Pre GE2025 Ntobi avuliwa Uenyekiti Mkoa wa Shinyanga kutokana na utovu wa maadili na nidhamu dhidi ya Lissu

Pre GE2025 Ntobi avuliwa Uenyekiti Mkoa wa Shinyanga kutokana na utovu wa maadili na nidhamu dhidi ya Lissu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

mshale21

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2021
Posts
2,126
Reaction score
5,068
Screenshot_20250109_030942_Instagram.jpg

Kamati tendaji ya Kanda ya Serengeti katika kikao chake cha jana Jumatano Januari 08, 2025 kimefikia maamuzi ya kumvua Uongozi Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Shinyanga Bw. Emmanuel Ntobi kutokana na utovu wa nidhamu na maadili ikiwemo kuchafua Viongozi wa Chama chake Kitaifa kupitia mitandao ya Kijamii.

Akizungumza ma JamboTv Usiku huu (Januari 09, 2025) Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la CHADEMA Kanda ya Serengeti Lucas Ngoto ameiambia JamboTv kuwa maamuzi hayo ya Kikao yamefikiwa Kisheria ikiwa ni mara baada ya kumpa fursa ya kuweza kujitetea dhidi ya kauli na maandiko yake kadhaa yasiyokuwa na utu na heshima kwa Viongozi wa Chama Taifa.

Ntobi ambaye pia mwaka 2023 aliwahi kusimamishwa Uenyekiti wake kwa mwaka mmoja kutokana na makosa ya kinidhamu, amejitanabaisha mitandaoni kama muungaji mkono na Mpiga kampeni kwaajili ya Mhe. Freeman Mbowe kuweza kurejea tena madarakani kama Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, amekuwa na mfululizo wa maandiko kadhaa, yenye nia ya kumchafua, kumtweza na kumtusi Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa Mhe. Tundu Lissu ambaye pia ni Mshindani na mgombea mwenza wa Mhe. Mbowe kwenye nafasi ya Uenyekiti wa Chadema taifa kwenye uchaguzi utakaofanyika baadae mwezi huu.

Miongoni mwa kauli zake ni pamoja na kumuita Makamu mwenyekiti huyo kuwa Mropokaji, Mmbea, sambamba na kumtuhumu kufadhili na kuunda kikosi kilichokuwa kinatumia jina la "Sauti ya Wananchi" akishirikiana na watu maarufu mtandaoni na maafisa wa CCM, idara ya usalama wa taifa na Diaspora kwaajili ya kumfitini Mhe. Mbowe

Aidha Ntobi amekuwa akimuhusisha na baadhi ya matendo yasiyofaa kimaadili kupitia maandikio yake akimuhusisha na "Mzungu" hasa pale Mhe. Lissu anapokuwa safarini nje ya nchi kama " Soon ataweka wazi faragha za Mzungu wake" pamoja na "Si tuliwaambia jamaa yenu kakimbilia kwa mtasha wake? kiko wapi?", mwisho wa kunukuu.


============== ==============

JOHN MNYIKA AULIZWA
JamiiForums ilipowasiliana na Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika akasema “Naomba wasiliana na Mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti au Katibu wake kwa kuwa maamuzi hayo ni ya Kanda ya Serengeti na wao ndio watakaosema kama ni taarifa sahihi au sio sahihi.”

UONGOZI WA KANDA WANENA
JamiiForums imewasiliana na Mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti (CHADEMA), Lucas Ngoto amesema:

“Ni taarifa ya kweli, kikao kilifanyika Januari 8, 2025, Shinyanga Mjini, alipewa nafasi ya kujitetea, akatakiwa kuondoka kwenye kikao baada ya hapo ili maamuzi yafanyike ndipo taratibu za maamuzi zikaendelea.

“Maamuzi yameshafanyika, Ofisi ya Katibu inaandaa barua ili imjulishe maamuzi ya kikao, bado hajakabidhiwa majibu rasmi licha ya kuwa maamuzi yameshatoka.”


Pia soma
 

Kamati tendaji ya Kanda ya Serengeti katika kikao chake cha jana Jumatano Januari 08, 2025 kimefikia maamuzi ya kumvua Uongozi Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Shinyanga Bw. Emmanuel Ntobi kutokana na utovu wa nidhamu na maadili ikiwemo kuchafua Viongozi wa Chama chake Kitaifa kupitia mitandao ya Kijamii.

Akizungumza ma JamboTv Usiku huu (Januari 09, 2025) Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la CHADEMA Kanda ya Serengeti Lucas Ngoto ameiambia JamboTv kuwa maamuzi hayo ya Kikao yamefikiwa Kisheria ikiwa ni mara baada ya kumpa fursa ya kuweza kujitetea dhidi ya kauli na maandiko yake kadhaa yasiyokuwa na utu na heshima kwa Viongozi wa Chama Taifa.

Ntobi ambaye pia mwaka 2023 aliwahi kusimamishwa Uenyekiti wake kwa mwaka mmoja kutokana na makosa ya kinidhamu, amejitanabaisha mitandaoni kama muungaji mkono na Mpiga kampeni kwaajili ya Mhe. Freeman Mbowe kuweza kurejea tena madarakani kama Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, amekuwa na mfululizo wa maandiko kadhaa, yenye nia ya kumchafua, kumtweza na kumtusi Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa Mhe. Tundu Lissu ambaye pia ni Mshindani na mgombea mwenza wa Mhe. Mbowe kwenye nafasi ya Uenyekiti wa Chadema taifa kwenye uchaguzi utakaofanyika baadae mwezi huu.

Miongoni mwa kauli zake ni pamoja na kumuita Makamu mwenyekiti huyo kuwa Mropokaji, Mmbea, sambamba na kumtuhumu kufadhili na kuunda kikosi kilichokuwa kinatumia jina la "Sauti ya Wananchi" akishirikiana na watu maarufu mtandaoni na maafisa wa CCM, idara ya usalama wa taifa na Diaspora kwaajili ya kumfitini Mhe. Mbowe

Aidha Ntobi amekuwa akimuhusisha na baadhi ya matendo yasiyofaa kimaadili kupitia maandikio yake akimuhusisha na "Mzungu" hasa pale Mhe. Lissu anapokuwa safarini nje ya nchi kama " Soon ataweka wazi faragha za Mzungu wake" pamoja na "Si tuliwaambia jamaa yenu kakimbilia kwa mtasha wake? kiko wapi?", mwisho wa kunukuu
Safi sana kamatri ya Nidhamu, wameonesha kutenda haki pasipo kuangalia alikuwa chawa wa kigogo!!!
 

Kamati tendaji ya Kanda ya Serengeti katika kikao chake cha jana Jumatano Januari 08, 2025 kimefikia maamuzi ya kumvua Uongozi Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Shinyanga Bw. Emmanuel Ntobi kutokana na utovu wa nidhamu na maadili ikiwemo kuchafua Viongozi wa Chama chake Kitaifa kupitia mitandao ya Kijamii.

Akizungumza ma JamboTv Usiku huu (Januari 09, 2025) Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la CHADEMA Kanda ya Serengeti Lucas Ngoto ameiambia JamboTv kuwa maamuzi hayo ya Kikao yamefikiwa Kisheria ikiwa ni mara baada ya kumpa fursa ya kuweza kujitetea dhidi ya kauli na maandiko yake kadhaa yasiyokuwa na utu na heshima kwa Viongozi wa Chama Taifa.

Ntobi ambaye pia mwaka 2023 aliwahi kusimamishwa Uenyekiti wake kwa mwaka mmoja kutokana na makosa ya kinidhamu, amejitanabaisha mitandaoni kama muungaji mkono na Mpiga kampeni kwaajili ya Mhe. Freeman Mbowe kuweza kurejea tena madarakani kama Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, amekuwa na mfululizo wa maandiko kadhaa, yenye nia ya kumchafua, kumtweza na kumtusi Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa Mhe. Tundu Lissu ambaye pia ni Mshindani na mgombea mwenza wa Mhe. Mbowe kwenye nafasi ya Uenyekiti wa Chadema taifa kwenye uchaguzi utakaofanyika baadae mwezi huu.

Miongoni mwa kauli zake ni pamoja na kumuita Makamu mwenyekiti huyo kuwa Mropokaji, Mmbea, sambamba na kumtuhumu kufadhili na kuunda kikosi kilichokuwa kinatumia jina la "Sauti ya Wananchi" akishirikiana na watu maarufu mtandaoni na maafisa wa CCM, idara ya usalama wa taifa na Diaspora kwaajili ya kumfitini Mhe. Mbowe

Aidha Ntobi amekuwa akimuhusisha na baadhi ya matendo yasiyofaa kimaadili kupitia maandikio yake akimuhusisha na "Mzungu" hasa pale Mhe. Lissu anapokuwa safarini nje ya nchi kama " Soon ataweka wazi faragha za Mzungu wake" pamoja na "Si tuliwaambia jamaa yenu kakimbilia kwa mtasha wake? kiko wapi?", mwisho wa kunukuu
Democracy nchi hii bado ni ndoto. Hayo yanayodaiwa kuwa matusi yako wapi? Kwahiyo Lissu naye karibu atafukuzwa kwa utovu wa nidhamu dhidi ya Ayatollah Mbowe?
 
Back
Top Bottom