NMB Bank huduma mtandaoni inahitaji muwe na Watalaamu wa IT

NMB Bank huduma mtandaoni inahitaji muwe na Watalaamu wa IT

GwaB

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2014
Posts
4,291
Reaction score
5,786
Katika hali ya kushangaza NMB mmeamua kufunga kimya kimya matawi kadhaa mliyofungua kwa mbwembwe huko nyuma. Hata mawakala mliowapa ujiko wa kufungua matawi kwa niaba yenu mmewaacha solemba baada ya kuingia gharama kubwa za ujenzi au mmelipana kimya kimya pia?

Siku hizi mmekuja na upepo wa kila huduma kufanyika kupitia mtandao, lakini bado hamjawa mahiri kwenye eneo hilo kwa sababu hata hizi Apps mnazotegemea zinahitaji vijana wa IT wanaofahamu vizuri kazi yao. Ajirini basi wasomi hawa wawasaidie kupelekesha mambo. Kuwategemea hao vijana wa zamani waliobobea ku-balance mahesabu wawe ndio wabobezi kwenye IT, Hamtutendei haki tulioweka hela zetu kwenu. Tangu wameondoka waholanzi, ukweli usemwe mnayumba sana katika kutoa huduma zote tawini na mtandaoni.

Jirekebisheni.
 
Juzi kadi imekataa kutoa hela leo naenda tawini wananambia niende na barua ya mtendaji na kitambulisho[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ukitumia crdb app na Nmb app ni kama vile mbingu na ardhi
Nmb inataka sms verification ili iendelee ku log in , maana yake ni kuwa ukiwa nje ya network ya simcard uliyosajilia , hutaweza kutumia app hiyo ,
App inatakiwa ifanye kazi popote kwenye uwepo wa internet, ukitoka nje ya Tanzania, Nmb app haifanyi kazi.
 
Tangu aondoke Deusdedit Pastory Masuka kwenda CRDB, yan NMB upande wa IT imekuwa mavi mavi
 
Kweli mkuu nimediwnload app yao haieleweki kabisa nikitaka kuingia naambiwa namba unayoingia Nayo sio uliyosajiliwa basi najaribu manamba yote niliyonayo inanigomea naenda tawini nao vichwa vitupu hakuna msaada kifupi ni kero.
 
Back
Top Bottom