Njoo ujifunze kukaanga nyama ya bata

Njoo ujifunze kukaanga nyama ya bata

Numbisa

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2016
Posts
301,221
Reaction score
1,172,274
Hawa ni bata wale wafugwao,kama ilivyo kwa kuku bata hawa pia wanauzwa masokoni na wachinjaji hadi wanyonyoaji wapo huko huko sokoni,wananyonyoa na kukukatia katia nyama vizuri,pesa yako tu inaongea.

Nyama yake ni tamu sana hasa ukipatia kumpika vizuri na kumkaanga.

Mahitaji
Nyama ya bata
Tangawizi
Kitunguu swaumu
Chumvi
limao\ndimu
Maji
Mafuta ya kupikia lita moja

Jinsi ya kupika
Osha nyama vizuri weka limao na chumvi,kisha tenga jikoni,maji ya kwanza yakishakaukia weka ya pili kiasi.(hii inasaidia kuilainisha nyama na pia kuondoa mafuta kwa wale wasiopenda mafuta ya bata)

Twanga tangawizi na vitunguu swaumu. Maji ya pili yakishakaukia sio sana,epua sufuria changanya kwenye nyama vitunguu swaumu na tangawizi rusha rusha au geuza geuza kwa mwiko mpaka vichanganyike vizuri.

Tenga kikaangio jikon,weka mafuta ya kukaangia,acha yachemke kisha weka nyama kiasi kaanga mpaka ziwe rangi ya kahawia zinakua zimeshakaangika vizuri,toa kwenye mafuta weka kwenye chombo safi,fanya hivyo kwa nyama zote.

Baada ya hapo nyama yako itakua tayari kwa kuliwa unaweza kula kwa ndizi,chips,wali,ugali,pilau nakadhalika

Vitunguu swaumu na tangawizi zinaleta harufu nzuri na ladha murua
images(3).jpg

Unaweza kufanya hivi pia kwa nyama ya kuku etc
 
Jamani wanaume na wanawake wa daslam mnawaza dawa za nguvu za kiume all the time, kulikoni? Mtakuja kulishwa sumu nyie!! [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Sikuwa na maana hiyooo[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]

Mkuu hayo maneno "za kiume" umenilisha.
 
Waooooo! ngoja nimpe wifi yako asome hii kitu!
Nitaleta mrejesho
 
Hahahah lakin wewe,naliona la kawaida tamu likishushiwa kwa thoda
Hips lake unalionaje?
Tabia zake zooote chafu achana nazo... "Enjoy the meat,forget the animal"
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] sema ukweli toka kumoyo ulikusudia kusema nguvu zipi?
Sema

Vya ukweli ukweli nilimaanisha hizi hizi nguvu za "kwenda na kurudi" bila kuchoka..
Maana akichomwa ana style yake ya kukaa kwenye chombo[emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12]
 
Vya ukweli ukweli nilimaanisha hizi hizi nguvu za "kwenda na kurudi" bila kuchoka..
Maana akichomwa ana style yake ya kukaa kwenye chombo[emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12]
Hahaaa!! Ona nmekukamata, kwa hiyo anaongeza uwezo wa kuishughulikia.......!!!
Basi mwororo!!
 
Back
Top Bottom