Njoo tusimualiane Mambo ya kutisha/kuogopesha uliyowahi kushuhudia hapa Duniani

Nataka nivione mkuu!
 
Picha ya huyo jini mrefu mwanamke wa baharini iko wapi sasa na utuwekee picha yako ulipokamatwa na wasaidizi wa sangoma wako pale ulipokuwa unataka kukimbia kumuhofia yule jini. Tunataka kuthibitisha ukweli wake.
 
Imenikumbusha miaka ya 2000 nikiwa secondary Shule moja mugumu serengeti nilikuwa naenda kusoma masomo ya ziada kwa nyakati za jioni saa 12:00 jioni narud saa nne hadi saa sita usiku, eneo nilikuwa naenda kusoma ni ndani ya uzio wa kanisa fulani. Mara zote nilikuwa nikitoka nafatwa na ndugu zangu wakubwa waliopo nyumbani au nasindikizwa na mwalimu wangu alikuwa ni mwinjilisiti wa dini fulani hapo kanisani maana kuna umbali kidogo kufika nyumbani . Kilichotokeo siku hiyo nilimwambia huyo mwinjilisiti aniache niende home mwenyewe maana ndugu zangu walikawia.

Mwinjilisiti aligoma akasema twende wote nikamwambia nimezoea arudi nitafika alikataa tukafika sehemu nikamwambia arudi nitafika home arudi aligoma, Tulifika njia panda ya kuelekea nyumbani nilichokikuta nilihisi ndio mwisho wangu ila yule mwinjilisiti alinikamata mkono mkono na kunipa ishara ya kuzunguka kile kiumbe nikapita kulia yeye kushoto yeye akiendelea kuongea ila mm akili ilishahama aisee tumefika mbele aliambia je ningekuacha wazazi wako wasigenielewa kama ungekutwa na madhara. Nafika nyumbani nakuta ndugu zangu wanasimulia wameshindwa kunifata wamekuta kiumbe mrefu kwenye eneo ninalopitaga kwenye miti ya migiriveria ikabidi warudi nyumbani. Kesho yule mwinjilisiti alikuja kumwambia mzee nibadili muda wa kwenda masomo ya ziada. Ila kwangu ilikuwa mwisho wa hayo masomo.

Mkasa wa pili nikiwa secondary shule moja nilikuwa mtu wa Sara sana na nikihubiri siku moja niliamka kwenda kusoma na rafiki yangu alikuwa anaitwa Emmanuel nilifika darasani nimetangulia nikawasha socket nilichokiona kwenye darasa nilishituka nikazima taa nikakemea kimoyomoyo nikatoka nje, sikumwambia rafiki yangu kwanini nimetoka nje zaidi nilimwambia ngoja niende bweni fulani nikamwamshe kupanga mmoja aje anipige pindi kumbe niliamua kwenda bwenini nikitafakari nilichokiona sijafika mbali nikasikia kishindo nikajua tayari kumbe ni Emma rafiki yangu alianguka baada ya kushuhudia na alikuja kubebwa na mlinz hadi alipozinduka.

E bhana mm nimeenda kulala bwenini usingiz ukagoma kabsa wanafunzi wote wakiwa wamelala NILISHUHUDIA WAZEE WAKIWA WAMEKAA KWA KUZUNGUKA KATIKATI YA BWENI nikaanza kukemea sina budi kusema jamaa walikuwa na nguvu ya ziada alinifata mzee mmoja na kunishika paji la uso napiga kelele hakuna aliesikia namshika bedmate wangu hageuki baada ya pale niliamshwa kesho saa nne na nilikuwa nikimuulizia imma yupo wapo imma alipona yupo vzur
Ila mashuleni kuna vitu vingi sana tuombee watoto wetu
 
Aisee Pole sana
 
I.Huyo mwinjilisti alikushika mkono ndio mkakizunguka kiumbe? Mlikizungukaje kwa kushikana kama ni kirefu

Au alikushika usikimbie akakuachia mkakizunguka? Na hukukimbia tena? Sio rahisi

II. Hao wazee uliowaona bwenini ndio mwendelezo wa ulichokiona darasani?
 
Umenena sahihi kabisa mike, WO's wengi wanafanya hayo mambo kwaajili ya ulinzi wavue buti salama wakapumzike. Shuguri ipo kwa hawa SNO's (Ensiors)
 
Nakubaliana nawe mike kwa WO's wengi ni kwaajili wavue buti salama kabisa bila maslahi yao kuguswa. Ila kimbinde kiko kwa hawa SGT's (ensiors)

Kuna mmoja tulikuwa nae pale 835 alikuwa anawaingilia sana na MTM's mpaka wakamriport kwa Charlie Oscar lakini hawakupata msaada wowote maana nae alikuwa anamhofia Sana na deals zao walikuwa wanakula pamoja. Alikuwa anaogopeka mpaka alipovua buti ndio mamtm wakapumzika nakushangilia....
 
mbn hujasema hicho kitu ulichokiona darasani? na kwann umwache ima aende wkt umeona kitu kisicho cha kawaida

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
kuvua buti ndo nn afande

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
umewahi kuona paka akipambana na mauzauza?
 
Kuamka unakuta wadogo zangu wamenyolewa nywele na wembe size ya sumuni au shilingi ilikua kawaida sana pale mtaani kwetu sijui walikua wanazifanyia nn wanga πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€ alafu tulikua hatuna habari tunaona poa tuu kama kitu cha kawaida
 
Tulivyokiona alinishika mkono kwa maana nasiweweseke na kukimbia kutokana na mshtuko na kunipa ishara tukakizunguka kile kiumbe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…