Nyerere aliwahi sema “Nilitegemea majitu yenye nguvu ndani ya CCM yangehamia upinzani ili kupambania mabadiliko ya nguvu”

Nyerere aliwahi sema “Nilitegemea majitu yenye nguvu ndani ya CCM yangehamia upinzani ili kupambania mabadiliko ya nguvu”

mavumbi

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2013
Posts
596
Reaction score
328
1. RIP kwa wote waliotangulia, miongoni mwa watu maarufu na wenye ushawishi / mvuto
  • Mrema alihamia upinzani kwa shinikizo la Mwl Nyerere
  • Sumaye alihamia upinzani kutafuta umaarufu alioukuwa akiendelea kuutamani
  • Lowasa alienda kwa kusukumwa na tamaa yake ya Urais
  • Kingunge alihamia huko kufukuzia umaarufu wa uzeeni - alikuwa wapi huko nyuma?
  • Membe aliwakimbia wana CCM wenzie akijua hakubaliki - hadi kuwekewa vikao na CCM
  • Nyalandu alikimbia baada ya kuona mwelekeo unataka kumtafuna kwa madudu yake serikalini.
Wote ilikiuwa maslahi tu. 90% wakarudi CCM, ukiacha Mrema aliyekuwa na mahesabu yake
2. Na huko kwenye upinzani
  • Lipumba kayumba yumba hadi kuyumbisha Chama
  • Walid Kabouru wapi – CCM
  • Hata Masumbuko Lamwai?
3. Nyerere aliwahi sema “Nilitegemea majitu yenye nguvu ndani ya CCM yangehamia upinzani ili kupambania mabadiliko ya nguvu” - maana aliona ili nchi ipige hatua mbele ni lazima kuleta mabadiliko ya msingi ambayo yeye asingeweza kuyaongoza . Lakini hata hivyo, WaTz na hasa wana CCM kwenye nafasi za ushawishi wakawa waoga.

4. Ndio maana MAGUFULI akajijengea umaarufu – na tutaendelea hivyo hadi aje MAGUFULI mwengine ndani ya CCM
 
Back
Top Bottom