Nyani Ngabu Mjengoni! Interview: Mapenzi, Utajiri&Mali, Marafiki na Maisha ya ugenini.

Nyani Ngabu Mjengoni! Interview: Mapenzi, Utajiri&Mali, Marafiki na Maisha ya ugenini.

Marafiki wa huku uraiani:

Kusema ukweli mimi niko 'picky' sana na pia niko 'mfikiriaji' sana.

Huwa siruhusu kirahisi watu wanijue kiundani hadi niwe nawaamini.

Na hadi nije nimwamini mtu hunichukua muda mrefu sana.

Kwa msingi huo, marafiki wa karibu nilionao huku uraiani ni wale niliosoma nao kuanzia chekechea mpaka shule ya upili.

Kwa bahati nzuri sana nilibahatika kusoma nao shule moja...kuanzia chekechea, msingi, hadi upili.

Hivyo hao nimejuana nao tokea utotoni. Nimecheza nao, nimepigana nao, nimewinda nao ndege, nimefuga nao njiwa, na mengineyo mengi.

Idadi yao hao haizidi vidole vya kiganja kimoja!

Wa mtandaoni:

Kusema ukweli, mtandaoni sijawahi kupata rafiki wa kweli.

Ambao ninao ni washikaji tu.

Siwajui kivile na wao hawanijui hata robo.

Huku kwenye mitandao huwa nipo makini sana kuliko hata umakini wenyewe.
Mimi nikiwa rafiki yako wa mtaani ni vibaya?

Mbuke.
 
niliona apa Jf kwenye comment sikumbuki uzi gani kuwa una mahusiano ya kimapenzi na Malaika je ni kweli.?
 
niliona apa Jf kwenye comment sikumbuki uzi gani kuwa una mahusiano ya kimapenzi na Malaika je ni kweli.?

Mmmh! malaika wa mbinguni ama? Au yule mwanamziki? Nfyuuuuuuuuu! Hata kama Ngabu simjui tofauti na hapa jf ila sidhani kama ni mtu wa kuzoazoa mwanamziki kama yule anaetoka na kila mtu.
 
Mmmh! malaika wa mbinguni ama? Au yule mwanamziki? Nfyuuuuuuuuu! Hata kama Ngabu simjui tofauti na hapa jf ila sidhani kama ni mtu wa kuzoazoa mwanamziki kama yule anaetoka na kila mtu.
watu watakuwa waliunganisha dots kwasababu kuna kipindi alikuwa anafanya show marekani aka kaa uko kama mwaka hivi
 
watu watakuwa waliunganisha dots kwasababu kuna kipindi alikuwa anafanya show marekani aka kaa uko kama mwaka hivi
Kwani Ngabu ndo mtanzania pekee marekani? Akifanya show lazima atoke nae? Watanzania kwa kutunga habari ni balaa.

I
 
Back
Top Bottom