Nunua bidhaa kutoka Mataifa 15 ikiwemo USA, UK, UAE na China sasa

Nitumie nafasi hii na mimi kutoa mrejesho wangu kuhusu hii huduma.
Mnamo tarehe 8/12/2017 nilifanya maamuzi ya kutumia hii huduma kwa mara ya kwanza kwa kuwa nilikuwa na hitaji simu aina ya XIAOMI MI5x(China) au MiA1 (global).

Niliwasiliana na Mwl. RCT kwa WhatsApp kama alivyo elekeza katika hii thread. Akanitajia gharama siku hiyo nikafanya malipo kwa mpesa kwenda kwenye Account yake aliyo nipatia.
Nilikuwa na mawazo sana hiyo siku mtu simfahamu halafu nimemtumia kiasi kikubwa cha pesa basi nikajipa moyo. Pia baadhi ya member humu walinitia moyo niwe na imani.

Baada ya siku kama saba Mwl. RCT alinipatia tracking number ambayo hutolewa ilikufuatilia mzigo kila hatua, siku kama tatu mbele nilianza kupata update za shipment ya mzigo wangu.
Ilichukua kama week mbili mzigo kufika dar.

Na kwakuwa nilikuwa dar mzigo wangu nilichukua siku ya jumatano ya tarehe 3/01/2018 PPF TOWER POSTA nikajiridhisha mzigo ndiyo wenyewe, then tukakabidhiana.

Mwl. RCT Mungu akubariki sana kwa uaminifu ulio nao, kwa pesa unazotumiwa ungekuwa na tamaa ungeweza kufanya chochote lakini unathamini kile kidogo unacho kipata kupitia hii huduma yako.
 
Mkuu mimi nahitaji power bank orgn 12000mAh je itanigharim kiasi gani ? Aina ya samsung au xiaomi ikipatikana au zile orgn ambazo wazifahamu waweza nisaidia pili gharama mpk usafirishaji
 
Tafuta hapa ALIEXPRESS .COM kisha nipe link ya bidhaa husika
kiongozi nimependa hii hapa naimani ni nzuri kwa matumizi maana simu yangu ni samsung so nilihitaji ninunue ya samsung nachoomba unisaidie ni manunuzi na usafirishaji jumla niwe na kiasi gani ? ili tuzungumze na nijue ntaipata lini ? baada ya manunuzi
 
Je na kodi inaweza kuwa kiasi gani pili mimi nipo mkoa shinyanga utanisaidia kufanya shipping dar to shy ?
Utatumiwa shinyanga kwa EMS, ambapo utalipia TZS 15,000
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…