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
Kwa upande wake, Nicodemus Funi, ambaye ni msimamizi msaidizi wa uchaguzi katika mtaa huo, alieleza kuwa hadi sasa ni vyama viwili tu, CCM na CHADEMA, ambavyo vimechukua fomu za kugombea.
Wanachama wa CHADEMA waliomsindikiza mgombea wao katika zoezi hilo wameonyesha imani kubwa kwake, wakiamini kuwa atachangia kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi wa Kambarage.
Source: Uplands FM