NSSF Mwanza punguzeni urasimu mnawasumbua wateja wenu

NSSF Mwanza punguzeni urasimu mnawasumbua wateja wenu

Huyo ndo hakunisaidia kabisa ikabidi nimcheki yule mama Ndalichako alinipa ushirikiano wa kutosha nikapata haki yangu.
Angalau wewe ulipata bahati ya kumuona Ndalichako kuna watanzania wengi hata Dar hawajafika lkn wanamadai yao NSSF sijui watasaidiwaje.
 
Angalau wewe ulipata bahati ya kumuona Ndalichako kuna watanzania wengi hata Dar hawajafika lkn wanamadai yao NSSF sijui watasaidiwaje.
Yaani we acha mkuu, hasa hiyo branch ya mwanza ni uozo mtupu.
 
NSSF ni kikundi cha WAHUNI tu kuanzia kwa Mkurugenzi Mkuu wao Mshomba,mtu una pesa yako imekaa kule haiongezeki maana umeamua kujiajiri baada ya kuacha kuajiriwa,lakini wanakwambia usubiri mpaka miaka 55 ndio wakupe as if wana uhakika utafikisha umri huo,ni kikundi cha kihuni tu
Duh! Mimi ni mhanga lakini kwa hili sikubaliani na wewe....haiwezekani uweke hela usipate faida...tuache kudanganya jamani 😌
 
Kuna urasimu mkubwa sana kwenye ofisi za NSSF Mwanza ukilinganisha na mikoa mingine, bila kuwa na ndugu au jamaa anayekujua faili lako la mafao linaweza kuzungushwa hata mwaka mzima.

Mimi na wafanyakazi wezangu tuliacha kazi siku moja kwenye kampuni binafsi mimi nikiwa branch ya Mwanza wenzangu wakiwa branch ya Dar. Tulipoacha kazi tulifuata taratibu zote na tukalipwa mkupuo wa kwanza, shida ni kupata mkupuo wa mwisho.

Wenzetu waliofungulia madai yao Dar tayari walilipwa tangu mwezi wa Nne mwaka huu, tuliofungulia Mwanza imekuwa ni danadana tu, ukifika ofisini visingizio ni vingi, utaambiwa malipo yapo tayari lkn bosi wa kuidhinisha kasafiri mara utaambiwa tayari kaidhinisha lkn mje ofisini kuangalia baada ya mwezi, ukienda unaambiwa nendeni baada ya wiki mbili angalieni kwenye akauti zenu, tarehe ikifika unaambiwa nendeni tutawapigia simu.

Sasa ni zaidi ya miezi 6 tunazungushwa huku wenzetu wa Dar tayari wameshasahau kama walikuwa wanadai.

Tunajuta kufungulia madai kituo cha Mwanza, hivi kuna uwezekano wa kuhamisha faili kutoka Mwanza kwenda Dar, au tutakuwa tunapoteza muda zaidi.

Kwa wazoefu wa NSSF tunaomba ushauri.
Hebu tujadili hili linalotuhusu wote🏃🏿‍♂️🏃🏿‍♂️ Tusome hii picha na tutafakari kwa pamoja
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-11-02 at 5.46.04 PM.jpeg
    WhatsApp Image 2023-11-02 at 5.46.04 PM.jpeg
    39.1 KB · Views: 15
Kuna urasimu mkubwa sana kwenye ofisi za NSSF Mwanza ukilinganisha na mikoa mingine, bila kuwa na ndugu au jamaa anayekujua faili lako la mafao linaweza kuzungushwa hata mwaka mzima.

Mimi na wafanyakazi wezangu tuliacha kazi siku moja kwenye kampuni binafsi mimi nikiwa branch ya Mwanza wenzangu wakiwa branch ya Dar. Tulipoacha kazi tulifuata taratibu zote na tukalipwa mkupuo wa kwanza, shida ni kupata mkupuo wa mwisho.

Wenzetu waliofungulia madai yao Dar tayari walilipwa tangu mwezi wa Nne mwaka huu, tuliofungulia Mwanza imekuwa ni danadana tu, ukifika ofisini visingizio ni vingi, utaambiwa malipo yapo tayari lkn bosi wa kuidhinisha kasafiri mara utaambiwa tayari kaidhinisha lakini mje ofisini kuangalia baada ya mwezi, ukienda unaambiwa nendeni baada ya wiki mbili angalieni kwenye akauti zenu, tarehe ikifika unaambiwa nendeni tutawapigia simu.

Sasa ni zaidi ya miezi 6 tunazungushwa huku wenzetu wa Dar tayari wameshasahau kama walikuwa wanadai.

Tunajuta kufungulia madai kituo cha Mwanza, hivi kuna uwezekano wa kuhamisha faili kutoka Mwanza kwenda Dar, au tutakuwa tunapoteza muda zaidi.

Kwa wazoefu wa NSSF tunaomba ushauri.

Pole Sana mkuu, NSSF wanaboa Sana. Kupata pesa yako ni kazi Hadi utachoka.
 
Wanasema eti ukiacha haulipwi mpaka ufukuzwe ndio ulipwe ni kweli?

Hata ukifukuzwa hawakupi mpaka wafanye upelelezi Kama umepata ajira sehemu nyingine. Huo upelelezi unaweza kuchukua miaka miwili.
 
Kuna urasimu mkubwa sana kwenye ofisi za NSSF Mwanza ukilinganisha na mikoa mingine, bila kuwa na ndugu au jamaa anayekujua faili lako la mafao linaweza kuzungushwa hata mwaka mzima.

Mimi na wafanyakazi wezangu tuliacha kazi siku moja kwenye kampuni binafsi mimi nikiwa branch ya Mwanza wenzangu wakiwa branch ya Dar. Tulipoacha kazi tulifuata taratibu zote na tukalipwa mkupuo wa kwanza, shida ni kupata mkupuo wa mwisho.

Wenzetu waliofungulia madai yao Dar tayari walilipwa tangu mwezi wa Nne mwaka huu, tuliofungulia Mwanza imekuwa ni danadana tu, ukifika ofisini visingizio ni vingi, utaambiwa malipo yapo tayari lkn bosi wa kuidhinisha kasafiri mara utaambiwa tayari kaidhinisha lkn mje ofisini kuangalia baada ya mwezi, ukienda unaambiwa nendeni baada ya wiki mbili angalieni kwenye akauti zenu, tarehe ikifika unaambiwa nendeni tutawapigia simu.

Sasa ni zaidi ya miezi 6 tunazungushwa huku wenzetu wa Dar tayari wameshasahau kama walikuwa wanadai.

Tunajuta kufungulia madai kituo cha Mwanza, hivi kuna uwezekano wa kuhamisha faili kutoka Mwanza kwenda Dar, au tutakuwa tunapoteza muda zaidi.

Kwa wazoefu wa NSSF tunaomba ushauri.
Hawa watu pamoja na mambo mengine hebu tuwafuatilie kuna vipindi vyao nimeshaona kipindi cha mafao ...faida wanapata
 
Kwanza pale kuna ndugu(mapacha) wa kike, najiuliza walipataje kazi sehemu moja?.
 
Back
Top Bottom