NSSF Mwanza punguzeni urasimu mnawasumbua wateja wenu

NSSF Mwanza punguzeni urasimu mnawasumbua wateja wenu

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Kuna urasimu mkubwa sana kwenye ofisi za NSSF Mwanza ukilinganisha na mikoa mingine, bila kuwa na ndugu au jamaa anayekujua faili lako la mafao linaweza kuzungushwa hata mwaka mzima.

Mimi na wafanyakazi wezangu tuliacha kazi siku moja kwenye kampuni binafsi mimi nikiwa branch ya Mwanza wenzangu wakiwa branch ya Dar. Tulipoacha kazi tulifuata taratibu zote na tukalipwa mkupuo wa kwanza, shida ni kupata mkupuo wa mwisho.

Wenzetu waliofungulia madai yao Dar tayari walilipwa tangu mwezi wa Nne mwaka huu, tuliofungulia Mwanza imekuwa ni danadana tu, ukifika ofisini visingizio ni vingi, utaambiwa malipo yapo tayari lkn bosi wa kuidhinisha kasafiri mara utaambiwa tayari kaidhinisha lkn mje ofisini kuangalia baada ya mwezi, ukienda unaambiwa nendeni baada ya wiki mbili angalieni kwenye akauti zenu, tarehe ikifika unaambiwa nendeni tutawapigia simu.

Sasa ni zaidi ya miezi 6 tunazungushwa huku wenzetu wa Dar tayari wameshasahau kama walikuwa wanadai.

Tunajuta kufungulia madai kituo cha Mwanza, hivi kuna uwezekano wa kuhamisha faili kutoka Mwanza kwenda Dar, au tutakuwa tunapoteza muda zaidi.

Kwa wazoefu wa NSSF tunaomba ushauri.
 
Kuna urasimu mkubwa sana kwenye ofisi za NSSF Mwanza ukilinganisha na mikoa mingine, bila kuwa na ndugu au jamaa anayekujua faili lako la mafao linaweza kuzungushwa hata mwaka mzima.

Mimi na wafanyakazi wezangu tuliacha kazi siku moja kwenye kampuni binafsi mimi nikiwa branch ya Mwanza wenzangu wakiwa branch ya Dar. Tulipoacha kazi tulifuata taratibu zote na tukalipwa mkupuo wa kwanza, shida ni kupata mkupuo wa mwisho.

Wenzetu waliofungulia madai yao Dar tayari walilipwa tangu mwezi wa Nne mwaka huu, tuliofungulia Mwanza imekuwa ni danadana tu, ukifika ofisini visingizio ni vingi, utaambiwa malipo yapo tayari lkn bosi wa kuidhinisha kasafiri mara utaambiwa tayari kaidhinisha lakini mje ofisini kuangalia baada ya mwezi, ukienda unaambiwa nendeni baada ya wiki mbili angalieni kwenye akauti zenu, tarehe ikifika unaambiwa nendeni tutawapigia simu.

Sasa ni zaidi ya miezi 6 tunazungushwa huku wenzetu wa Dar tayari wameshasahau kama walikuwa wanadai.

Tunajuta kufungulia madai kituo cha Mwanza, hivi kuna uwezekano wa kuhamisha faili kutoka Mwanza kwenda Dar, au tutakuwa tunapoteza muda zaidi.

Kwa wazoefu wa NSSF tunaomba ushauri.
 
Pole sana mkuu. Kwani fao la kujitoa limerejeshwa? Kwa ujumla hii mifuko ya hifadhi ya jamii ni ujinga mtupu. Kama ingekuwa mifuko ya hiyari ni watu wachache sana wangejiunga nayo. Serikali ya CCM imekomba fedha kwenye mifuko na kuiacha ikiwa imefilisika matokeo yake ni usumbufu kwa wanachama wasiokuwa na hatia. Mungu anawaona hawa majizi.
 
NSSF ni kikundi cha WAHUNI tu kuanzia kwa Mkurugenzi Mkuu wao Mshomba,mtu una pesa yako imekaa kule haiongezeki maana umeamua kujiajiri baada ya kuacha kuajiriwa,lakini wanakwambia usubiri mpaka miaka 55 ndio wakupe as if wana uhakika utafikisha umri huo,ni kikundi cha kihuni tu
 
Kuna yule dada wa apa reseption ujamaliza kuongea anakwambia nenda chumba namba 1 yule dada nadhan akil yake haiko Timamu hta ujitahid vip kumweleza changamoto yako yeye atasimama naujuaj wake .. kanifanya nmefunga safar kutoka mwanza ad dar wakat kila ktu kngeishia mwanza nkirud mwanza ntamtukana siku nkienda apo
Nampromic..
 
Mama anaupiga mwingi, mama amewafikia watanzania.

Nani kama mama?

Cc: Lucas Mbwa Wa Shamba.
 
Nikufundishe umafia ambao ulinisaidia,nenda Kwa branch Meneja ofisini ukiingia usitoke,mdai Kwa nguvu mwambie au mnataka rushwa?Kwa nguvu.Usipopata msaada njoo uniambie.Mimi nilifanikiwa
 
Kuna yule dada wa apa reseption ujamaliza kuongea anakwambia nenda chumba namba 1 yule dada nadhan akil yake haiko Timamu hta ujitahid vip kumweleza changamoto yako yeye atasimama naujuaj wake .. kanifanya nmefunga safar kutoka mwanza ad dar wakat kila ktu kngeishia mwanza nkirud mwanza ntamtukana siku nkienda apo
Nampromic..
Huyo dada namfahamu kila mtu anamlalamikia
 
Wanasema eti ukiacha haulipwi mpaka ufukuzwe ndio ulipwe ni kweli?
 
Walinisumbua sana zaidi ya miezi 8, hadi nilipowashtaki kwa waziri Ndalichako, walinipigia wenyewe fasta ndani ya siku 4 nikalipwa changu.
 
80% ya madai ni ya vijana na hela wanazodai sidhani hata zinafika milioni mbili, kimsingi ni vibarua ndo waliojazana nssf

Hivi tumeshindwa kweli kutengeneza sustainable employment? Au wanataka vijana wote waende bbt kujifunza kulima nyanya chungu?

Mumepeleka vijana hamas eti kujifunza kilimo au mlipeleka vijana vitani?

Wala hatustiku kwanini wanao dai nssf wengi wao ni vijana? Unamwambia mtu eti wamtunzie fedha asizeeke vibaya mtu hana ajira siatakufa na njaa tu, huko uzeeni atafikaje?
 
Walinisumbua sana zaidi ya miezi 8, hadi nilipowashtaki kwa waziri Ndalichako, walinipigia wenyewe fasta ndani ya siku 4 nikalipwa changu.
Huyu katambi ndio bure kabisa hata hasikilizi shida za watu, yaani kanda ya ziwa hatuna wabunge safari hii tunapiga chini wote tunaanza moja
 
Huyu katambi ndio bure kabisa hata hasikilizi shida za watu, yaani kanda ya ziwa hatuna wabunge safari hii tunapiga chini wote tunaanza moja
Watanzania tunapenda kweli kweli kulalamika bila kuchukuwa hatua. Nakuapia bila kuandamana na kudai mfumo mpya wa uongozi utakaowafanya viongozi kuwajibika zaidi na pale wanaposhindwa wachukuliwe hatua ni bure. Nchi ina matatizo kila kona lakini wananchi ni kama wameridhika kuishi na matatizo huku wakilalamika kichini chini.
 
Huyu katambi ndio bure kabisa hata hasikilizi shida za watu, yaani kanda ya ziwa hatuna wabunge safari hii tunapiga chini wote tunaanza moja
Huyo ndo hakunisaidia kabisa ikabidi nimcheki yule mama Ndalichako alinipa ushirikiano wa kutosha nikapata haki yangu.
 
Back
Top Bottom