CAF Confederation Cup 2018 :
Northern Dynamo vs Mtibwa Sugar
Mtibwa Sugar walivyowasili mjini Victoria ktk visiwa vya Seychelles bahari ya hindi.
Baada ya Mtibwa kuibuka na ushindi mnono wa mabao manne kwa nunge dhidi ya Northern Dynamo nyumbani ktk viwanja vya Chamazi Complex jijini Dar-es-Salaam, Tanzania timu hiyo itaingia uwanjani kucheza mchezo wa pili wa marudiano hapa Seychelles.
Mchezo huo utafanyika leo December 4, 2018 ktk uwanja wa Stade de Linite wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 10,000 uliopo mjini mkuu wa Victoria , Seychelles.
Source : mtibwaofficial
Northern Dynamo 0 – 1 Mtibwa Sugar (68′ Haruna Chanongo)
AGGREGATES
Northern Dynamo 0 – 5 Mtibwa Sugar
Matokeo ya Mwisho ya Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Kombe La Shirikisho Mtibwa Sugar
Kikosi cha Mtibwa Sugar, kimefanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Northern Dynamo katika mchezo wa marudio wa kombe la shirikisho Afrika uliochezwa katika visiwa vya Shelisheli.
Katika mchezo wa kwanza uliochezwa uwanja wa Chamazi, Mtibwa walifanikiwa kushinda kwa mabao 4-0 hivyo mzigo waliokuwa nao Dynamo leo ulikuwa mzito kuweza kufunga mabao 5-0.
Kwa matokeo hayo Mtibwa wanafanikiwa kusonga mbele katika hatua ya kwanza ya michuano hiyo baada ya kufanikiwa kushinda mchezo wa leo ugenini.