Elections 2010 NO way, No how, No Slaa!


Wewe umejiandaa kutoelewa make hata wanafunzi darasani wako wa type yako, hivo mi sikushangai. Sasa JK anajua huo uchumi? Mpaka sasa hivi unajua katoa ahadi hewa ngapi? Kwa vile ubongo wako umeuandaa kutoelewa, itakuwa hivyo.
Subiri kesho JK atakachoongea ndo ulinganishe na alichokisema Dr Slaa. Jk tunamjua ni mbumbumbu mzungu wa leli, hata degree yake alipata gentle, mvivu kusoma huyo.
Kesho utapata majibu, ila watu kama wewe huwa wanashabikia upuuzi.
 

Unajua Kanisa lilichelewa kumletea majibu ya maswali hayo.
 

Ushauri wako ni mzuri, LAKINI KATIKA VITU ULIVYOORODHESHA UMESAHAU HELKOPTA YA KUPIGIA KAMPENI.

NAusisahau kuhesabu gharama za helkopta toka kampeni za 2005 (Mbowe) na ule uchaguzi mdogo wa Mara. Nyani haoni kundule!!!!"!

Eti huyo mtu anayetumia gharama hizo kwa kampeni tu NDIO ANATUDANGANYA AKIINGIA IKULU YUPO TAYARI KULA MUHOGO
 

And it is here that I have always had a problem with Willibroad Slaa! Mambo ya kulipua mabomu tuu na bila kutoa au kussuggest viable solutions to the issue he has raised leaves me much to desire from him. Yeye akisikia kitu tuu anaibuaa bomu - sasa, until when? I get a feeling that he sometimes is leaning towards the populist side then the doers side.
 
This is another commedian!!!stupidity shall be entertained in JF.
 

Sina PhD, lakini amini usiamini, swali hilo la elimu nitalijibu vizuri sana kuliko huyu mbumbumbu wa Uchumi. Hii nina hakika 100%.

Hata wanafunzi wa NABOCE watajibu vizuri sana kuliko huyu mtu hatari.

Eti nilitoa mahesabu ya kupata pesa, lakini Bunge ikakataa! Walifanya sahihi kabisa maana sitegemei lolote lile zuri kuhusu uchumi toka kwa huyu mbumbumbu. Kama ushauri wake ni wa maana mbona hakutupa DONDOO katika mdahalo.


NO WAY, NO HOW, NO SLAA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Pole sana Zawadi. Bila shaka ulikuwa unapata kigugumizi kuandika huo utumbo kwa sababu unajua ukweli. Huwezi kumlinganisha Dk Slaa na huyo mgombea wenu; amemuacha kwa mbali sana na ndio maana amekataa mdahalo naye. Kwa ulinganisho Dk Slaa ni kama gari aina ya ROLLSROYCE na JK ni kama BAJAJ. Acha kabisa we Zawadi. Ebo!
 

nDUGU YANGU, zile pumba za Mh Slaa utazi evaluate vipi? Maana nimerudia mara mbili kuzisikiliza hata data moja ya utatuzi wa matatizo hakuna. Data alizonazo ni zile za profesional yake ya kuwa Critical, yaani zimepotea, zimepotea na ...na...na Ufisadi. Anahitaji ngapi hasemi, sasa utaanalyse wapi?

Tuchukulie kuna pesa za ufisadi X sh, na pesa unazohitaji kutoa elimu bure ni Y sh. Tunachotaka kujua kama X sh ni nyingi kuliko Y sh au kinyume chake. Aanze na hapo tu, na wala haichukui zaidi ya dakika 4 kuwaeleza wananchi.

Huyu Mh Slaa si tu kuwa ni MBUMBUMBU katikia uchumi bali KATIKA MAISHA YAKE KWA UJUMLA.

By the way, kwanini aliacha upadre?
 


 
Zawadi,majibu ya wengi hayakulenga kukujibu bali yana moto wa kisiasa.Umuliza swali muhimu lakini majibu ndiyo hayo....
 
Kweli huyu mtu ni kichwa maji, wewe unaamini kweli kuwa dola 1 mil zinatosha kusomeshea wanafunzi tanzania nzima?
Majibu ya swali hilo yanahitajika yawe katika mtiririko ufuatao:
Idadi ya wanafunzi mwaka huu ni...........
Kila mwanafunzi anagharimu sh..........
Jumla ni sh..........
Pesa hiyo tutaitoa hapa sh.......pale sh.......na.....na...
Hivyo ndivyo wizara yake kivuli ya uchumi ilibidi ifanye mahesabu kabla ya kupayuka kwenye majukwaa elimu bure.
Huyu kwenye uchumi ni Mbumbumbu kabisaaaa


ZAWADI NGODA NI MAFANIKIO YA CCM KUTENGENEZA VILAZA(WENYE MAWAZO MGANDO). Kwa faida ya jamvi hayo ya hapo ya Ngoda yanaonyesha kutokujifahamu kwa sababu ya fikira za mgando. Mfano majibu ya DR (wa ukweli) ni mapana ambayo akili finyu au mgando si rahisi kuyatafuna na kupata maana. Bajeti mdala ya serikali ya kivuli sisi wenye ufahamu tuliielewa kuwa ililenga kufanikisha ukusanyaji wa mapato ili mipango iliyopo itekelezwe. Imekuwa ikitupwa kapuni kwa sababu ya kutokuwepo wabunge makini wa ccm.

Kwa kifupi Ngoda po pote ulipo ccm ilishajipata majukumu ya watendaji wa serikali toka 1985. Ushahidi ni pale mgombea wa ccm anaponadi kuahidi mipango ya maendeleo ya serikali kuwa ndizo sera za serkali. Anafika mbali kutoa ahadi za mfukoni za Bilioni 90 kwa miaka mitano.

Wenye zao wanajua woga wa ccm kuwajibishwa. Ndiyo tabia ya mafisadi. Kura yangu ya mabadiliko nataka wawajibishwe kwanza ili njia na ajenda ya maendeleo ifuatwe.

Lakini inawezekana Zawadi anachezea akili za wanajamvi. Ushauri wa bure ajiunge na jamvi la Michuzi
 
Tusubiri hadithi na nadharia za namna dkt.Slaa alivyoshindwa katika uchaguzi.Hawezi kushinda.
Wachawi ni Chadema na mgombea wao.Amejitengezea maadui wengi kwa kushindwa kuzuia mdomo wake.Hakuwa na hekima ya kuomba kura.
Miongoni mwa maadui zake ni wanaCCM ambao hawako tayari kushindwa bila kuonesha upinzani.Ana maadui miongoni mwa watu aliowataja vibaya bungeni,ukweli hauwezi kuwa kupitia mdomo wake pekee.Waislamu nao wanamuona bomu sana.
Huu wakati wa kampeni amejidhihirisha umbumbumbu wake kwa kutaja vitu vyenye utata mpaka viongozi wanaotarajia kufanya naye kazi pindi angeshinda wameshtuka.
 
Watu kama zawadi wana lengo la kupindisha mada ili tuache kujadili mambo ya msingi ya kuingia kwenye utawala mpya na matokeo yake tumjadilili mbumbumbu ambaye hana muda wa kutafakari bali kurukia mambo kama CCM.

DK Slaa ni mtu Makini mno na ndiye anayefaa kuwa rais wetu Baaaasi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 

Pumba nyingine huwa ni Crap
 

Unataka vya bure ni ghali. Ndivyo hivyo vya ccm vya ZAWADI YA UJINGA
 


 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…