NMB wafungua tawi Buhigwe nyumbani kwa Makamu wa Rais

NMB wafungua tawi Buhigwe nyumbani kwa Makamu wa Rais

Camilo Cienfuegos

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2015
Posts
18,960
Reaction score
67,654
Benki ya NMB yazindua tawi jipya Buhigwe nyumbani kwa Makamu wa Rais Philip Mpango.

Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango leo ameipa Benki ya NMB baraka zake na kuzindua Tawi jipya la Benki hiyo Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma na kuipongeza kwa uthubutu na kuwafuata Wananchi popote walipo na kuwaondolea kero Wananchi ambao walikua wanalazimika kusafiri umbali mrefu kufuata huduma hiyo na wengine kulazimika kutunza fedha majumbani.

Tawi hili la NMB Buhigwe ni Tawi la sita la benki hiyo ndani ya Mkoa wa Kigoma na la 229 kwa Nchi nzima ambapo kabla ya kufunguliwa kwake Wananchi kutoka Vijiji kadhaa walilazimika kutembea karibu kilometa 140 kwenda na kurudi katika Wilaya ya Kasulu kufuata huduma za kifedha za Benki.

Tawi la Benki ya NMB linakuwa la kwanza katika wilaya hii ya Buhigwe ambayo sasa imefunguliwa na kutarajiwa kutoa huduma zote za kifedha ikiwemo kufungua akaunti, kuweka na kutoa pesa, mikopo, kubadilisha fedha za kigeni, huduma za bima pamoja na ushauri wa masuala ya kifedha na biashara.
6DA33735-31B5-49BA-9FF5-B9B9E82264A0.jpeg
 
 
Kulikua na ulazima wa kumtaja mheshimiwa? Au kutumia neno nyumbani kwa makamo wa Rais? Mbona ungeandika Kama maandishi yanayosomeka hapo pichani ungeeleweka
 
Benki ya NMB yazindua tawi jipya Buhigwe nyumbani kwa Makamu wa Rais Philip Mpango.

Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango leo ameipa Benki ya NMB baraka zake na kuzindua Tawi jipya la Benki hiyo Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma na kuipongeza kwa uthubutu na kuwafuata Wananchi popote walipo na kuwaondolea kero Wananchi ambao walikua wanalazimika kusafiri umbali mrefu kufuata huduma hiyo na wengine kulazimika kutunza fedha majumbani.

Tawi hili la NMB Buhigwe ni Tawi la sita la benki hiyo ndani ya Mkoa wa Kigoma na la 229 kwa Nchi nzima ambapo kabla ya kufunguliwa kwake Wananchi kutoka Vijiji kadhaa walilazimika kutembea karibu kilometa 140 kwenda na kurudi katika Wilaya ya Kasulu kufuata huduma za kifedha za Benki.

Tawi la Benki ya NMB linakuwa la kwanza katika wilaya hii ya Buhigwe ambayo sasa imefunguliwa na kutarajiwa kutoa huduma zote za kifedha ikiwemo kufungua akaunti, kuweka na kutoa pesa, mikopo, kubadilisha fedha za kigeni, huduma za bima pamoja na ushauri wa masuala ya kifedha na biashara.
View attachment 2678710
Sehemu kama hizo mawakala tu wanatosha
 
Ni wilaya mpya hiyo, hivyo hata kama siyo kwa boss wa Tanganyika, lazima kungefunguliwa tawi la NMB.

Nadhani Nmb wana matawi karibu wilaya zote
 
Barclays na DTB banks wajiandae nikishika hatamu huko juu wake kufungua matawi kwenye chimbuko langu huko mkoa mmoja hivi nami nivimbe
 
Barclays na DTB banks wajiandae nikishika hatamu huko juu wake kufungua matawi kwenye chimbuko langu huko mkoa mmoja hivi nami nivimbe
Barclays na dtb hawawezi, hawana wateja wengi. Nchi hii ni crdb na nmb ndio wanaokimbizana huko wilayani.

Buhigwe imekua wilaya muda kidogo, nmb wamechelewa tu kwenda. Hataa crdb wataenda muda si mrefu
 
Back
Top Bottom