Nusu Karne na CCM?



Kwa kweli kwa kuliona hilo tuu,sasa naamini CHADEMA kuna vichwa.Hapa nilipo natafuta kijikadi chao CCM walichonitumia eti cha kufungulia matawi hapa ughaibuni nikipige mkasi.Hebu ngoja nikitafute haraka ili nikichane haraka kabla sijasahau........Yaaani inasikitisha mimi baada ya kwenda majita na kuona niliyojione.Kuanzia Kamnyonge (Majita road) hadi bukumi hali inatisha SANA.Wakondya Zitto​
 
Tanzania sio Kenya kama vile ilivyo kuwa Tanzania sio Zambia

...tatizo ni kuwa CCM haina nusu karne toka izaliwe, sasa sijui imekuwa vipi madarakani kwa nusu karne! vinginevyo nusu karne siku hizi ina maana nyingine, na 2008 kutoa 1977 unapata miaka 50.

mtasema, "oooooh kinachojalisha ni ujumbe"!! sawa, hata mie naukubali...lakini usahihi usio doa wa ujumbe pia ni nyeti, @least ktk dunia yangu.🙁

chinks!!
 

Mheshimiwa Zitto,

Nimependa uchambuzi wako na inaonyesha munaanza kujifunza kwa kwenda vijijini.

Nimeguswa na baadhi ya mambo, kwanza umeongelea sana umaskini wa wilaya za Mara, je hivi kule Kigoma ni tofauti? Mimi kila wilaya niliyowahi kupita vijijini ni hoi bin taabani. Kuna jamaa yangu mmoja alipita Kigoma juzi juzi tokea Dar, akasifia ardhi ilivyo mzuri lakini umaskini wa kutisha. Binafsi nilifikiri kwa kuzunguka wilaya za Kigoma tayari unakuwa na picha kamili juu ya jinsi nchi ilivyo nyuma.

Pili mtafanya la maana kama zile wilaya ambazo mnaongoza halmashauri mtazitumia kama show case, kwa maana ya kwamba hizo wilaya zitakuwa na maendeleo makubwa kuliko wilaya za CCM.

Tatu, watu wengi sasa wanajua makosa ya CCM, kinachowasumbua watu ni huo upande wa pili, je nyie mkipata madaraka mtafanya nini? Naona katika mijadala yenu hicho ndio kinakosekana, sawa ni vizuri kukosoa lakini pia ni vizuri zaidi kuja na solutions.

Mafanikio mema kwa mwaka 2010.
 
Zitto; Umenena; kazi nzuri sana; naona mwanga ( light)

Nakuhakikishia na ninaamini mpaka sasa WATZ vijana wasomi karibu wote wako pamoja na chama kama hiki; kwa mitizamao na mikakati ya kisayansi; ila sasa kwa kutumia wasomi inabidi tutafute namna rahisi ya kuwafikishia ujumbe wa namna hii mhimu kwa mstakabali wa taifa letu watu wale uliowataja Mil 12.7 maskini wa kutupwa kwa sasa; maana wale ndio wanaohongwa Tshirt/kofia/khanga/chumvi nk na kudanganyika na kumbuka hawajaeleimika vema; ujumbe wa operation Sangara ni vema ulenge maeneo maalumu; ukisema uzunguke nchi nzima mafuta yataisha na ujumbe hautafika sawa sawa; mfano kuweka mkakati wa kuhakikisha kanda ya ziwa yote inakuwa himaya maalumu ya Chadema; maanake mnawekeza mawazo na mkakati huko mpaka kieleweke kwanza; na kuwa na uhakika kabisa kwa asilimia 80 wa ushindi majimbo yote hayo; then mnatafuta strategic area nyingine; nasema hata siasa za marekani zina maeneo maalumu ya kuanzia kabla hujaenda eneo jingine; maeneo yawe defined ya kuanzia mkakati kama mlivyoanza na kila sehemu ina slogani yake;na mkipeleka operation iishi huko kimkakakati; mambo yakienda sawa; maeneo mengi yatakubalika na kufuata; nashauri msilazimishe kuzunguka nchi nzima; let be strategic maana unaweza kuzunguka nchi nzima then watu wasielewe vema na mwisho wa siku usiambulie chochote; Wabunge zaidiya 150 wanahitajika toka Chadema by 2010; sasa nini kifanyike; ni strategy kama hizo; define area and concetrate

Yangu ni hayo leo

Malunde
 
Mweshimiwa nakubaliana na wewe mia kwa mia;kwamba ccm haina hadhi ya kupewa kipindi kingine cha miaka 5, ila na nyie inabidi muwaeleze wananchi mtafanya nini kama mtapewa nafasi kwa mfano kwenye afya, elimu,miundombinu nk.
Na siyo kubakia nayo kwenye katiba au ilani ya chama tu, kwani si wote wenye uwezo wakupa hizo katiba na ila.
Yote katika yote nakupa big up mkubwa.
 
Asante sana Mheshimiwa Zito,
Tulio wengi tumeshangazwa na Matamshi ya Chiligati, kwamba, kama mwenyekiti wa chama cha chadema au chama chochote cha siasa anaambiwa 'yeye ni nani?' itakuwaje kwa wakulima na wananchi masikini kabisa, siwataminywa ili wafie mbali.

Asante kwa makala yako imekaa makini sana ukizingatia imetoa data kusapoti maelezo yako.

BigUP!

cheers,
 

Zitto:Hongereni sana kwa kazi nzuri!.Fanyeni mambo yenu tofauti na CCM ili muwe kweli chama mbadala!.
 

Chinkala,

Utawala wa CCM unaanzia TANU na ASP. Ni hawahawa wapo madarakani toka 1961 na 1964
 
Mhe. Zitto; hivi tatizo la Tanzania ni kuelewa kiini na kina cha hali ngumu ya maisha ya watu wetu? Au unataka kudokezea kuwa hizo sehemu ulizopita na kuona adha na hali ngumu ya maisha ya watu CCM hawajaona kabisa au hawataki kuona? Yawezekana tatizo letu siyo kuona na kuelewa ugumu wa hali ya maisha?

Kuna ripoti nyingi kuanzia zile za kimataifa na hizo ulizodokezea na nyingine kwenye poverty reduction programs. Yawezekana tatizo letu ni zaidi ya namba na idadi?
 

Upo sahihi kabisa................ Ningependa uniite Zitto, achana na maneno mheshimiwa kaka. Ukipenda Prefix, ndugu is better kwangu
 
Inauma sana tena mno.
Wachache ndo wananufaika sana tena sana.
Wakati umewadia wa kuyapunguza matumbo yao.Angalia wenzetu Zambia Satta anaongoza kwa kura 40,000... za awali Banda yupo nyumba mbali mno ana kura 20,000..
 
Umenikumbusha kauli za mwenyekiti wa CCM na Rais wetu aliyesema kuwa Hajui kwa nini Tanzania ni Maskini. Huyo ni Rais anayesema hivyo
 
Zitto,
Nimeziona sera zenu kule kwenye tovuti ya CHADEMA. Ni nzuri ingawa nyingi kama sio zote ni hizi za CCM. Mlichokifanya ni kukosoa au/na kutoa suluhuhisho pale walipokwama wao. Tatizo kubwa kwa sasa katika Nchi yetu ni UONGOZI. Bahati mbaya kabisa CHADEMA mnao baadhi VIONGOZI wanaoabudu MALI kama ilivyo kwa CCM.
 
Umegusia vema sana matatizo ya taifa letu.
Cha msingi kwa sasa tuunganishe nguvu kwa kuwaelimisha watu zaidi umuhimu wa kubadili utawala uliopo. Ninaamini kwa dhati ccm haistahili tena kututawala kwa sasa. Lazima tujiunge pamoja kuwabadili.

Ninaamini kwenye grass root movement tunaweza kabisa kufikia malengo yetu. Vipi suala la kuwezesha kampeni hizi, chadema ikafungua akaunti watu wakaruhisiwa kuchangia kwa uwezo wao?? Hebu tujaribu tuone kwani rasilimali fedha ni muhimu kufikia watu wengi hasa ukichukulia ubovu wa miundo mbinu yetu.

Watu wa mijini sielewi kwa nini muamkoo wetu uko chini hasa kwa vitendo? Mfano dsm tunaongoza kuwa na wabunge dormant kabisaaaaaaaaaaaaaaa.....
 
Hapa ndo ninapoona uhuru wa fikra, ahsante Zitto
 
ZITTO,
Big up tuko pamoja.
`SLAA FOR PRESIDENCY 2010'.

Ukitaka kupima ukomavu wa kisiasa wa CHADEMA, basi hapo ndipo penye mtihani mkubwa! Slaa can make a better president for this country than Mbowe!

Ila kwa kuwa kuna tabia za ubinafsi kwa wanasiasa wetu, yaani mtu kama Mbowe hawezi kuelewa kabisa mkimwambia hilo!

SLAA FOR PRESIDENCY 2010
 
www.chadema.net

Zitto;

Excuse me plz, huyu jamaa alieuliza hili swali huenda anawatu anawakilisha wewe unasema aende kwenye Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Sawa mimi nitaenda, Je

Hivi wananchi wako wote kule kigoma kaskazini wanapata huu mtandao?

Hvi ni wananchi wangapi wana acess na internet?

Hivi internet ni nani anaeijua zaid yangu mimi na wewe?

Inawezekana mimi na wewe tunajuana lakini nijibu kama hatujuani ili ukomavu wa kisiasa uonekane basi.

ahhaaaaaaaaa
 

Tusibadili mwelekeo wa mada jamani, na pengine tusimsemee Mbowe kwamba hawezi elewa, kwani naamini si yeye anaye jipendekeza kusimama nafasi ya uraisi nadhani kuna mfumo huru wa kupata mgombea ndani ya Chadema, na kama tunaona Slaa anafaa wajibu wetu ni kumsahauri achukue fomu na sisi tumpe sapoti.

Back to the issue, Zitto huu ni mwanzo mzuri, tuna amini 2010 mabadiliko makubwa yatatokea ikiwa ni matunda ya juhudi hizi.
 
Nani amekudaganya kwamba vyama vya upinzani vichochee mabadiliko ya kiuchumi??

wewe hujui Sera ya upinzani TZ uchochezi wa uchumi ni lazima wapewe u Rais na serikali??

Hapo ndipo tatizo kubwa lilipo, na hapo ndipo wanaponifanya nikose imani nao hawa wapinzani. Wao sio malaika, wanaweza kuingia madarakani wakaishia kuwa mafisadi tu. Kama kweli wana nia njema na nchi hii, wawe na njia mbadala ya kupunguza matatizo ya Watanzania.Badala ya kutumia mamilioni kukodishia ma-helkopta, watumieni hizo pesa kuwajengea wananchi, hasa wa vijijini nguvu za kiuchumi.

Wanaweza kuanza kwa kanda, kama vile hiyo kanda ya Ziwa. Kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa kutumia rasimali zilizopo kwenye maeneo wanayoishi kutawafanya wasirubuniwe na khanga, pilau, fulana na vijirushwa wakati wa uchaguzi. Lakini ukienda na sera tu kwa watu ambao hata mlo mmoja kwa siku wanaupata kwa tabu, hawawezi kukuelewa, watamwelewa yule aliyekuja na burungutu la pesa!

Hebu jiulizeni, kwanini mkoa wa Dar es Salaam hauna mbunge hata mmoja wa upinzani wakati ndiko kwenye mwamko mkubwa zaidi wa kisiasa? Wapiga kura walio wengi wa Dar es Salaam ni watu wa kipato cha chini, na hakika nawaambia wanarubuniwa kwa pesa, vitenge, fulana na khanga kama wale wa vijijini tu!

Jipangeni kwa kuanzia kwenye kiini cha tatizo! Kujaza watu kwenye mkutano wa kampeni kwa sababu umekwenda na helkopta halafu ukaondoka na kuwaachia "SERA" huku wakiwa bado wanalala na njaa ni kujidanganya mwenyewe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…