Nyasi kuota kwenye maungio ya pavements

CHIBA One

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2018
Posts
558
Reaction score
2,093
Wakuu,

Naomba msaada, nafanyaje ili kuzuia hii hali ya nyasi kuota kwenye maungio ya paving blocks ambazo zimekwishawekwa?

Kadri mvua zinavyonyesha majani yanastawi sana kwenye maungio inakuwa kama sina pavements kabisa ndani ya Nyumba.

Naamini ntapata msaada juu ya namna ya kutoa nyasi na jinsi ya kuzuia isitokee tena.
 
Kwanza mafundi hawakumwaga mchanga wa kutosha, wamejenga juu ya udongo...na kingine hukuweka lile nailoni kabla hujapanga hizo paving
 
Mkuu kama kazi ULIFANYA ukiwa mbali hapo karatasi hawakuweka chini Ile nyeusi kazi yake ni kuzuia nyasi zisiote
 
Kuna hii material, Damp Proof Membrane (DPM).
Kazi yake kuzuia unyevunyevu toka aridhini na majani nk nk
 

Attachments

  • images.jpeg
    4.7 KB · Views: 12
Kwahiyo mvua zikiisha, tenga hela, ita fundi afumue hizo paving kisha uweke hilo nailoni jeusi kisha mwaga mchanga kisha wZipange upya.

Pole kwa kadhia unayopata.

Wakimaliza tafuta fundi wale uliowapa kazi mara ya kwanza waambie una kazi nyingine unataka kuwapa waje kwanza nyumbani wanunulie vinywaji halafu wawekee viagra nyingi kisha wafungie kwenye chumba wote pamoja kwa siku nzima, jioni wafungulie waambie umepata dharula kazi haipo tena.

Au wasamehe tuu kawaida ya mafundi kulipua kazi.
 
Sidhani kama fundi wa paving anawez kukupigia hesabu ya materials hlf asikwambie kuhusu hiyo nylon,
Sema maboss wetu mnapenda mteremko, kila muda unawaza "nikizubaa fundi atanipiga!"
Issue ya nylon, na compactor machine boss hua haoni umuhimu wake kwamba inamuongezea gharama tu.
 
Nimeona mtu mmoja hapa Dodoma,Nyasi zilikuwa zinaota kama ulivyosema,fundi maiko mmoja akamshauri aanze upya kwa kuzitoa na Kisha kuweka nailoni na baadae ndo pavements ifuate.Ziko vizuri!Mimi sio fundi.
 

Kanunue dawa za kuua magugupulizia,shida inaisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…