Niliwai kuishi wilaya ya bahi Dodoma...kuna siku moja Niko nje ya nyumba majira ya mchana wa saa 7 hivi,alitokea mtu gafla akaniomba nimletee maji ya kunywa ,nilipoingia ndani nakutoka nikakuta yupo kifua wazi wakati alikuwa kavaa shati....na Hana chochote alichobeba.....nikampatia maji akanywa kisha akaniambia kuwa anaenda safari ya mbali na katokea Dodoma mjini kwa mguu....kisha akaondoa ....alipiga hatua Kama 4 baada ya hapo sikuona mtu upande wowote ule ........2005 ilikuwa .....
Duh!mzee ulienda kuwanga wewe bila kujijua[emoji2] [emoji2]hili tukio sijui niite ndoto au uhalisia.
nikiwa na miaka 14 mikoani mbeya wilaya ya kyela, kuna siku nimelala usiku nikaota nipo sehemu na mtoto wa jirani yangu na baba yake ambao wanakijiji walikuwa wanawatuhumu kwamba ni wachawi, sina uhakika kuhusu hilo.
basi huko tulipokuwa tulikuwa tunafanya mambo mengi ni kama sherehe hivi, baadae baba wa yule kijana akasema mda umeisha inatubidi turudi nyumbani. Tukaanza kupaa wakati tunakaribia kufika nyumbani ghafla nikawa kama nimeshtuka kutoka usingizini kabla sijaingia ndani, lakini chakushangaza nikiwa bado sijielewi vizuri nikaona ukuta unafunguka na nikaingia kwa kasi ya kama spidi 500 mpaka kitandani. Nilivyofika kitandani akili ndio ikaa sawa, sasa nikawa najiuliza hii ni ndoto au uhalisia sijawahi pata jibu mpaka leo.
hakuna kitu nakichukia duniani kama kuwa mchawi.Duh!mzee ulienda kuwanga wewe bila kujijua[emoji2] [emoji2]
Wachawi wangese sana ila shukur wamekurudishahakuna kitu nakichukia duniani kama kuwa mchawi.
Mkuu ilikua kweli hiohili tukio sijui niite ndoto au uhalisia.
nikiwa na miaka 14 mikoani mbeya wilaya ya kyela, kuna siku nimelala usiku nikaota nipo sehemu na mtoto wa jirani yangu na baba yake ambao wanakijiji walikuwa wanawatuhumu kwamba ni wachawi, sina uhakika kuhusu hilo.
basi huko tulipokuwa tulikuwa tunafanya mambo mengi ni kama sherehe hivi, baadae baba wa yule kijana akasema mda umeisha inatubidi turudi nyumbani. Tukaanza kupaa wakati tunakaribia kufika nyumbani ghafla nikawa kama nimeshtuka kutoka usingizini kabla sijaingia ndani, lakini chakushangaza nikiwa bado sijielewi vizuri nikaona ukuta unafunguka na nikaingia kwa kasi ya kama spidi 500 mpaka kitandani. Nilivyofika kitandani akili ndio ikaa sawa, sasa nikawa najiuliza hii ni ndoto au uhalisia sijawahi pata jibu mpaka leo.
ni fumbo kwa kweli.Mkuu ilikua kweli hio
ila najiulizaga hii teknolojia ya kufungua ukuta inawezekanaje hasa process zake
Hii ilikua kweli[emoji26]wachawi sio watu wazurihili tukio sijui niite ndoto au uhalisia.
nikiwa na miaka 14 mikoani mbeya wilaya ya kyela, kuna siku nimelala usiku nikaota nipo sehemu na mtoto wa jirani yangu na baba yake ambao wanakijiji walikuwa wanawatuhumu kwamba ni wachawi, sina uhakika kuhusu hilo.
basi huko tulipokuwa tulikuwa tunafanya mambo mengi ni kama sherehe hivi, baadae baba wa yule kijana akasema mda umeisha inatubidi turudi nyumbani. Tukaanza kupaa wakati tunakaribia kufika nyumbani ghafla nikawa kama nimeshtuka kutoka usingizini kabla sijaingia ndani, lakini chakushangaza nikiwa bado sijielewi vizuri nikaona ukuta unafunguka na nikaingia kwa kasi ya kama spidi 500 mpaka kitandani. Nilivyofika kitandani akili ndio ikaa sawa, sasa nikawa najiuliza hii ni ndoto au uhalisia sijawahi pata jibu mpaka leo.
hili tukio sijui niite ndoto au uhalisia.
nikiwa na miaka 14 mikoani mbeya wilaya ya kyela, kuna siku nimelala usiku nikaota nipo sehemu na mtoto wa jirani yangu na baba yake ambao wanakijiji walikuwa wanawatuhumu kwamba ni wachawi, sina uhakika kuhusu hilo.
basi huko tulipokuwa tulikuwa tunafanya mambo mengi ni kama sherehe hivi, baadae baba wa yule kijana akasema mda umeisha inatubidi turudi nyumbani. Tukaanza kupaa wakati tunakaribia kufika nyumbani ghafla nikawa kama nimeshtuka kutoka usingizini kabla sijaingia ndani, lakini chakushangaza nikiwa bado sijielewi vizuri nikaona ukuta unafunguka na nikaingia kwa kasi ya kama spidi 500 mpaka kitandani. Nilivyofika kitandani akili ndio ikaa sawa, sasa nikawa najiuliza hii ni ndoto au uhalisia sijawahi pata jibu mpaka leo.
Aliweka yeye hii, mtumishi hagangui kama wagangawakuu mie binafsi sijawahi kukutana na kisa kikubwa chakutisha kivile sema kunakimoja ambacho kilitokea ambacho kinanipa maswali mpaka iitwayo leo
ilikuwa ni kipindi flani wazee wangu wanapata huduma ya kiroho ka waumini wengine katika kanisa flani basi wakawa wanapata shuhuda mbalimbali toka kwa wenzao basi nao wakataka nao wapate baraka hizo za Mungu maana hakuna asiyezitaka ukizingatia nao walikuwa na shida zao. Basi wakaendelea kufanya taratibu zao ka kawaida ili wawezepata kibali chao cha kumshuhudia Mungu wao namie nikiwa ka mtu wa kando ka hayo mambo hayaniusu. Wakaendelea kupata maombi na kuhudhuria ibada basi siku moja kiongozi wao wa kiroho akawaahidi kufika nyumbani kwaajili ya kufanya maombi na kuombea nyumba na familia kwa ujumla
Day one alifika mida ya usiku ka mida ya saa mbili, ikiwa mama ndo alikuwepo akanialika namie kuweza kupata baraka na mengine ya kiroho, mchungaji akafanya maombo kiasi pamoja na wasaidizi wake baada ya muda akasema nitakuja sikunyingine kwaajili ya maombi tena. basi akaondoka. na mzazi akaondoka siku iliyofuatia mie ndo nikaachwa kwaajili ya kumpokea kiongozi huyo wa kiroho siku atakayokuja.
Siku iliyofuatia baada ya siku kadhaa ilikuwa ngumu kumpata kiongozi huyo wa kirohoo maana alikuwa anahudumia watu wengi na alikuwa busy na majukumu mengine ya Kanisa, nikafanya jitihada za kuwasiliana nae mara kwa mara basi akaniahidi one day atafika.
Hiyosiku aloyofika akafika salama maana alikuwa anatokea mbali kiasi na alifika mida ya usiku maana alitoka kutoa huduma sehemu nyingine basi akafanya maombi nikiwa nae na baadhi ya watu wengine baada ya hapo akaanza kumwaga maji ya baraka nyumba nzima na vyote vilivyokuwepo nyumbani hasa magari na nyumba zote na vyumba vyote, baada ya hapo akarudi tena akafanya maombi kiasi then akaniambia twende nje.
Tukazunguka kwenye eneo la nje akaanza kutafuta tafuta akaniambia ka naona kitu, nikamjibu sioni akatafuta tena na tena kwakutumia mwanga wa simu basi akaanza kusema 'lilikuwa linataka kukimbia tena na leo' basi akakiona kumbe ilikuwa kibuyu na kichupa vimefungwa pamoja na vinashanga na kitu ka irizi nyeusi na nyekundu, nilistaajabu sana. akanijuza kuwa ilikuwa inataka kukimbia na ndo maana siku ya kwanza alishindwa kuikamata. na hizo zana za kishirikina zilikuwepo sehemu nyeupe ambayo ni rahisi kuviona ila akaniambia vilikuwa ndani ya banda lililokuwepo karibu ila kwakuwa alimwaga maji yaliyobarikiwa kikashindwa kukimbia kikaishia hapo nje na akanijuza kwa macho ya kawaida huwezi ona
Mpaka leo najiuliza sana hivi ule ushirikina ulitoka wapi na uliwekwa pale nyumbani toka lini na unawezaje kukimbia pindi nguvu ya Mungu ijitokezapoooo? Mpaka leo lile tukio huwa nalikumbuka sana na vile kibuyu kilivyousisimua moyo wangu.
Dah stori inatisha hiiAcha nami nishee story yangu japo si mzuri sana katka uandishi.
Ilikua 2010 Dar es salam enzi hizo nikiwa mwanafunzi wa chuo kimoja hapo. Ukweli sikukutana nakiumbe cha kutisha bali ni binaadam alienifanya nibaki na sintofaham na maono tofauti ktk maisha.
Sikubahatika kupata chumba ktk hostel za chuo ikanibidi nipange kitaa flan uswahilini karibu na mwenge hapo. Maisha yalikua fresh tu fadha house alikua na wake wawili na watoto kadhaa hapo kijana mkubwa wa mwenye nyumba alitokea kua mwanangu sana story za hapa na pale, jamaa alikua mstaalabu sana na anasura ya upole by that time alikua kama ana 30 yrs nakuendelea.
Tukio lilotokea lilinifanya nibaki mdomo wazi ni siku moja mida ya saa tisa kasoro huyo bro aliniamsha kwa kugonga mlango nlisita kuitika lkn mwisho nilifunua nakumkuta amemkamata kijana mmoja wa makamo. Jamaa akanambia kwamba huyu ni mwizi na huwa anaibia watu hapo mtaani. Nikamuuliza vp ushahidi unao akadai hana ila amemkuta na kisu mfukoni. Nilitaka kuacha kumpa ushirikiano ila nikaona nimsaidie huyo kijana asijedhurika kwani hakukua na ushahidi wowote. Nilimshauri jamaa kua tuamshe majirani au ndg zake jamaa akawa mbogo. Ilibidi nimfate kwanyuma akiwa amemkamata yule kijana shingoni tukielekea nyumba iliokua opposite na hii tunayokaa. Nilipata bahati ya kumuuliza jamaa akakubali ni kweli hapo aliwahi iba shati na sendoz. Nilijua itakua kesi ndogo lkn tulipofika kwa huyu jirani aligonga mlango mara mbili tatu huyo mzee akafungua na kuelezwa dhumuni la sie kuwepo hapo. Alimtazama yule kijana kwa macho ya dharau na kuulizia mimi kwani hakuwahi niona maeneo hayo ndo jamaa akanitambulisha kama mpangaji wao. Yule mzee haraka bila uoga alitupa jukumu tumuue huyo dogo then tukimaliza tumchome moto hapo hapo. Nilihisi kuogopa nikaona ni kama mzaha vile kwani tulikua wawili tunaopewa jukum hilo. Alipomaliza kufunga mlango wake mzee yule nilimwambia huyu mshkaj kwanini tusimteme tu dogo coz vitu alivyoiba nividogo sana. Msela alinifokea sana na kunipolomoshea matusi makali. Ilibidi niwe mtazamaji asikwambie mtu kifo ni kitu rahisi sana, dogo alishushiwa kipigo hevy ngumi na mateke mpaka akazimia ndipo jamaa alipoanza kutumia mawe yaliyokua pembeni . Ilifika muda dogo alipiga mayowe maskini it was too late, jamaa alihitaji kuua siku hiyo. Baada yakama dakika saba dogo alivuta nikimshuhudia alimsihi yule jamaa akimtaja kwa jina kua unaniua bure bro mimi ni mdogo wako, haikusaidia kitu dogo alipigwa taili mbili na kumwagiwa mafuta ya taa. Aliwaka mpaka mwisho. Niliogopa sana na usiku huo sikulala tena taswira ya kile kipigo ilikua ikinijia kichwani. Niliogopa sababu dogo alouwawa na huyu jamaa ni wa pale mtaani vp mimi mgeni. Nakwanini jamaa hakutaka watu waamshwe na dogo mbona hakua amemuibia huyu jamaa kitu.
Ilibidi iwe siri yangu mpaka nilpokuja kufahamishwa na majirani wengine juu ya kuokotwa mara kwa mara maiti zisizo julikana mtaani. Ilibidi nihame kimya kmya na kujiapiza kua sintokuja kupanga uswahilini tena na hawa binadam wenye sura nzuri za upole niishinao kwa tahadhari kubwa.
Sent using Jamii Forums mobile app
haikujirudia.Huikujirudia tena hio hali?
Ndo ukome!!Ukitaka kufatilia mambo ya kutisha iandae akili yako na mwili vinginevyo unaweza data kabisa,
Nikiwa kijijini nyumbani nasoma shule ya msingi nilikuwa mkorofi sana na jeuri siku moja rafiki yangu wa kike alinunuliwa Baiskel zile za gia na baba yake akatoka nayo kwao mjini hadi nyumbani kijijini basi mm na ukorofi wangu nikachukua ile baiskel nikaiendesha njia zote za kijijini zile nzuri nawavimbia watu kwamba nina chombo yenye gia nne ilipofika saa 12 jioni nikarudi home,nikapaki na rafiki yangu alinambia analala ataondoka kesho yake.
Ratiba yangu lazima nisafishe uwanja jioni ili nikiamka asubuhi uwanja msafi naamkia shambani laah kabla ya usafi nikachukua baiskeli nikaiweka ndani nikafunga chumba na kufuli kubwa la store then nikasafisha uwanja kilichofata ni kulala hapo ndio tatizo lilianza usiku nilishtuka usingizini nikasikia kelele nje ila sasa kelele ni kama mtu anaendesha baiskeli mwanzo nilijua mwizi ila nikatulia kidogo ndipo nilipogundua mchana nilifanya kosa kuwalingia watu na kile ki baiskeli usiku ule kama masaa matano baiskeli ile iliendeshwa kuzunguka nyumba mpaka nikachoka kusikiliza sauti nilipomwamsha kaka asikilize zile sauti ajabu hasikii kitu, nikijaribu kuwasha kibatari unatokea upepo unazima mpaka nikachoka nikaaamua kulala tu asubuhi nilikuta mistari ya baiskeli mji mzima kufungua store baiskeli ipo vilevile niliogopa hata kuigusa
Pole sana vp dogo anaendeleaje?Binafsi sikuwahi kushuhudia mambo ya kutisha,hata Kama yalikuwepo madogomadogo yalikuwa ya kawaida tu..Ila baada ya kuoa na kubarikiwa na mwanangu wa kiume mambo yalianza kubadilika.
Ni hivi,
Mwanangu wakati akiwa na miaka Kama mitano hivi alianza kuongea kuhusu mambo yaliyotushangaza sana mimi na mke wangu..kuna wakati mmoja kulinyesha mvua ya rasharasha tu tukawa tunarudi home kutoka madukani naye..kawaida Kuna Ile harufu ya mchanga baada ya mvua ya aina hii kunyesha baada ya muda mrefu..sasa kilichonishangaza ni kuwa mwanangu alianza kusema kwamba anahisi harufu ya mungu..nikamwambia ni harufu ya mchanga tu Ila akawa mkali kidogo kwamba nakataa kukubaliana naye kuwa mungu hunukia hivo..tulipofika home lile Jambo likanifikilisha sana nikasema japo huenda ni upuuzi tu wa kitoto wacha nimwambie mke wangu..ndipo naye akaniambia kwamba kuna wakati kijana wetu alikuwa akimtayarisha kuenda shuleni kisha mtoto akamwambia kwamba anampenda sana na sio Kama mamake yule mwingine wa "nyumba iliozeeka"alisema kwamba yule mamake mwingine ni mkali na wakati mwingine hampi hata chakula kizuri..hili Jambo lilitushtua Sana na siku moja nikamwambia mwanangu anipeleke "nyumbani kwao huko kulikozeeka"
Yani nilishtuka mwanangu aliponiongoza hadi tunafika sehemu flani kuna jumba kubwa na ambalo kwa muonekano ni Kama lilijengwa miaka ya zamani na ambalo hamna anayeishi humo..japo hatukuingia nilishtuka sana.
Ilipita siku nyingi mwanetu akitupa shuhuda za mambo ya ajabu ajabu nasi tukawa tunaomba Mungu sana amuepushe na mambo ya kivile..Ila yaliendelea tu..
Siku moja nakumbuka ilikuwa jumapili fulani naelekea home mida ya saa tatu hivi usiku..nikawa nimepitia kwenye njia flani ambacho kipo katikati ya shamba kubwa na wakati ule limepandwa mhindi..niseme tu nilikuwa nimetoka kujipumzisha kidogo na marafiki kwa hiyo nilikuwa nimenyonya Guiness mbili hivi..ila nilipoinua macho kuangalia mbele nilishtuka kuna mwanamke mbele yangu na manukato yake nayahisi kabisa..alikuwa mrefu kidogo ana mwili wa kawaida tu nikimaanisha kimaumbile..alionekana kutembea Kama mtu aliyechoka sana kwa hiyo hakuwa anaharakisha..kilichonishangaza ni kwamba nilijitahidi sana kuharakisha nimkaribie yule mwanamke Ila ilishindikana..nikawa ni Kama vile nimesimama kabisa naye akawa bado anatembea..
Ni mambo mengi tu ila kwa sasa ni muda sana sijasikia mambo Kama hayo tena na namshukuru mungu sana..tukio la mwisho lilitokea 2004