Vhagar
JF-Expert Member
- Jun 8, 2015
- 20,550
- 39,949
Kama una pesa za kupoteza yaweza usijali sana.
Wafanya biashara na watoa bidhaa wanafanya kila mbinu kuitaka pesa yako. Wana kila mitego ambayo usipoangalia unaweza kuwa mtumwa wa kununua vitu bila mpango. Matangazo kila station ya redio na tv kupamba bidhaa.
Hii kesi hasa ni kwa bidhaa za elecronics.
Unanunua tv kubwa ya 4k na smart os kwa bei kubwa. Mwisho wa siku huna content yeyote ya 4k unayoitazama kutoka kwenye hiyo tv. Hizo feature za smart ni za kulipia kila mwezi + mabundle bei juu. Toka ununue huna mpango nazo. Kumbe tv ya kawaida na bei stahiki tu ya FHD ingekufaa.
Leo umenunu simu hii kwa million moja baada ya mwaka inatoka aina nyingine kwa millioni mbili. Kisa umesikia kuna vitu flani imeongezewa. Unakuta hata ile kwanza hukuzingatia kwamba features nyingi wala hukua na kazi nazo.
Umeona nguo kisa tu umeipenda unainunua ukizingatia muuzaji amekushawishi. Unavaa mara moja then unaachana nayo inaozea kabatini.
Umepewa ramani na mchoraji ya nyumba umeipenda design tu kijuu juu. inajengwa inawekwa kila makororo mengine huna hata mpango nayo hapo kwako zaidi yamekuongezea gharama zisizo na msingi. Jumba limekuwa kubwa na uko ww tu na mkeo hata hao watoto muda mwingi wako shule.
Ni vyema kukitambua kitu na kuwa na sababu na kitu kabla hujafanya maamuzi kujua je kwanini nakihitaji.Je, kwa mahitaji yangu hiki kitaendana na mimi?
Unaweza nunua kitu cha mamilioni kumbe kwa matumizi yako kifaa cha laki tano tu kingetosha sana.
Wafanya biashara na watoa bidhaa wanafanya kila mbinu kuitaka pesa yako. Wana kila mitego ambayo usipoangalia unaweza kuwa mtumwa wa kununua vitu bila mpango. Matangazo kila station ya redio na tv kupamba bidhaa.
Hii kesi hasa ni kwa bidhaa za elecronics.
Unanunua tv kubwa ya 4k na smart os kwa bei kubwa. Mwisho wa siku huna content yeyote ya 4k unayoitazama kutoka kwenye hiyo tv. Hizo feature za smart ni za kulipia kila mwezi + mabundle bei juu. Toka ununue huna mpango nazo. Kumbe tv ya kawaida na bei stahiki tu ya FHD ingekufaa.
Leo umenunu simu hii kwa million moja baada ya mwaka inatoka aina nyingine kwa millioni mbili. Kisa umesikia kuna vitu flani imeongezewa. Unakuta hata ile kwanza hukuzingatia kwamba features nyingi wala hukua na kazi nazo.
Umeona nguo kisa tu umeipenda unainunua ukizingatia muuzaji amekushawishi. Unavaa mara moja then unaachana nayo inaozea kabatini.
Umepewa ramani na mchoraji ya nyumba umeipenda design tu kijuu juu. inajengwa inawekwa kila makororo mengine huna hata mpango nayo hapo kwako zaidi yamekuongezea gharama zisizo na msingi. Jumba limekuwa kubwa na uko ww tu na mkeo hata hao watoto muda mwingi wako shule.
Ni vyema kukitambua kitu na kuwa na sababu na kitu kabla hujafanya maamuzi kujua je kwanini nakihitaji.Je, kwa mahitaji yangu hiki kitaendana na mimi?
Unaweza nunua kitu cha mamilioni kumbe kwa matumizi yako kifaa cha laki tano tu kingetosha sana.