Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 11,550
- 40,697
Nina experience mbaya sana kuhusu kuwekeza pesa kwenye mabenki.
Nakumbuka miaka zaidi ya kumi iliyopita nilijaribu kuwekeza laki tatu hivi katika NBC (malengo akaunti) ili kutest mitambo. Sasa baada ya mwaka mmoja na miezi kadhaa kupita nikafika benki kutaka kucheck trend, nilichokikuta kilinihuzunisha sana. Haya ndio niliyokuta:
1. Niliambiwa siwezi kutoa chochote kwa kuwa akaunti yangu imefungiwa kwa sababu sijaweka pesa mara kwa mara!. (Nilipewa fomu ya kujaza, kuzunguka nayo ofisi kadhaa (ikiwemo za mwajiri wangu), kuweka picha ya passport, kuweka kiasi kisichopungua elfu 5 ili kuifufua)
2. Nikatakiwa kuandika barua ya kuomba kuchukua fedha zangu (faida), kusubiri siku kadhaa ili ombi langu kukubaliwa. Kwa wastani ilinichukua kama wiki mbili hivi.
3. Nilifika benki zaidi ya mara tatu na kila nikifika benki nilitumia zaidi ya masaa mawili ya kusubiria kupewa jibu (hakukuwa na foleni yoyote ya wateja). Njoo kesho, njoo kesho niliizoea!
4. Mwisho wa siku nilifanikiwa kupata pesa zangu kwa mbinde sana, lakini nikiwa nimepata hasara. (Niliwekeza laki tatu na nikaongeza elfu tano ya kuifufua akaunti yangu (jumla 305,000/=) halafu nikaja kuambulia 269,000/=, yaani hasara ya shilingi 36,000/=)
Nakumbuka miaka zaidi ya kumi iliyopita nilijaribu kuwekeza laki tatu hivi katika NBC (malengo akaunti) ili kutest mitambo. Sasa baada ya mwaka mmoja na miezi kadhaa kupita nikafika benki kutaka kucheck trend, nilichokikuta kilinihuzunisha sana. Haya ndio niliyokuta:
1. Niliambiwa siwezi kutoa chochote kwa kuwa akaunti yangu imefungiwa kwa sababu sijaweka pesa mara kwa mara!. (Nilipewa fomu ya kujaza, kuzunguka nayo ofisi kadhaa (ikiwemo za mwajiri wangu), kuweka picha ya passport, kuweka kiasi kisichopungua elfu 5 ili kuifufua)
2. Nikatakiwa kuandika barua ya kuomba kuchukua fedha zangu (faida), kusubiri siku kadhaa ili ombi langu kukubaliwa. Kwa wastani ilinichukua kama wiki mbili hivi.
3. Nilifika benki zaidi ya mara tatu na kila nikifika benki nilitumia zaidi ya masaa mawili ya kusubiria kupewa jibu (hakukuwa na foleni yoyote ya wateja). Njoo kesho, njoo kesho niliizoea!
4. Mwisho wa siku nilifanikiwa kupata pesa zangu kwa mbinde sana, lakini nikiwa nimepata hasara. (Niliwekeza laki tatu na nikaongeza elfu tano ya kuifufua akaunti yangu (jumla 305,000/=) halafu nikaja kuambulia 269,000/=, yaani hasara ya shilingi 36,000/=)