NMB acheni kutuibia fedha zetu

Ndumbayeye

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2009
Posts
7,413
Reaction score
4,020
Mwezi huu wamekithiri. unahamisha hela kwa mobile inapotea hewani, unajazishwa fomu pale kaunta unaambiwa baada ya masaa 2 utarudishiwa. unakaa siku 8 . baada ya masaa 2 kila saa kila muda unauliza salio na wanakukata. tangazeni kusitisha basi huduma yenu ya mobile
 
Mkuu hiyo shida hata mie nimekumbana nayo nilikuwa natransfer kwenda tigo pesa ili nitume mchango wa harusi, pesa imekatwa nazungushwa tu mara nenda tigo, ukienda tigo wanasema rudi nmb huku pesa haijaingia.
mbaya zaidi kwenye bank statement ya NMB inaonesha kuwa transaction ilikamilika kwenda hiyo namba sasa. yaani hii nchi kila mtu ni jangili kwa nafasi yake
 

Ktk hili NMB ni zero kabisa, ningekuwa na uwezo ningewashauri wadau wote kuacha kutumia huduma hii sbb ni benki inatajirika kwa makato.
 
Wasemeeni bank kuu au kwa Kamisheni ya Ushindani!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…