Isije kuwa Mo ana overprice wachezaji ili aweze kuiba vizuri hapo simba
Mo hatoiba ila ataichukua kabisa simba kuwa mali yake. Hata hapo sasa ilipofikia uongozi wakiambiwa walipe madeni kwa Mo watamlipa nini?
Uongozi wa simba walipaswa kupunguza thamani ya club kwa kumzuia Mo kununua nunua wachezaji wakigeni. Watamzuia vipi?
Wanatakiwa kuwekeza kwa wachezaji wadowafogo, mfano angali wakina Mkude, Ndemla, Shabalala. Hawa ni mfano mzuri unazidisha mshahara tu kwao kila msimu anabaki kundini.
Angalia Messi, Jordi Alba,Sergi Roberto, Busquet, Pedro, Pique, Xavi, Iniesta, Puyol, mfano wa project bomba sana kutokea katika historia ya timu. Ni wachezaji wa gharama ndogo kwa timu na wameleta mafanikio makubwa sana.
Sisi soka kwetu ni burudani, na bado litakuwa burudani tu. Simba ipo kwa ajili ya Mo. Na hatuna ubavu wa kumfukuza Mo hata ulete sheria ipi pale. Simba haijajitegemea, na Mo anaitegemeza kwake kwa style ya kumiliki.
Tubaki kuwa mashabiki, maana hakuna namna, angalia wakati Mo hayupo simba. Simba ni nzuri Mo akiwepo tu. Mo atapata anachostahili kwa sababu anatumia fedha zake kuijenga timu. Ukiacha Mo nani alishasimama kuitetea simba kwa gharama zake kufa na kupona? Jibu ni Mo tu.
Nani mpaka sasa ameshanunua hisa zilizobakia hata kwa 10% ? Hakuna. Acha Mo aendelee tu, Kilomoni funga mdomo.