November 25 yagombaniwa, Efm/TvE vs Clouds Media

November 25 yagombaniwa, Efm/TvE vs Clouds Media

Yani niende kwenye tamasha la bure nirudi na ngeu???? kwa sisi wapenda burudani na starehe tunapendelea matamasha yenye viingilio tena ikiwezekana bei ikiwa kubwa mana ustaarabu unakuwepo, tunahangaika kutafuta pesa haipaswi kupata mateso wakati wa kuitumia.....wahenga wanasema "bure gharama"
yan mm bure siwez kwenda aisee
huko unashangilia hapa mtu anavuta ganja
mwingne kashka bisi bisi mambo haya ya kijinga siwez kujaribu
 
Mtanange huu ulianza hapo jana pale ambapo TvE/Efm walipotoa tangazo la Ssebo kuzungumza leo na Clouds nao wakapandisha Ruge kuzungumza muda uleule wa Watani wao wa Jadi!

Nimepata butwaa kusikia Efm/TvE watakuwa na tamasha la bure 25th Novemba 2017 ambayo ndio siku Fiesta Dar itafanyika.

Haya sie wajuvi wa mambo husema ngoma bado mbichi...mtoto wa miaka 3 na miezi 8 anamvimbishia babu wa miaka 20.

Hii vita ya kichini chini ni tamu sana na itakuza media za nchi kama wote watakuwa na akili ya ushindani!!!!
"babu" wa miaka 20!!
 
Ni kitu kizuri kuwa na ushindani kwani wasanii watakuwa na uwezo wa kuchagua wapi kuna maslai mazuri na ushindani unakuza ufanisi na ubunifu pongezi kwa Clouds na ETV
 
Kama unahisi wanachofanya EFM/TVE ni fikra za kimsakini utakuwa unachemka...

Mwaka 2013 Lady Jay Dee aliandaa show yake kubwa tu katika ukumbi wa Nyumbani Lounge- Namanga...Ruge na Clouds nao siku hiyohiyo wakaandaa show ya Mwana FA ukumbi wa Makumbusho - Posta kwa lengo la kumkomoa Jide...Hawakufanikiwa kuharibu show ya Jide kwa sababu Jide alipewa support na Profesa Jay, Sir Nature & Wanaume Halisi, Grace Matata, Langa Kileo, M 2 the P, Mr Sugu na Bantu group Band ya Mzee Kalala....Mwana FA yeye alisindikiwa na Mandojo na Domokaya (ambao walipelekwa na Clouds kwa sababu tu walikuwa na beef na Lady Jay dee), Dully Sykes na Kilimanjaro Band ‘wana Njenje’..

Pia kumbuka kwamba kuna kipindi Mr Sugu na Vinega waliandaa tamasha la Antivirus viwanja vya Posta Kijitonyama ...Ruge na Clouds nao wakaandaa lao Leaders...Kijitonyama palifurika na siku hiyo Mbowe, Lissu, Mdee na wabunge wengine wa Chadema walipanda jukwaani...

Iweje leo uwatuhumu Efm/Tve?

Btw; kwenye dunia hii ya soko huria na utandawazi kila mtu/kampuni ana uhuru wa kufanya jambo analoona linafaa mradi tu havunji sheria...Efm/Tve ni vituo ambavyo vinajitangaza katika soko la habari na burudani...Mkakati wanaotumia kujitangaza ni pamoja na kuandaa matamasha ya bure na kutoa zawadi kwa wananchi kwa lengo la kuwavuta wasikilize/kutazama vituo vyao..Angalia matamasha kama Mchizi wangu, Shika ndinga na Muziki mnene au utaratibu wa kurusha matangazo ya moja kwa moja njue ya studio na kukutana na wasikilizaji wao (NJE NDANI)...Udhamini wa BIKO, Coca Cola na Fast Jet unawapa jeuri ya kuyafanya haya matamasha bure....

Sasa hivi EFM wanarusha matangazo yao mikoa ya Dar, Pwani, Mtwara, Mwanza, Mbeya na Tanga wanapatikana na mikoa jirani na hiyo...Muitikio walioupata katika mikoa hiyo ni mkubwa kiasi cha kuwa tishio kwa Clouds ambao matamasha tyao wanatoza viingilio...Umati uliohudhuria uwanja wa Sokoine juzi kwenye tamasha la Muziki mnene ni mkubwa sana sana...

Efm/Tve ni tishio kwa Clouds FM/TV....Clouds inabidi walijue hilo na kujipanga kushindana katika strategies badala ya mafumbo ya Ruge na public sympathy...

Sorry kwa waraka mrefu...

Wakatabahu...

Bala.
mwambie ivi mtenda akitendwa hujihisi kaonewa
 
Nawengine tunaweka tamasha la nyimbo za injili( Gospel music Concert ) siku hiyo hiyo, nimesikia kuwa wasambaa watakuwa na ngoma ya mdumange na kiingilio bure kwa wasambaa wote, kama sio msambaa unaingia kwa buku jero
[emoji28][emoji28][emoji28] mi ntatoa hiyo buku jero hata kama ni Msambaa
 
Usijitoe ufahamu kujisahaulisha hao clouds walipopanga show ya Mwana Fa wakati siku hiyo Ladyjaydee alikuwa na uzinduzi wa albamu yake na wasanii aliowaalika Jide hawakwenda wakaenda show ya clouds
Ndio hapo nnapowachukia clouds! Ni wanafiki sana hawa jamaa, now wanatafuta sympathy kwa raia wakati wanakandamiza wasanii hasa wale wasiokubaliana na malipo ya show zao
 
Hata kama ni Competition hicho wanachotaka kufanya Efm/TVE ni utoto sasa... Kwa style hii maendeleo nchi hii ngumu sana

Inajulikana Fiesta ni brand ya clouds kwa nini usipange ratiba zako tarehe nyingine kama unahamu ya kutupa tamasha la bure? To me that is so low and pathetic! Kama wao ndio walianza kutangaza tarehe basi clouds wasogeze mbele
Wamewahi kumfanyia upuuzi huo jide acha nao wasome no
 
Efm wanainvest katika mabif ya kijinga...

WCB crew tayari wana mgogoro nao .

Watafeli vibaya sana. Wabaki tu na singeli zao.
Endelea kujidanganya E fm hawana bifu ila clouds FM walianza kuwafanyia uhuni enzi zile makonda yupo nao walifanyiwa uhuni ikiwemo ya kusajili watangazaji wa efm like yule masawe mtata
 
Kama mnafuatilia zamani clouds walishawafanyiaga hivi hivi times FM au magic (mtanirekebisha kidogo) walimleta Joe Thomas na wasanii wengine kutoka nje (venue leaders club ) na wao walikuwa wakwanza kutangaza siku ya tukio na clouds baada ya muda wakatangaza kumleta eve na fat Joe (venue viwanja vya posta) ,kusema kweli leaders kulipwaya yaani ile nafasi mnaweza mkaweka magori mkacheza mipira ya miguu ,alafu asubuhi take Gerald hando aliwaponda sana kwenye PB Leo yupo E FM.Clouds watu wafitina huwezi jua waliwafanya nini E FM.
Ilikuwa times fm
 
Uzinduzi wa albam ya ay chini ya management ya earadio ulivurugwa na ujio wa Eve na fat Joe, tofauti ikiwa siku moja
 
Back
Top Bottom