Nyifwila, nyoka aliyemzuia mwl. JK Nyerere kuvuka daraja la Mungu

Nyifwila, nyoka aliyemzuia mwl. JK Nyerere kuvuka daraja la Mungu

Mnamo karne ya uwepo wa Mrusi hapa nchini, wakati huo Hayati baba wa taifa,Mwl. JK Nyerere alipomruhusu Mrusi awekeze katika ujenzi wa bwawa la kufua umeme katika eneo la Kijungu, maarufu kama DARAJA LA MUNGU, huko Mbeya.

Katika uchunguzi wa awali wa eneo hilo Urusi iligundua kuwa eneo lile lina madini aina ya MERCURY, kulingana na jiografia ya zamani ya Tanzania ilikuwa ni ngumu kwa maeneo yote kufikika kirahisi, Kwa kutumia Mwanya huo mrusi aliacha kazi iliyomleta na akaanza kuchimba madini hayo.

Ishu sasa ikaja kuyavusha ng'ambo kwani palikuwa na mto wa asili ambao uliweza kuvukika kwa kutumia Daraja la Mungu. Warusi walipojaribu kuvuka daraja hili wakiwa na madini nyoka huyu aliwazuia na alikuwa mkali mno.

Wakaamua kujenga daraja upande wa pili na wakaanza kusafirisha madini hayo kwa siri wakitoroshea kwao.

Nyerere alipoona mda umepita bila taarifa yoyote kutoka kwa watu hawa akaamua kwenda lakini alipofika daraja la mungu nyoka yule alimzuia kuvuka, ikabidi atume wasaidizi wake wakaangalie kunaendeleaje huko ng'ambo.

Walitahamaki kukuta daraja limejengwa na ajabu ni kuwa daraja hilo liliishia katika nyumba walipoishi Warusi na hakukuwa na njia inayoendelea Zaidi.

Baada ya taarifa hiyo Nyere aliamuru Warusi waondoke mara moja na kwa sababu hawakuweza tena kubeba madini waliamua kuyaficha kwa kudai wanaweka alama za ardhi(beacon), Nyerere akaamrisha askari waishi nyumba zile na iwepo kambi eneo lile.

Miaka kadhaa baadae Warusi walirud kufuata madini yao lakini walistaajabu walipokuta kuna kambi ya askari hivyo wakarudia mbali.
Porojo za kizamani tu
Hakuna cha Nyifwila wala chochote
 
Mara ya mwisho kumwona ni 2009 ,alimulika nusu saa katka safu za livingstone mounts, mzee mmoja akaniambia kesho usiondoke kuna msiba,maana nilipanga kusafiri,nikaamuuliza why akasema hujamwona yule nyoka?

Asubuhi babu mmoja kafariki kweli,nilishangaa sana
 
Sio nyifwila,ni NYAFWILA,halafu si nyoka kama nyoka wengine,nakumbuka enzi hizo,akipita maeneo yetu ya bush,hapo asubuhi watu au mtu mmoja lazima adanje.

Wazee walikuwa wakituonya sana tusikanyage mafuta ya huyu nyoka,siku hizi hata hapiti wala kuonekana.
KashAbalehe ndio maAnA uMUoni>....
 
Mnamo karne ya uwepo wa Mrusi hapa nchini, wakati huo Hayati baba wa taifa,Mwl. JK Nyerere alipomruhusu Mrusi awekeze katika ujenzi wa bwawa la kufua umeme katika eneo la Kijungu, maarufu kama DARAJA LA MUNGU, huko Mbeya.
Katika uchunguzi wa awali wa eneo hilo Urusi iligundua kuwa eneo lile lina madini aina ya MERCURY, kulingana na jiografia ya zamani ya Tanzania ilikuwa ni ngumu kwa maeneo yote kufikika kirahisi, Kwa kutumia Mwanya huo mrusi aliacha kazi iliyomleta na akaanza kuchimba madini hayo.
Ishu sasa ikaja kuyavusha ng'ambo kwani palikuwa na mto wa asili ambao uliweza kuvukika kwa kutumia Daraja la Mungu. Warusi walipojaribu kuvuka daraja hili wakiwa na madini nyoka huyu aliwazuia na alikuwa mkali mno.
Wakaamua kujenga daraja upande wa pili na wakaanza kusafirisha madini hayo kwa siri wakitoroshea kwao.
Nyerere alipoona mda umepita bila taarifa yoyote kutoka kwa watu hawa akaamua kwenda lakini alipofika daraja la mungu nyoka yule alimzuia kuvuka, ikabidi atume wasaidizi wake wakaangalie kunaendeleaje huko ng'ambo.
Walitahamaki kukuta daraja limejengwa na ajabu ni kuwa daraja hilo liliishia katika nyumba walipoishi Warusi na hakukuwa na njia inayoendelea Zaidi.
Baada ya taarifa hiyo Nyere aliamuru Warusi waondoke mara moja na kwa sababu hawakuweza tena kubeba madini waliamua kuyaficha kwa kudai wanaweka alama za ardhi(beacon), Nyerere akaamrisha askari waishi nyumba zile na iwepo kambi eneo lile.
Miaka kadhaa baadae Warusi walirud kufuata madini yao lakini walistaajabu walipokuta kuna kambi ya askari hivyo wakarudia mbali.
Hivi hamna historia ya maana km vile hao mashujaa wenu kuwapiga nchi nyingine?Au hao wanaojiita mashujaa wa usalama wa taifa na majeshi ya kupiga raia,tusikie waliweza hamisha mahela nchi fulani, wakashinda kesi kadhaa za kiuchumi?
 
Hizi Mali za mzungu navyo wajua wabongo wangekuwa washavuta mpunga kitambo sana
 
Madini yapo ila ni eneo lenye maajabu mpaka kupita tu pale kuna masharti ya kimila. Pia kama ujuavyo kuna mali nyingi za mkoloni maeneo ya Tanzania ila zimehifadhiwa kimila so ukienda macho kumchuzi ndio mwisho wako.
Wewe unachanganya kijungu na daraja la mungu, kijungu ndio huwezi kuvuka ila daraja la mungu unapita tu bila wasiwasi, nimepita sana kwenye lile daraja hamna kitu niliona.
 
Sio nyifwila,ni NYAFWILA,halafu si nyoka kama nyoka wengine,nakumbuka enzi hizo,akipita maeneo yetu ya bush,hapo asubuhi watu au mtu mmoja lazima adanje.

Wazee walikuwa wakituonya sana tusikanyage mafuta ya huyu nyoka,siku hizi hata hapiti wala kuonekana.
Mkuu, Mafuta yake yalikuwa yakionekana kwani?
 
Ningependa kujua zaidi kuhusu huyu nyoka
Wenye habari zake watuambie kama bado wapo
Nyoka anawasha taa duh😳😳😳
 
Mara ya mwisho kumwona ni 2009 ,alimulika nusu saa katka safu za livingstone mounts, mzee mmoja akaniambia kesho usiondoke kuna msiba,maana nilipanga kusafiri,nikaamuuliza why akasema hujamwona yule nyoka?

Asubuhi babu mmoja kafariki kweli,nilishangaa sana
Kuambiwa ndio kumwona ?

Halafu hizi ni imani tu hazina uhalisia
 
Nilishawahi kumsikia huyu Nyifwila kama nyoka mwenye vichwa vingi. Wenzetu wanaita dragon. Jamii nyingi sana zina aina hii ya viumbe (fikirika), hata nchi za magharibi. Uskoti (Scotland) wana Neiss wa Loch Ness ambaye wamemfanya kivutio cha utalii. Huko Norway wana kiumbe aliyetambulika kama Kraken, aliyeaminika kuwinda wavuvi. Sasa hivi ni chapa inayojulikana na kutumika kwenye filamu, vitabu, vinywaji, nk.

Hata huyu Nyifwila ni jinsi tu tukavyoamua kumchukulia. Anaweza kuwa sehemu ya kivutio cha utalii wa Daraja la Mungu.
 
Back
Top Bottom