Njoo tusimualiane Mambo ya kutisha/kuogopesha uliyowahi kushuhudia hapa Duniani

Njoo tusimualiane Mambo ya kutisha/kuogopesha uliyowahi kushuhudia hapa Duniani

Huyo alikuwa na malengo naye, wewe ukawa chovyachovya. Alikupenda sana, yote alifanya hayo usiondoke. Kabla ya kukusaidia, niambie kwanza ni dini gani ili nikueleze ukafanyaje.

Hizo dude ungekuwa unazijua toka mwanzo ungemtilia ubani kwenye moto zipite kwenye hiyo tarasimu ndiyo uchome moto. Zisingekuwa na nguvu yeyote
Muslim
 
Mtafute Sheikh mwenye kujua visomo vya kutengua uchawi, akusomee ibtwaal sihr..... Au unaweza kujisomea mwenyewe ila unatakiwa uache mambo mschafu yote, uweze kukisoma. Uwe unaswali swala tano
Inshaalah sheikh kusoma mimi sijui labda nimtafute uyo sheikh na sijui nitampata wapi manke wwnfine wanajua kusoma lakin hayo mambo ya lutoa uchaw hawajui
 
Inshaalah sheikh kusoma mimi sijui labda nimtafute uyo sheikh na sijui nitampata wapi manke wwnfine wanajua kusoma lakin hayo mambo ya lutoa uchaw hawajui
Ibtwaal sihri ni hizi:

Ayatul kursiyu×3
Suratul Az-Zilzallah×3
Suratul Ikhlaas×3
Suratul Falaq×3
Suratul An-nas×3

Kama unazijua jisomee kwa wiki mbili, ukimtegemea Mungu zaidi
 
Dah imenikumbusha miaka ya 90s nikiwa Tabora wilaya moja hivi kijijini nikichukua elimu ya msingi shule yetu ilikuwa upande wa magharibi kuna makaburi halafu shule ina miti kibao ya mikaratusi,mikorosho mijohoro mizambarawe na miti fulani hivi inatoa ubani upepo ukipiga inavuma kama gari,

Dah nakumbuka hiyo siku niliamka kwenye kigheto changu pale home kama saa nane hivi mabalamwezi imekubali nje maana ilikuwa wiki ya mwalimu mmoja hivi kusimamia usafi na wechelewaji na ukichelewa unapata bakora za miguuni na lile baridi la kijijini balaa mwanaume mbalamwezi ile nikajua kumekucha nikanawa faster faster hata sikuwastua wazazi ambapo sio kawaida huwa lazima niwaamshe kwenye gheto lao mzee nikanyanyua ufagio mkononi na kidumu cha maji mbio kwenda kabla ya kufika shule kuna kipori fulani lazima ukipite ndio ufike shule mwanaume sikujari japo njiani sikuona mtu yeyote hiyo haikunistua mie nilijona mshindi leo nawahi namba shule,

aisee nimepita chini ya mikorosho na hiyo miti mingine bila kujari nahisi akili haikuwa yangu nakumbuka nafika shule nikakimbilia darasani nafika mlangoni nilichokishuhudia acha niliona moto mkubwa unawaka mule na kuna watu wamekaa kama wako kwenye kikao halafu wote wakaniangalia ila sura sikuziona hapo ndio akili ikarudi kwamba nimezingua niligeuka mbio kurudi home halafu ule upande wa makaburi nilishuhudia watu wakiwa na mguu mmoja wanaruka ruka kwa mstari mbio zangu nilikuwa nahisi kuna kitu nyuma kinanifata kugeuka nyuma niliona mtu mrefu sana kichwa hakionekani ila kavaa vazi refu linag'aa kama mbaramwezi ilivyokuwa inag'aa mwanaume niliongeza speed nilienda nikaingia na mlango mpk ndani yule jini sijui nini nilipokaribia nyumbani nilisikia msonyoo mmoja hatari sana wazazi wakaamka kufungua mlango kuja kunikuta sijitambui wakanichukua nikaenda kulala kwao asubuhi ndio kuwaelezea ni moja ya tukio ambalo huwa sipendi kabisa kulikumbuka maana baada ya hapo mpk leo kuna vitu huwa naviona ambavyo sio vya kawaida na niliwasumbua sana wazazi baada ya hapo . nimejaribu kufupisha ila kuna mambo mengi sana kwa ule usiku na miaka ile niliyashuhudia baada ya ilo tukio.
😃😃😃😃
 
Ilikuwa mwaka 2004 Mzee wetu alihamishiwa kikazi mkoa fulani kanda ya ziwa, ikabidi familia yote tuhamie huko..
Kutokana na uchache wa nyumba za serikali akapangisha nyumba mtaani.

Mzee akapata safari ya kikazi kwa muda, Maza nae akawa chuo mkoa mwingine.. Nikabakia mimi na brother.
Mambo yakaanza, siku ya kwanza tukasikia madirisha ya nyumba yanafunguliwa na upepo mkali unaingia ndani ilikuwa saa nne usiku, tukatoka na mapanga kutafuta mwizi hakuonekana.

Siku ya pili mlango ukafunguliwa na kiumbe kilichoingia kikawa kinafanya shughuli zote tunazofanya mchana mf. Kuwasha radio na kubadili station, kufagia, kufungua fridge nk.

Tulihangaika ikawa kila siku mziki unanza saa mbili usiku, tukawa hatulali.. Akaja mshikaji wake broo akamwambia tukae nje usiku kwenye pembe ya nyumba tutawaona wanaotusumbua.

Tukajipanga tukaenda kukaa, baada kama ya dakika arobani alipita mtu wa kwanza anakimbia kinyume nyume mwendo wake sijapata kuona, baada ya muda akarudi akiwa na mwenzake wakiwa na mwendo wa kawaida tukawatambua kumbe ni baba mwenye nyumba na jirani yetu.

Jambo la kutisha waliamua kutuadhibu baada ya kutugundua tumewaona.. Hivyo tulipigwa ganzi karibia masaa matatu hamna kusogea wala kuongea hata kujikuna. Wao wakaendelea na mambo yao.
😃😃😃😃😃😃
 
😂😂😂 daah noma sana aisee,nimekaa hapa katika kona na stuli na jiwe naona bado,sijui wamenishtukia au sijakaa fresh,kuna mother ana shape wanasema ni mkali wa hizo mambo,akija kinyume nyume sirushi jiwe na enjoy tu
😃😃😃
 
Mi sijawahi shuhudia mauzauza yoyote ila hadi leo nashangaa kuna siku nimeota mama flani hapa mtaani (namjua) alikuwa ananilazimisha kula nyanya,nyanya zilikuwa nyingi sana ananisokomezea mdomoni mimi nameza tu....ajabu nilipokuja kushtuka nikajikuta nimeshiba halafu tumbo limejaa kishenzi yaani
😃😃😃
 
Back
Top Bottom