Noti mpya hazina ubora?

Inashangaza kuona noti mpya zimetengenezwa lakini zile za zamani hazitoki kwenye mzunguko. Cha ajabu hizi mpya zinachakaa mapema na kuharibika na kuacha zile za zamani. Maeneo ya vijijini wanalia sana na noti ya TSh 500/= ambayo inachomoka kile kinachongaa nakuacha matundu na kusababisha zikataliwe. Noti ni mbovu zinazidiwa ubora na zile za zamani. Baada ya BOT kushtukia hili zile za zamani bado zipo tu. Walijifanya kuchapisha mpya na kupunguza thamani ya noti ili wachakachue. Swali, kama zilipunguzwa ili ziweze kuenea kwenye Wallet, kwa nini wasingepunguza saizi noti hizohizo zikaenea? Serikali inaona aibu kusema kuwa noti mpya wamechemsha , badala yake wameziacha kwenye mzunguko!!!! Hii ni aibu noti mpya hazina ubora. Kwa nini isiwe kashafa? Jk anadanganywa kila sehemu. Hakuna walikombakiza kila kitengo anatendwa tu. Hii ni balaa.
 
Watanzania huwa hatufikr possible outcome tunapoamua kufanya jambo. Na huwa tukiambiwa kitu na Wazungu tuna waamin Prof. Ndulu ajiuzulu kwa kuletea taifa hasarag. Pesa mpya wazitoe kwenye mzunguko tubak na za zaman.
 
Watanzania huwa hatufikr possible outcome tunapoamua kufanya jambo. Na huwa tukiambiwa kitu na Wazungu tuna waamin Prof. Ndulu ajiuzulu kwa kuletea taifa hasarag. Pesa mpya wazitoe kwenye mzunguko tubak na za zaman.

Kweli kabisa mkuu yaani hii ni aibu
 
zitatokaje namtu hela ni chache?
Tumeweka noti nying il kuziba magepu ya mashimo ya ufisadi.

Ivi wakenya wamebadil ln zakwao?
 
Inashangaza bado wanatoa noti za zamani ambazo ni mpya kabisa. Hapa kuna ishu.
 
Yaani inashangaza kwa kweli, kuna kitu hakijakaa sawa hapa. Hawa jamaa wa BOT inabidi watoe maelezo...
 
Mbunge machachari kutoka Mwanza aliwahi kuwaeleza viongozi wa nchi waache kupiga Deal. Nadhani hapo sasa ndo mtajua kuwa hilo lilikuwa Deal la wakubwa wa Ikulu.
 
Hizi noti hazina muda mrefu kwenye mzunguko lakini cha ajabu ni kwamba leo hii kuna noti mpya ambazo zimechoka kiasi kwamba unashidwa kuamini kama ni noti mpya....noti hizi zinachomoka sana ule mkanda wa mng'ao ...kwani point ya kubadili noti hizi ilikuwa nini kama zina mapungufu makubwa kuliko zilizokuwepo....nani alisimamia hii tenda zima ya utengenezaji wa noti mpya...anawajibikaje kama noti zikionesha mapungufu makubwa kiasi hichi kwa kipindi kifupi namna hii...///natoa hoja////
 
Hakika za sasa ni takataka tu, inabidi bora tuendelee na za zamani
 
Kama sababu moja wapo ya kutengeneza noti mpya ni kuziwezesha kuingia na kuenea kwenye Wallet.........wangepunguza umbo tu la noti za zamani ili ziwe ndogo kuliko kuzibadili kabisa. Huu ni wizi kabisa. Noti mpya kwa sasa ndizo za zamani na noti za zamani ndizo mpya!!!!
 
pamoja na udhaifu wa noti hizi watanzania nao hawana heshima na pesa. Hawazitunzi.

Unakuta mtu anachukua hela anazisweka kwenye matiti, au maeneo nyeti, huko zinaloa jasho zinakuwa tepetepe unategemea nini?

Au anauza mkaa, hela zote zitapakaa mkaa, kama muuza samaki toooba pesa yote inanuka samaki.

Acha wale ambao hela wanazikunja kunja kiasi kwamba ili zipite kwenye mashine ya kuhesabia hela lazima ufanye kazi ya ziada kuzinyoosha. Sasa hapo zitaacha kuchakaa kweli?

Tutakapojifunza kutunza hela hata hizi mpya zitadumu.
 
tafuta shiling mia 500 au 1000 kwenye hizi wanazosema mpya,
ni uchafua ambao hata kuuweka mfukoni unajiuliza mara mbili mbili
 
Iyo inaitwa mission accomplished bse walikuwa na lengo fulani wakati waphase out izo za zamani hasa baada ya kudump fake notes sokoni.
 
Watu wameshakula chao taratibu. Only in Tanzania ambako Kiongozi yuko juu ya Sheria. Wizi mtupu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…