NMB Yazindua Hati Fungani ya Jamii Bond Yenye Thamani ya Shilingi Trilioni.Yavunja Rekodi ya Kijani Bond ya CRDB

NMB Yazindua Hati Fungani ya Jamii Bond Yenye Thamani ya Shilingi Trilioni.Yavunja Rekodi ya Kijani Bond ya CRDB

Nina experience mbaya sana kuhusu kuwekeza pesa kwenye mabenki.

Nakumbuka miaka zaidi ya kumi iliyopita nilijaribu kuwekeza laki tatu hivi katika NBC (malengo akaunti) ili kutest mitambo. Sasa baada ya mwaka mmoja na miezi kadhaa kupita nikafika benki kutaka kucheck trend, nilichokikuta kilinihuzunisha sana. Haya ndio niliyokuta:
1. Niliambiwa siwezi kutoa chochote kwa kuwa akaunti yangu imefungiwa kwa sababu sijaweka pesa mara kwa mara!. (Nilipewa fomu ya kujaza, kuzunguka nayo ofisi kadhaa (ikiwemo za mwajiri wangu), kuweka picha ya passport, kuweka kiasi kisichopungua elfu 5 ili kuifufua)

2. Nikatakiwa kuandika barua ya kuomba kuchukua fedha zangu (faida), kusubiri siku kadhaa ili ombi langu kukubaliwa. Kwa wastani ilinichukua kama wiki mbili hivi.

3. Nilifika benki zaidi ya mara tatu na kila nikifika benki nilitumia zaidi ya masaa mawili ya kusubiria kupewa jibu (hakukuwa na foleni yoyote ya wateja). Njoo kesho, njoo kesho niliizoea!

4. Mwisho wa siku nilifanikiwa kupata pesa zangu kwa mbinde sana, lakini nikiwa nimepata hasara. (Niliwekeza laki tatu na nikaongeza elfu tano ya kuifufua akaunti yangu (jumla 305,000/=) halafu nikaja kuambulia 269,000/=, yaani hasara ya shilingi 36,000/=)
 
Inamaana kwamba banks zikiweka kwenye masoko ya hisa hizi bonds manake wanatafuta pesa yaani kama pesa iddle somewhere wanakushawishi Kwa riba kwamba ukiwapa pesa Zako Kwa mda Fulani utapata riba,wao wanataka pesa zako Ili wakopeshe na wapate faida.

Mfano CRDB wao wanatoa riba ya 10.25% Kwa mwaka Kwa mtu anaeweka pesa kuanzia 100k na wao over the bond life time wamesema wanaseeza pata faidia ya bil.40-50 Kwa kukopesha hizo bil.700 plus mtakazo deposit.

View: https://twitter.com/CRDBBankPlc/status/1706287825677639791?t=kn93NPAAbAN3q9k6kXP9fA&s=19

View attachment 2762066

Halafu ndio hawa wakiingia 18 za mfilisi mkuu kila mteja analipwa mil. 2 hata kama alikuwa na amana za bilioni! Banking sector bado sana; too risky!
 
Dah! Mafisadi na wazee wa 10% watanufaika kweli na hizo bonds.
 
Halafu ndio hawa wakiingia 18 za mfilisi mkuu kila mteja analipwa mil. 2 hata kama alikuwa na amana za bilioni! Banking sector bado sana; too risky!
Hakuna kitu kama hicho
 
Bond za serikali ni nzuri. Ingawa zipo competitive sana na watu private wanapata lakini ni kwa ugumu.
Bondi iwe na faida angalau uweke 50M++++++
Hapo utakula bila jasho kweli.
In all ukitaka kukwepa laana za uzeeni na kuwapa laana za ajabu ajabu watoto wako, wekeza kwenye hii kitu.
 
Niweke million 10 nikapate laki 5 na point si bora nikanunue vidume vya ng'ombe nivinenepeshe
 
Naona banks zimeingia kwenye ushindani wa bonds Kufuatia kuimarika Kwa Biashara ya mikopo yaani watu na kampuni za biashara zinamiminika sana kukopa hivyo banks zinalazimika kutafuta pesa Kwa Ajili ya kukidhi soko la mikopo.

Baada ya CRDB kuzindua Kijani Bond yenye thamani ya Dola za Marekani 300 sawa na zaidi ya bil.700 za Madafu,NMB nao wamekuja na kubwa kuliko inaitwa Jamii Bond ya Trilioni Moja.

Haya kwenu wenye mapesa Yao kama Wastaafu na wengine mnaofikitia muwekeze nini na wapi ,katunzeni mapesa yenu huko kwenye banks.

Kwa hatua hizi ni wazi Uchumi unazidi kufunguka na Biashara zimerejea Kwa Kasi sana.

======

Benki ya NMB hii leo imezindua na kutangaza rasmi dirisha la uwekezaji wa toleo la kwanza la kuuzwa kwa hati fungani iliyopewa jina la hati fungani ya NMB Jamii (NMB Jamii Bond) yenye lengo la kukusanya fedha ambazo zitawezesha utolewaji wa mikopo yenye kuleta matokeo chanya kwenye jamii kupitia miradi ya mazingira, afya, elimu, wanawake na vijana, pamoja na miradi inayolenga kuhakikisha usalama wa chakula.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna akiongea katika halfa ya uzinduzi huo amesema “Lengo letu ni kukusanya Tsh. bilioni 75, tunaishukuru Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) kwa kuruhusu ongezeko la mpaka Tsh. bilioni 25, pia idhinisho la USD million 10 limetolewa, na kuruhusu ongezeko la mpaka USD milioni 5, ambapo jumla inafikia USD milioni 15, itakayouzwa kwa Mashirika na Wawekezaji walioko nje ya Tanzania"

Hati hii fungani ya NMB Jamii imepewa muda wa uwekezaji wa miaka mitatu ambapo Wawekezaji watapata riba ya asilimia 9.5 kwa mwaka na kulipwa mara nne huku kiwango cha chini cha uwekezaji kikiwa ni Shilingi laki tano (500,000) ambapo dirisha hilo la Uwekezaji likitegemewa kufungwa Octoer 27, 2023.

Benki ya NMB pia imezindua programu ya muda wa kati (Multicurrency Medium Term Note – MTN) ya miaka kumi yenye jumla ya Tsh. trilioni moja iliyopewa idhini na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) kwa muda wa miaka 10.

Hafla hiyo imefanyika Jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na Mgeni rasmi Nehemiah Mchechu ambaye ni Msajili Mkuu wa Hazina akiambatana na Mwenyekiti wa Bodi ya NMB, Dkt. Edwin Mhede.
Tufafanulie tafadhali hatui hati fungani
 
Bond za serikali ni nzuri. Ingawa zipo competitive sana na watu private wanapata lakini ni kwa ugumu.
Bondi iwe na faida angalau uweke 50M++++++
Hapo utakula bila jasho kweli.
In all ukitaka kukwepa laana za uzeeni na kuwapa laana za ajabu ajabu watoto wako, wekeza kwenye hii kitu.
Fafanua mkuu..japo kidgo
 
Lki 5 ni kwa miezi 6 kwa maelezo yao hapo juu tena Hao crdb. Maana wameonyesha ukiweka million 100 unapata million 5,125,000 kwa miezi Sita.

Sasa nawaza kwa mimi mfugaji nikaweke million 10 ili nipate laki 5.125 kwa miezi 6 wakati kidume cha ng'ombe kilichohasiwa nikikinunua kwa laki 6 ndani ya hiyo miezi 6 naweza kuja kukiuza kwq million 1.2
 
Back
Top Bottom