Nyerere na Harakati za Ukombozi wa Bara la Afrika

Nyerere na Harakati za Ukombozi wa Bara la Afrika

Tatizo lako ahali yangu ni kuwa unachambua sana KISIASA na sio KIUCHUMI.

Kumbuka umasikini wenu hauhusiani kabisa na SIASA ZENU bali ni UCHUMI WENU. Jaribu kupambanua alifanya nini kuhakikisha uchumi wenu unajengeka na kuwa stable?

Naomba nichangie kidogo...
Kuna kitu nahisi tumelishwa na kimejikita fikrani mwetu sisi watu weusi. Siasa, Uchumi na Utamaduni...kama nyanja kuu tatu za maisha ya binadamu!
Tumeaminishwa kwamba, mtu anaweza kuwa mwanauchumi na akawa si mwanasiasa au tamaduni. Yaani ni kusema kuwa Uchumi unaweza kusimama pekee pasi kuwa na Siasa na Utamaduni, au Siasa inaweza kujitegemea yenyewe pasi kuwa na Uchumi wala Utamaduni, vivyo hivyo kwa Utamaduni. Na matokeo ya imani hii ni kutokea kuzaliwa kwa mifumo KINZANI kuongoza njanja hizi tatu! Mfano mdogo leo, ni wazi kuwa HAKUNA muislamu safi kama anaamini katika Demokrasia, vile vile hakuna mkristo safi kama anaamini katika Ubepari, ni sawa na kumkuta mlokole ama jeshini! Leo hii tujiulize, nani hapa haishi Ubepari na Demokrasia? Je, Ukristo na Uislamu wetu tunauweka wapi? Haujafa tu? Je, Mifumo inayoongoza nyanja hzi tatu, INASHABIHIANA ama INAKINZANA? MATOKEO YAKE NI NINI KAMA SI KILA AINA YA UOVU NA UCHAFU TUUSHUHUDIAO LEO? Naita HESABU, zimetushika pabaya, only LOGIC to save us! Ni Mungu tu!
Binafsi naamini...
1. UCHUMI, has got nothing more than Physical and Biological Factors for Human Development.
2. SIASA. Ni mchakato wa kuratibu Uchumi. It is the procces!
3. UTAMADUNI. Ni jinsi/namna ya Uratibishaji wa Uchumi. The way is the the Procces! Mahusiano kati ya Uchumi na Siasa!
Kwa tafsiri hyo, mimi ni mwanasiasa, mwanauchumi na mwanatamaduni pia tangu kuzaliwa!
Labda tu nitamuita mtu mwanasiasa ama mwanauchumi au mwanatamaduni katika uwanja wa FASIHI tu. Kwani huko neno moja laweza beba lukuki ya maana!
*Nikirudi kwenye mada...
Kama alivyosema Mkuu wangu Nicholoas. Ni wazi kuwa mkono hauwezi kukataa kupaka dawa jeraha mguuni, kwani athari zake si kwa mguu tu, bali ni mwili mzima. Mafungamano yetu Afrika, ndiyo yaliyopaswa kutangulizwa kwanza! Huwezi kupona wewe mwanaafrika wa Tanzania, kama mkenya ana mafua. Uganda wakilia njaa, nasi tukakaa kimya, matokeo yake watatumia nguvu kuja kutuibia mifugo mpakani, hatutokubali tutapigana nao...ni VITA-MACHUNGU KOTEKOTE. Chanzo ni KUTOFIKIRIANA, OGOPA sana aina yoyote ya UMIMI, SISI KWANZA, kwani mwisho wake ni MAUMIVU. Ndicho KINACHOTUTOKEA LEO.
Viongozi weledi wachache wa Afrika Nyerere akiwemo, walishayaona haya mapema. HULKA na MATAMANIO yetu ambayo ndio mama wa UBINAFSI, ukapindisha UKWELI-MANTIKI-UTU. Leo tunalilia asali, halikuwa wenyewe tufuga manyigu na kuua nyuki.
Vijana siku hzi tunasema "TUNAONESHWA MATITI YA NYOKA"
HESABU KALI wanaafrika wenzangu. TUUMIZE VICHWA.
Mungu wetu anaita sasa!
 
Usimwamshe aliyelala. Kama mtu hajaona umuhimu wa kulikomboa Afrika kutoka minyororo ya ukoloni ni kupoteza muda bure kujadiliana na mtu kama huyo kwa sababu hata kama utampa darsa halitaingia akilini.
 
Usimwamshe aliyelala. Kama mtu hajaona umuhimu wa kulikomboa Afrika kutoka minyororo ya ukoloni ni kupoteza muda bure kujadiliana na mtu kama huyo kwa sababu hata kama utampa darsa halitaingia akilini.
Mhh! unataka kuniambia kuwa si Nyerere wala washauri wake waliokuwa na uwezo wa kusoma alama za nyakati kuwa ukombozi wa bara zima la Afrika uko njiani?!
 
Mhh! unataka kuniambia kuwa si Nyerere wala washauri wake waliokuwa na uwezo wa kusoma alama za nyakati kuwa ukombozi wa bara zima la Afrika uko njiani?!

Like I said usimwamshe aliyelala. Huo ukombozi ulikuwa unajileta wenyewe? Kamuulize Mugabe.
 
Like I said usimwamshe aliyelala. Huo ukombozi ulikuwa unajileta wenyewe? Kamuulize Mugabe.
Mkuu! angalia nilichoandika mwanzoni kabisa utaona kuwa swali langu linahusu kuwekeza nguvu nyingi namna ile,sijakataa kuwa hakukuhitajika mtu au nguvu za kuupigania.
Nchi karibu zote zilizokuwa huru wakati ule zilitoa michango yao lakini ilikuwa limited, isipokuwa Nyerere tuu! kulikuwa kuna nini nyuma yake??!
 
Ningependa kujua ni sababu gani iliyomfanya Nyerere ajikite zaidi katika juhudi za ukombozi wa bara la Afrika kiasi cha kumfanya atumie muda mwingi, rasilimali za Taifa na maisha ya Watanzania huku ikijulikana wazi kuwa kama vile ambavyo Tanganyika ilipewa Uhuru pamoja na nchi nyingine kabla yake, hivyohivyo nchi nyingine zilizosalia zingepewa tu Uhuru wao wakati ukifika.

Hivi kulikuwa na haja gani kwa Nyerere kujikita namna ile?

Wakati nchi nyingine zikiona hakuna umuhimu wa kuwekeza nguvu nyingi kwenye ukombozi wa Afrika (mfano Wakenya) na kuwa bize katika kuimarisha Uchumi wao Nyerere alikuwa bize kwenye "ukombozi wa Afrika"!(usishangae sasa ni kwa nini Kenya imeipita Tanzania ambayo ilipata Uhuru kabla ya Kenya).

Swali: hivi kweli Nyerere alikuwa ni mpigania Uhuru wa Bara la Afrika? au kuna vitu vingine nyuma ya pazia kama vile ambavyo inatajwa kuwa alikuwa akitumiwa kuwadhibiti wapigania Uhuru?

Tafadhali wajuvyi wa haya masuali nijuzeni.


Jambo moja la msingi ni kujiuliza kwa nini Nyerere alikuwa na itikadi za kusaidia ukombozi bara lote la Afrika?

Tunatakiwa kufahamu kipindi hicho vita baridi vilipamba moto, na khofu ya kuibuka vita vikuu vya tatu vya dunia ilindanda anga la dunia. Viongozi wa kisiasa katika wakati huo kilichofanyika ni kuangalia upande wa kuegemea pindi vita hivyo vikiibuka ili kujenga umoja na kujiimarisha katika kujihami na pia ushirikiano shirikishi kati ya nchi zenye kupigana vita kuwa kitu kimoja bila kusubiri uungwaji mkono baada ya vita kuanza kwa sababu ya kukosa common goals.

Mataifa makuwa kwa wakati huo yalikuwa ni Marekani na USSR ambayo nguvu zao zilitokana na kuunganika kwa nchi mbalimbali na kufanya shirikisho la nchi moja kubwa yenye serikali mbalimbali za state. Siri ya mataifa hayo makubwa kuibuka na nguvu kubwa za kiuchumi na kisiasa kuongoza dunia papo kushindana wenyewe kwa wenyewe kwa kupimana nguvu za kivita nguvu walizopata kwa kuunganisha mataifa kadhaa kuwa taifa moja lenye state kadhaa zenye serikali zao ambazo zilikuwa chini ya serikali kuu. Hali hiyo ndiyo iliyomwibulia Nyerere maswali mazito ambayo yalimfanya awe mtume kwa mataifa ya Kiafrika kuwa na ummoja na pengine kuunganisha bara lote la Afrika kuwa taifa moja kubwa kama ilivyokuwa USSR na USA. Uganda, Msumbiji, Zambia na Zaire walioekana kumwelewa Nyerere katika itikadi hizi ila Kenya iliyoongozwa na Jomo Kenyata ndiyo iliyozua kuwa nchi tata kutokana na kuegemea mataifa ya magharibi zaidi.

Jitihada zote za Nyerere kutumia nguvu kubwa katika ukombozi barani Afrika ajenga ilikuwa kwamba huwezi kuunganisha bara la afrika likawa na kauli moja wakati nchi nyingine ndani ya bara hili zikiwa chini ya utawala wa haya mataifa ya ulaya. Kuna baadhi wa viongozi wa Kiafrika ambao walikuwa na mvuto huo wakiwamo akina NKRUMA, KAUNDA, PATRIC LUMUMBA, SAMORA, MUGABE na baadhi ya wengie ambao sijapata muda wa kufunua makarabasha kupata majina yao. GADAFI alikuja kuwa member wa fikra hizo baadaye nadhani tokana na tofauti za kiitikadi zao na Nyerere zilizomchelewesha kuonyesha msimamo wake mpaka Nyerere alipofariki na kuja kutamka wazi kuhusu kuunga mkono jitihada hizo za Nyerere mazikoni Tanzania.

Kuanza kwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar haikuwa tu iishie hapo, ilikuwa ni mwanzo wa kusogeza mataifa mengi yajiunge na umoja kisha kuendea bara lote la Afria, ndizo ndoto za Nyerere katika ukombozi wa bara hili. Mataifa ambayo yalisheheni ubepari kama Nigeria yalionyesha wazi kutomwunga mkono Nyerere, hali kadhalika Afriaka kusini kwa vile kilikuwa kitovu cha wazungu basi ilikuwa sawa na kupenya msitu ulioshonana usiowahi kupitika na binadamu ndiyo yaliyompata Nyerere.

Mwelekeo wa Nyerere kuiga mfumo wa socialism ni dhahiri kutokana na mataifa mengi ya kiafrika kuwa maskini na kwamba mfumo huo ungesaidia zaidi wafrika kuliko kuegemea nchi za magharibi ambazo zilikuwa na mfumo wa ubepari kwani hali ya kulinyonya utajiri wa bara la Afrika ungeshamiri zaidi na wananchi kubaki maskini. Ingawa mfumo huo unaonekana kusambaratishwa na nguvu za pesa kutoka nchi za magharibi miaka ya karibuni, lakini kwa wakati huo lilikuwa ni jambo muafaka kwa asilimia kubwa kwa vile waafrika wengi walikuwa bado kwa kiasi kukubwa hawajaelimika juu ya mambo yao na nchi ya na namna gani ya kulinda mali na utajiri wa bara hili.

Naweza kuona Nyerere alikuwa na akili kubwa na katu isiyo na ladha ya ubinafsi kwa kufikiria zaidi manufaa ya bara letu la afrika na kuwa ndio champion wa ukombozi wa bara hili makao makuu yakiwa nchini, jijini Dar es Salaam. Ilikwa sana na kusama akili kubwa kuongoza akili ndogo ambayo hata utambuzi wa kinachoongelewa na kufafanuliwa ili kuwa vigumu kuelewa bali kushabikia.

Kwa maoni yangu, sina shaka kwamba lengo la Nyerere lilikuwa wazi na dhahiri kisiasa, kiuchumi, kimapokeo na kiutamaduni wa Mwafrika kutokuwa na mipaka ya nchi bali mipaka ya miisho ya himaya ya ukoo wetu ni pale na ukiingia upande ule ni kwa wale wa ukoo wa madege. Mkoloni ndiye aliyetuharibia hiyo kwamba mtu kwenda upande ule lazima ujulikane unatoka wapi na uwe na makaratasi ya kukutambulisha wakati utamaduni wetu mtu ulikuwa huru kwenda po pote kwa vile sote tulikuwa ndugu tu ila uheshimu machifu wa eneo unakofikia.

Matokea ya mipaka ambayo wakoloni walituwekea ndiyo inayotuibulia kutoelewana na majirani kama itokeavyo mzozo wa Ziwa Nyasa, wakoloni wasingendikishana hayo wenyewe kwa wenyewe mambo haya yasingetusumbua watanzana na wamalawi leo hii.
 
Mkuu! angalia nilichoandika mwanzoni kabisa utaona kuwa swali langu linahusu kuwekeza nguvu nyingi namna ile,sijakataa kuwa hakukuhitajika mtu au nguvu za kuupigania.
Nchi karibu zote zilizokuwa huru wakati ule zilitoa michango yao lakini ilikuwa limited, isipokuwa Nyerere tuu! kulikuwa kuna nini nyuma yake??!
Sideeq,
Hapo sasa naweza kukujibu. Nilikutana na marehemu Abdulwahid Kliest Sykes mwaka 1965 nilipohamia Dar. Alifurahi kusikia natoka kumoja na Mwalimu Nyerere na akaanza kunisimulia uhusiano wake na Mwalimu Nyerere. Aliniambia kitu kimoja kilichomsukuma kumuunga mkono Nyerere ni kwamba alikuwa na "committment" ya ukombozi wa Afrika ikiwemo Afrika kusini. Ni viongozi wachache walioonyesha committment hiyo. Na katika manifesto ya TANU kama sijakosea, ukombozi wa Afrika ulikuwa mojawapo ya nguzo za harakati za uhuru wetu. Sasa unawezaje kuuliza ni kitu gani kilichomsukuma au kulikuwa kuna nini nyuma yake wakati alikuwa anatekeleza manifesto ya chama chake? Mimi nadhani that is one of the gloriest moments of TANU's contributions. Nitakupa mfano mwingine. Niliongea pia na marehemu Machel baada ya Msumbiji kupata uhuru wake. Wakati alipokuwa Tanzania akipigania uhuru alikwenda Kenya kukutana na Kenyatta kuomba msaada wa Landrover. Kenyatta alikataa. Lakini baada tu ya Msumbiji kupata uhuru Kenyatta huyo huyo akajitolea kuipa Msumbiji Landrover 16 huku akitafuta mkataba wa kibiashara. Machel akamkumbusha kuwa wakati alipokuwa anahitaji hizo Landrover Kenyatta alimtupa mkono. Sasa najua una akili nzuri tu. Tafakari.
 
Jitihada zote za Nyerere kutumia nguvu kubwa katika ukombozi barani Afrika ajenga ilikuwa kwamba huwezi kuunganisha bara la afrika likawa na kauli moja wakati nchi nyingine ndani ya bara hili zikiwa chini ya utawala wa haya mataifa ya ulaya. Kuna baadhi wa viongozi wa Kiafrika ambao walikuwa na mvuto huo wakiwamo akina NKRUMA, KAUNDA, PATRIC LUMUMBA, SAMORA, MUGABE na baadhi ya wengie ambao sijapata muda wa kufunua makarabasha kupata majina yao. GADAFI alikuja kuwa member wa fikra hizo baadaye nadhani tokana na tofauti za kiitikadi zao na Nyerere zilizomchelewesha kuonyesha msimamo wake mpaka Nyerere alipofariki na kuja kutamka wazi kuhusu kuunga mkono jitihada hizo za Nyerere mazikoni Tanzania.

Kuanza kwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar haikuwa tu iishie hapo, ilikuwa ni mwanzo wa kusogeza mataifa mengi yajiunge na umoja kisha kuendea bara lote la Afria, ndizo ndoto za Nyerere katika ukombozi wa bara hili. Mataifa ambayo yalisheheni ubepari kama Nigeria yalionyesha wazi kutomwunga mkono Nyerere, hali kadhalika Afriaka kusini kwa vile kilikuwa kitovu cha wazungu basi ilikuwa sawa na kupenya msitu ulioshonana usiowahi kupitika na binadamu ndiyo yaliyompata Nyerere.

Mwelekeo wa Nyerere kuiga mfumo wa socialism ni dhahiri kutokana na mataifa mengi ya kiafrika kuwa maskini na kwamba mfumo huo ungesaidia zaidi wafrika kuliko kuegemea nchi za magharibi ambazo zilikuwa na mfumo wa ubepari kwani hali ya kulinyonya utajiri wa bara la Afrika ungeshamiri zaidi na wananchi kubaki maskini. Ingawa mfumo huo unaonekana kusambaratishwa na nguvu za pesa kutoka nchi za magharibi miaka ya karibuni, lakini kwa wakati huo lilikuwa ni jambo muafaka kwa asilimia kubwa kwa vile waafrika wengi walikuwa bado kwa kiasi kukubwa hawajaelimika juu ya mambo yao na nchi ya na namna gani ya kulinda mali na utajiri wa bara hili.

Naweza kuona Nyerere alikuwa na akili kubwa na katu isiyo na ladha ya ubinafsi kwa kufikiria zaidi manufaa ya bara letu la afrika na kuwa ndio champion wa ukombozi wa bara hili makao makuu yakiwa nchini, jijini Dar es Salaam. Ilikwa sana na kusama akili kubwa kuongoza akili ndogo ambayo hata utambuzi wa kinachoongelewa na kufafanuliwa ili kuwa vigumu kuelewa bali kushabikia.

Kwa maoni yangu, sina shaka kwamba lengo la Nyerere lilikuwa wazi na dhahiri kisiasa, kiuchumi, kimapokeo na kiutamaduni wa Mwafrika kutokuwa na mipaka ya nchi bali mipaka ya miisho ya himaya ya ukoo wetu ni pale na ukiingia upande ule ni kwa wale wa ukoo wa madege. Mkoloni ndiye aliyetuharibia hiyo kwamba mtu kwenda upande ule lazima ujulikane unatoka wapi na uwe na makaratasi ya kukutambulisha wakati utamaduni wetu mtu ulikuwa huru kwenda po pote kwa vile sote tulikuwa ndugu tu ila uheshimu machifu wa eneo unakofikia.

Matokea ya mipaka ambayo wakoloni walituwekea ndiyo inayotuibulia kutoelewana na majirani kama itokeavyo mzozo wa Ziwa Nyasa, wakoloni wasingendikishana hayo wenyewe kwa wenyewe mambo haya yasingetusumbua watanzana na wamalawi leo hii.
Vitendo vyake havikuonyesha kuwa ni mtu ambaye ana nia ya dhati ya kuiunganisha Africa;
-Kauli yake ya kutamani kuikokota Zanzibar na kuizamisha kwenye Bahari ya Hindi.
-Kukataa kukaa meza moja na Rais wa Uganda wa wakati huo Idd Amin.
-Kuruhusu Wakenya kuitwa manyang`au.
-Kushiriki kwake kuigawa Nigeria (Biafra)
Vyote hivi vinatuonyesha kuwa kulikuwa na kitu kingine zaidi ya madai yake ya kuiunganisha Africa.
 
Vitendo vyake havikuonyesha kuwa ni mtu ambaye ana nia ya dhati ya kuiunganisha Africa;
-Kauli yake ya kutamani kuikokota Zanzibar na kuizamisha kwenye Bahari ya Hindi.
-Kukataa kukaa meza moja na Rais wa Uganda wa wakati huo Idd Amin.
-Kuruhusu Wakenya kuitwa manyang`au.
-Kushiriki kwake kuigawa Nigeria (Biafra)
Vyote hivi vinatuonyesha kuwa kulikuwa na kitu kingine zaidi ya madai yake ya kuiunganisha Africa.


Sideeq,
Hapo ndipo ninaposema usimwamshe aliyelala. Kwa sababu inaonekana wewe umeshamhukumu Nyerere kwa fikra zako potofu. Yaani kutaka kuiunganisha kwa dhati Afrika ni kukubali kukaa meza moja na Idd Amin? Kati ya Kenya na sisi nani aliyeanzisha matusi? Njonjo alituita man eat nothing. Ulitaka tukae kimya ili tu tuunganishe Afrika? Nyerere aliigawaje Biafra wakati alijitahidi kuwapatisha Gowon na Ojuku na Gowon akakataa huku mauaji ya Waibo yakiendelea? Leta hoja nyingine au rudi tena makhtaba ukabrush up elimu yako.
 
Sideeq,
Hapo ndipo ninaposema usimwamshe aliyelala. Kwa sababu inaonekana wewe umeshamhukumu Nyerere kwa fikra zako potofu. Yaani kutaka kuiunganisha kwa dhati Afrika ni kukubali kukaa meza moja na Idd Amin?
Hakuwa na sifa za kuiunganisha Afrika basi! alikataa kukaa meza moja na jirani yake tu, angewezaje kuinganisha Afrika nzima?...
Kama vision yake ya kuiunganisha Afrika ni kuwa wote wawe kama yeye basi ujuwe ni mtu aliyekuwa na matatizo makubwa sana ya kiakili.
jasusi said:
Kati ya Kenya na sisi nani aliyeanzisha matusi? Njonjo alituita man eat nothing. Ulitaka tukae kimya ili tu tuunganishe Afrika?
Unafikiri Njonjo aliamka tu na kutamka hayo maneno?
Maneno ya Nyerere ya kudai au kuruhusu Watanzania kufahamishwa kuwa Kenya wamechukua karibu vyote baada ya kuvunjika EAC wakati kulikuwa na makubaliano ya mgawanyo wa mali yaliyosimamiwa na yule raia wa Switzerland yangetosha kukuonyesha kuwa alikuwa ni mtu wa namna gani.
*Na ni muunganishaji gani huyo wa bara zima la Afrika ambaye ni easy provocated namna hiyo...kweli alikuwa na sifa ya kuunganisha Afrika mtu huyu?
jasusi said:
Nyerere aliigawaje Biafra wakati alijitahidi kuwapatisha Gowon na Ojuku na Gowon akakataa huku mauaji ya Waibo yakiendelea?
Hujuwi kuwa Nyerere aliisapoti Biafra kwa mali na watu kujitenga?
Nafikiri kufikia hapa tumeshajiridhisha kuwa Nyerere hakuwa na sifa za kuinganisha Afrika! sasa turudi kwenye swali letu,kitu gani kilichomfanya Nyerere ajikite katika namna ile katika ktk ukombozi wa Afrika?
 
Hakuwa na sifa za kuiunganisha Afrika basi! alikataa kukaa meza moja na jirani yake tu, angewezaje kuinganisha Afrika nzima?...
Kama vision yake ya kuiunganisha Afrika ni kuwa wote wawe kama yeye basi ujuwe ni mtu aliyekuwa na matatizo makubwa sana ya kiakili.Unafikiri Njonjo aliamka tu na kutamka hayo maneno?
Maneno ya Nyerere ya kudai au kuruhusu Watanzania kufahamishwa kuwa Kenya wamechukua karibu vyote baada ya kuvunjika EAC wakati kulikuwa na makubaliano ya mgawanyo wa mali yaliyosimamiwa na yule raia wa Switzerland yangetosha kukuonyesha kuwa alikuwa ni mtu wa namna gani.
*Na ni muunganishaji gani huyo wa bara zima la Afrika ambaye ni easy provocated namna hiyo...kweli alikuwa na sifa ya kuunganisha Afrika mtu huyu?Hujuwi kuwa Nyerere aliisapoti Biafra kwa mali na watu kujitenga?
Nafikiri kufikia hapa tumeshajiridhisha kuwa Nyerere hakuwa na sifa za kuinganisha Afrika! sasa turudi kwenye swali letu,kitu gani kilichomfanya Nyerere ajikite katika namna ile katika ktk ukombozi wa Afrika?

Naona unalo jibu tayari. Siku njema.
 
Hakika ni suala mujarabu sana.

Kwani kwa mtu makini yoyote yule asingeweza kukubali na kuacha watoto wake wanakufa njaa na kuwa mafukara wakti rasilimali zake zote anazitumia kujenga nyuma za jirani zake. HILO HALIINGII AKILINI HATA KIDOGO.

Kifupi naweza kusema NYERERE alipenda sana kujijenga BINAFSI kisiasa na kupenda kusifiwa na wazungu lakin KIUCHUMI ndio chanzo kikuu kwa nchi yake kuwa masikini. KWANI alijenga mifumo mibovu sana kiuchumi.

Poleni sana

Yah! Ni kweli kabisa. Ni bora uwe mbinafsi na mali na anasa na uhuru wako kisha uzungukwe na visirani vinavyotokana na hali ya dhiki za majirani. Utalala kwa amani sana na jino pembe pale utakaposikia kishindo na ukunga nje ya uga wako. Na utasema kelele za jirani hazinizuii kupata lepe la usingizi. Yani mshukuru kwa utulivu uliopo hapo nyumbani kwa sasa japo kuna manyang'au yanayotumia mgongo wa dini na kadhalika zingine kutaka kuchafua hali ya hewa. Laiti mngejua hapa Kenya tu hali ilivyo tete. Ukienda baa walinzi, ukienda supermarket walinzi, ukitaka kupiga picha unakatazwa, sababu za kiusalama. Ukaguzi ni mlo huku. Jirani wa Kenya ni huyu msomali matata. Mwacheni Nyerere atangazwe Mtakatifu.
 
Naona unalo jibu tayari. Siku njema.
Jasusi, nilikuwa na hamu ya kuijadili zaidi mada hii lakini kwa mwelekeo anaoonyesha mleta mada nasikitika kupoteza muda wangu kwa mchango wa hapo juu. Napendelea ushindani wa hoja, hii harufu ya itikadi fulani inatatufikishwa kusikotarajiwa. Siku njema mleta mada and stay blessed.
 
Back
Top Bottom