Noti mpya hazina ubora?

ndugu kuna upungufu mkubwa wa noti mpya na chakushangaza noti za zamani zinaendelea kutoka mpya wakati ndiyoilitakiwa noti za zamani zipunguwe kwakuwa kuna toleo jipya!. ndugu au noti hizo mpya zililetwa kwa majaribio. naomba mwenye tarifa atujuze.
 
ngoja Gavana akusikie atakuja na term za ajabu ajabu kuchanganya watu, hizo pesa zilikuwa hazifai kabisa
 
Mhe. Benno ndulu Note mpya zimeenda wapi? tunaomba majibu

Ni miezi sasa tokea Bank kuu itoe note mpya lakini cha kushangaza hizi noti hazipatikani mtaani, Je hizi chache zilizopo ziko kwenye TESTING?

Walisema kuwa note ziliibiwa pale Airport wakati zinaingia nchini kwanini jeshi la polisi hajachukua hatua mpaka sasa? Hii ni mbaya kwa Tanzania na uchumi wake

Hii sio kawaida nchi ikiwa inabadilisha note zake, note za zamani kukaa kwenye mzunguko zaidi ya miezi 4.

This is shame to BOT and government

:angry::angry::angry:
 
inaonekana mkakati wa kutoa note mpya haukuwa makini, kuna watu walikurupuka bila ya kufanya research nzuri na mchakato mzuri wa kupata mzabuni mwnye uwezo wa kutoa note zenye ubora, kutokana na ukimya uliopo ni busara kwa Gavana Ndulu kuweka wazi kama hizo note zitahimili au ziondolewe kwny mzunguko
 
wanafanya majaribio kwenye uchumi wetu, utafkiri tz haina washauri wa haya mambo...siasa chafu inaiharibu nchi
 
Huyu Ndullu ni bomu kabisa...Mimi nilitaka aondolewe baada ya ile scandal ya EPA lakini akaachwa na kuna watu wanasema huyu jamaa ni kichwa sana. Huwezi kuwa kichwa sana huku ukidai kutoa rangi kwa noti mpya ni mojawapo ya security measures ili noti hizo zisichakachuliwe. Wameziondoa kimya kimya sijui walitumia mabilioni mangapi kuzichapisha.
 
Noti mpya zipo mkuu mtaani, Juzi nimeziona Loliondo

Loliondo imeharibu sana vichwa vya watu,
Kwani hakuna vitu vingine vya kuwaza mpaka tuwazie Loliondo tuu????????????????????????ebana Rv..Fr Masanilo...na wewe upo kwene list ya Kuwazia Loliondo tuu,Vipi maisha ya watanzania walio maskini????ebana maslahi ya uchumi wa nchi ndio silaha ya kwanza...uongozi...ok...ok
 
KIMEI wa crdb nae alikua analalamika kuwa noti mpya ni kiini macho!benki hawazipati
 
Guangzhou cha mtoto! Kama hujaenda Loliondo fanya hima.

Wewe umeshapita huko na kupata kikombe chako toka kwa Babu? It is a pleasure to see you again. Please try to behave at least for few months...no more bans for Rev hahahahahah LOL!

Have a great day
 

Kiongozi ni wasi wasi hujui matatizo ya Watanzania, Loliondo ndipo ufisadi mkubwa wa nchi yetu ulipoanzia......enzi za sheikh Ally Hassan Mwinyi. Loliondo gate lie kashfa. Babu anatoa tiba midi ya taifa hili lenye wagonjwa na mfumo mbaya wa afya duniani. Mchungaji mtaafu huyo Mwasapila ni nuru ya taifa na mkombozi wa moja wa maadui wa Tanzania.

Nikukumbushe maadui wa taifa la Tanzania

1. Maradhi

2. Ujinga

3. Umasikini

4. Chama cha Magamba - CCM
 
Noti mpya zipo mkuu mtaani, Juzi nimeziona Loliondo

Kuna watu nilidhani wana mawazo mazuri kumbe wanawaza Loliondo kwa babu,sasa watanzania sijui tutafika kweli kwa stail hii mpaka Rev.Fr.Masanilo anakaa akiwaza kikombe babu saa zote.hana cha kuchangia badala yake anatoa ushauri wa watu kwenda Loliondo kuziona Noti Mpya na kunywa Kikombe.
 
Wewe umeshapita huko na kupata kikombe chako toka kwa Babu? It is a pleasure to see you again. Please try to behave at least for few months...no more bans for Rev hahahahahah LOL!

Have a great day

Mkuu I will be the same reverend! Kuna unafiki mkubwa sana JF....it's not related with the beauty of my behaviour.....fanya him a ukapate kikombe. Fikiria mzee mzima baada ya kupata kikombe alitoka na philosophy ya kuvua Magamba.
 
Kwa kweli hazipo, mimi nilizipata mara moja tu kwenye ATM almost two months passed, lakini hazipo tena, kwa kweli ni aibu wanafanyia majaribio kodi zetu, Nyerere wewe kwanini uliondoka??????????
 
Kweli BABU wa Loliondo anatisha mpaka Rev. Masanilo anamfagilia!! Rev. unaposema noti mpya umeziona huko Loliondo una maana gavana Ndullu kaonekana huko kunywa kikombe? Wenzie waliomtangulia wameonekana kwa babu kwahiyo nae itakuwa poa tu; benki inaongozwa na wagonjwa ndio maana uchumi unazorota.
 
Bora hizo noti zikaondolema maana zinazidiwa ubora kwa kiasi kikubwa sana na noti za zamani. Hizi mpya hasa za 500 na 1000 zinapauka vibaya sana tena kwa muda mfupi tu. Nafananisha na uzinduzi wa window vista ambayo ilikuja kupitwa ubora na mtangulizi wake window xp ikawalazimu watalamu kuja na window 7. Kwa kweli binafsi i fill comfortable kuwa na noti za zamani kuliko kuwa na noti mpya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…