Nyama Special Thread: Jifunze kupika mapishi mbalimbali ya aina tofauti za nyama

Nyama Special Thread: Jifunze kupika mapishi mbalimbali ya aina tofauti za nyama

Michael Amon

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2008
Posts
8,768
Reaction score
3,622
Jinsi ya kupika pweza

MCHUZI+MZITO+WA+PWEZA.jpg


Mahitaji


  • [*=left]70 gram kitunguu swaumu
    [*=left]150 gram kitunguu maji kata kata
    [*=left]150 gram karoti kata vipande vidogo
    [*=left]1 pilipili ya kijani fresh a pili pili mbuzi
    [*=left]1 kijiko kidogo cha chai unga wa korienda au girigilani
    [*=left]200 gram viazi ulaya
    [*=left]10 gram chumvi
    [*=left]150 gram pilipili hoho
    [*=left]160 ml mafuta ya kupikia
    [*=left]70 ml juisi ya limao
    [*=left]500 gram nyanya ya kopo
    [*=left]350 ml Maji
    [*=left]1 kilo ya pweza kata kata vipande vidogo vidogo

Jinsi ya kupika

  1. Weka mafuta katika sufuria kisha acha ya pate moto.
  2. Baada ya hapo weka kitunguu maji kaanga kwa dakika 1 kisha weka kitunguu swaumu kaanga tena kwa dakika 1.
  3. Weka pweza na viazi ulaya kaanga kwa dakika 10 - 15 kwa moto wa wastani.
  4. Kisha weka unga wa korienda, caroti, pili pili hoho, chumvi, pili pili mbuzi, juisi ya limao kaanga kwa muda.
  5. Kisha weka nyanya ya kopo na koroga vizuri kisha weka maji acha ichemke kwa dakika 5 mchuzi upungue pweza wako atakua ameiva.
 
Jinsi ya kupika prawns


prawn_masala.jpg


Mahitaji


  • 1 kg Prawn
  • 5 vitunguu vikubwa chop chop
  • 3 nyanya kubwa za kuiva chop chop
  • 3 kijiko kikubwa cha chakula Ginger-garlich paste
  • 6-7 kijiko cha chakula mafuta ya kupikia
  • 1 kijiko cha chakula Turmeric powder
  • 1 kijiko cha chakula Coriander powder
  • 1/2 kijiko cha chakula Garam Masala
  • 2 kijiko cha chakula maji ya limao
  • 10 gram chumvi
  • 240 ml maji ya baridi
  • majani ya Coriander chopped kwajili ya kupambia

Jinsi ya kupika


  1. Menya prawns wako na uwasafishe vizuri kisha changanya chumvi 10 gram,1/2 kijiko cha chakula turmeric powder, 1 kijiko cha chakula ginger-garlic paste, na maji ya limao na uache kwa muda wa dakika 30.
  2. Kisha pasha moto sufuria weka mafuta ya kupikia, weka kitunguu maji na endelea kukaanga.
  3. Weka ginger-garlic paste na endelea kuchanganya mpaka iwe rangi ya kahawia.
  4. Kisha weka garam masala na nyanya na endela kukaanga mpaka ziive na mafuta yaanze kuonekana kwa juu.
  5. Weka wale prawns uliokua umewaandaa kisha koroga vizuri ichanganyike na funika na mfuniko kwa dakika 4 mapaka 5 kwa moto wa wastani ili isiungue.
  6. Weka maji kiasi na koroga vizuri tena ichanganyike vizuri kabisa na funika kwa dakika 4 na funua ukishaona mchuzi unakua mzito na mafuta yanakuja tena juu, hapo chakula chako k itakua kimeshaiva
 
Jinsi ya kupika nyama ya figo/moyo/maini/firigisi

chef+issa++10.jpg



Mahitaji


  • 500 gram Nyama ya figo/moyo/maini/firigisi
  • 1 kitunguu kikubwa
  • 1 pili pili hoho kubwa
  • 5 gram chumvi
  • 150 gram nyanya ya kopo
  • 20 gram unga wa binzali
  • 1 kijiko kikubwa cha chakula mafuta ya kupikia

Jinsi ya kupika

  1. Kata kata nyama yako ya figo/moyo/maini/firigisi katika vipande vidogo vidogo ili iwe rahisi kuiva, pia kata kata pili pili hoho na kitunguu.
  2. Weka mafuta katika kikaango au sufuria ili yapate moto kisha weka mchanganyiko wako wa kitunguu, pili pili hoho na chumvi kwa wakati mmoja na uukaange kwa dakika 2.
  3. Funika kikaango chako kwa dakika 2 na baada ya dakika 2 funua uangalie chakula kinaendeleaje kisha weka unga wa binzali kwa harufu na ladha nzuri.
  4. Kisha weka nyanya ya kopo na uendelee kukaanga kisha funika sufuria tena kwa dakika 2.
  5. Baada ya dakika 2 funua, chakula chako kitakua kimeiva na tayari kwa kuliwa.
 
#chef mimi napenda sana kupika. Na kwa sababu hiyo napenda sana kujifunza kupika vyakula mbalimbali. Nimekufuatilia kwa masomo yote. Na wikiendi hii nitawapikia familia yangu figo au kamba. Ahsante sana
 
#chef mimi napenda sana kupika. Na kwa sababu hiyo napenda sana kujifunza kupika vyakula mbalimbali. Nimekufuatilia kwa masomo yote. Na wikiendi hii nitawapikia familia yangu figo au kamba. Ahsante sana

Karibu sana mkuu, tafadhali usisite kutuletea feedback ikiwezekana hata kwa picha.
 
Nimependa hayq mapishi

Asante sana mpendwa...tafadhali endelea kufuatilia maana libeneke ndo kwanza linaanza. Natamani niendelee kutupia vitu ila naona usingizi umenizidi nguvu. Acha nipumzike kidogo halafu nikiamka nitaendelea kuteremsha mambo.
 
Jinsi ya kupika samaki wa foil

Chef+Issa+Samaki+foil+kuoka+%284+%29.png


Mahitaji

  • 1 kitunguu maji kikubwa
  • 1 pc limao kubwa
  • 5 gram binzali
  • 5 gram chumvi
  • 5 gram pili pili manga
  • 1 pili pili hoho kubwa
  • 50 gram tomato pest (nyanya ya kopo)
  • kipande cha foil kutokana na ukubwa wa samaki

Jinsi ya kupika

  1. Mtoe magamba samaki wako kisha msafishe vizuri.
  2. Chukua vitunguu, pilipili hoho, maji ya limao, binzali, chumvi, pili pili manga na nyanya ya kopo na uvichanganye vyote kwa pamoja kisha paka mchanganyiko wako kwenye samaki wako pande zote mbili ulizompasua ili mchanganyiko huu uingie vizuri katika nyama. Mabaki ya huo mchanganyiko yaweke tumboni mwa samaki kisha mfunike vizuri na foil na muweke katika oven iliyokwisha pata moto.
  3. Unaweza kumpika katika oven kwa dakika 30 kwenye moto wa degree 200 hadi 250 pia unaweza kumchoma katika jiko la mkaa akiwa na akaiva vizuri kabisa
  4. Baada ya nusu saa samaki wako atakua ameiva na tayari kwa kuliwa.
 
darasa zuri.
hivi kweli prawns ni haramu?
sawa na alivyo nguruwe?
 
Back
Top Bottom