Pre GE2025 No reforms, no elections’ yawaweka CHADEMA njiapanda

Pre GE2025 No reforms, no elections’ yawaweka CHADEMA njiapanda

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Malaria 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2023
Posts
6,846
Reaction score
10,288
No reforms, no elections’ yawaweka Chadema njiapanda.

Kampeni inayoratibiwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ya ‘No reforms, no elections’ ikimaanisha “Bila mabadiliko, hakuna uchaguzi”, imewaweka njiapanda baadhi ya viongozi na makada wa chama hicho.

Wanaobaki njiapanda, ni makada ambao kwa namna moja au nyingine wana nia ya kugombea katika uchaguzi mkuu Oktoba 2025 kusaka udiwani, ubunge na hata urais, ambao wanaingia hofu ya kukosa fursa hiyo.

Makada hao hawajui iwapo wajiandae kujitosa kwenye kinyang’anyiro hicho au waendelee kuwa wasikilizia kauli ya chama iliyosisitizwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu, kwamba kwa sasa nguvu kubwa zinaelekezwa kwenye kupigania mabadiliko ya mifumo ya kiuchaguzi na si vinginevyo.

Wakati Chadema ikiendelea kujiuliza na kupigania mabadiliko, vyama vingine vinaendelea na maandalizi ya uchaguzi. Mathalan, ACT Wazalendo kimeshatangaza wanaotaka kuwania udiwani, ubunge, uwakilishi na urais wajitokeze na kutangaza nia.

Tayari Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othuman Masoud ameweka nia kuwania urais Zanzibar na Kiongozi wa chama hicho, Dorothy Semu ametamgaza kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Chama tawala CCM kimekwishapitisha wagombea wake wa uraia; Rais Samia Suluhu Hassan (muungano) na Dk Hussein Ali Mwinyi (Zanzibar). Dk Emmanuel Nchimbi amepitishwa kuwa mgombea mwenza wa Rais wa Tanzania.

Msimamo wa Chadema

Kwa nyakati tofauti Lissu aliyeshika wadhifa huo Januari 22, 2025, amekuwa akisisitiza dhana hiyo, kuwa iwapo hakutakuwa na mabadiliko kwenye mfumo wa kisheria, Chadema itafanya kila linalowezekana kuhakikisha uchaguzi haufanyiki.

“Hatuzungumzii kususuia uchaguzi, hatutasusia bali tutaenda kuwaambia Watanzania, jumuiya ya kimataifa na walimwengu kwamba kama CCM na Serikali hawako tayari kufanya mabadiliko kwenye mfumo wa uchaguzi ili kuwepo chaguzi huru na haki, uchaguzi wa mwaka huu usifanyike kabisa,” alisema Lissu katika moja ya hotuba zake.

Soma Pia: Pre GE2025 - Tundu Lissu: Kauli ya No Reform No Election hatujasema tunasusia Uchaguzi. Tutaongea na Rais Samia lugha atakayoielewa
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025


Majibu ya Serikali

Msimamo huo umemwibua Katibu Mkuu, Wizara ya Katiba na Sheria, Eliakim Maswi ambaye anasema kwa ajuavyo yeye mageuzi yalikwishafanyika.

“Mimi nimeona mageuzi yapo, sasa kama mwenzangu hayaoni, hata ukitwambia hakuna uchaguzi, wewe unayezuia kwani ndiye unayechagua pekee? Uchaguzi unafanywa na wananchi na ndio wanaopiga kura,” amesema Maswi.


Source: gazeti la mwananchi mtandaoni
 
No reforms, no elections’ yawaweka Chadema njiapanda.

Source: gazeti la mwananchi mtandaoni
cha kushangaza zaidi ni pale ambapo,
anaye ielewa agenda hiyo ni mwenyekiti wa chadema Taifa pekeyake,

viongozi na wanachadema wengine ni kama wako confused wameduwaa hawaelewi na hawajui hata nini cha kuhubiri vijiweni kuhusu hilo 🐒
 
cha kushangaza zaidi ni pale ambapo,
anaye ielewa agenda hiyo ni mwenyekiti wa chadema Taifa pekeyake,

viongozi na wanachadema wengine ni kama wako confused wameduwaa hawaelewi na hawajui hata nini cha kuhubiri vijiweni kuhusu hilo 🐒
Ajenda ya LISSU imeshaeleweka kitambo tu
.

Hamna Mabadiliko, hamna uchaguzi


Wajinga wajinga watanguliza matumbo, wanaoona Siasa ni Ajira za ktajiri ndio wanahaha
 
kwa yanayoendelea sasa kwenye siasa za tanzania nimeelewa vizuri kwanini ccm walikuwa na interest sana na uchaguzi wa chadema kuliko kawaida ya ambavyo ingetakiwa kuwa.
 
Ajenda ya LISSU imeshaeleweka kitambo tu
.

Hamna Mabadiliko, hamna uchaguzi


Wajinga wajinga watanguliza matumbo, wanaoona Siasa ni Ajira za ktajiri ndio wanahaha
kwahiyo viongozi na wanachadema walioduwaa na wasioelewa ndio unawaita wajinga right?

najua katika muda usiokua mrefu utawaita hao wasioelewa agenda hiyo isiyo na tija kua ni wasaliti, lakini pia ndio wahujumu wa agenda za chadema, si ndio?🐒
 
kwahiyo viongozi na wanachadema walioduwaa na wasioelewa ndio unawaita wajinga right?

najua katika muda usiokua mrefu utawaita hao wasioelewa agenda hiyo isiyo na tija kua ni wasaliti, lakini pia ndio wahujumu wa agenda za chadema, si ndio?🐒
Wajinga wajinga, sindo hao Timu Mbowe??

Huwez kua na akili timamu alafu ukawa Timu Mbowe
 
kwahiyo viongozi na wanachadema walioduwaa na wasioelewa ndio unawaita wajinga right?

najua katika muda usiokua mrefu utawaita hao wasioelewa agenda hiyo isiyo na tija kua ni wasaliti, lakini pia ndio wahujumu wa agenda za chadema, si ndio?🐒
LISSU ANAJUA NAMNA YÀ KUWASHUGHULIKIA.

LISSU HAJAWAHI KUSHINDWA KWA MANTIKI.
 
LISSU ANAJUA NAMNA YÀ KUWASHUGHULIKIA.

LISSU HAJAWAHI KUSHINDWA KWA MANTIKI.
mbona hawashughulikii sasa?

au ataanza lini kuwashughulikia ipasavyo?

niliwahi kusema uongozi mpya wa chadema utakua na kazi ya kusimamisha na kuengua wanachama tu kwa miaka yote mitano.
.Je,
utekelezaji ndio umeanza rasmi?🐒
 
Fedha za ABDULI mumekula Sasa inabidi mlipe 🤣🤣 unakulaje fedha za mwanaume mwenzio??yaani akuache hivihivi mbowe jiandae kuchunguliwa
 
CCM na vyombo vyenu mnahaha sana na propaganda zenu mfu. Nunueni vyombo vya habari vyote kama mlivyowanunua hao Mwananchi ila jueni tu hamtofanikiwa kuwarubuni Watanzania this time.

Watanzania washawajua na mbinu zenu za kutumia propaganda ili kuwaondoa kwenye hoja za msingi na this time wameamka kweli.

Hicho kipeperushi cha Mwananchi kitaendelea kuwapiga hela zenu na hao wajinga wa TISS ILA Watanzania tumeshasema No Reform No Election!
 
Back
Top Bottom