Nyoka ni alama ya Tiba na Uponyaji ndio maana taasisi nyingi za Tiba hutumia nembo ya Nyoka

Nyoka ni alama ya Tiba na Uponyaji ndio maana taasisi nyingi za Tiba hutumia nembo ya Nyoka

KWA MIZIMU NYOKA NI UKUU,NYOKA NI UTAWALA NA ANAPOONEKANA NDOTONI AU KWENYE MAONI HUTAFSRIKA KAMA ULINZI MTUKUFU DHIDI YA HATARI ILIYO DHAHIRI.KWA UTABIBU NYOKA HUASHIRIA NAMNA TUKUFU YA UTABIBU USIMITHILIKA.KIROHO HUTAFSRIKA KAMA TAWALA ISIYOTETEREKA NA YENYE UUNGU MTUKUFU.MWISHO KIUJUMLA HUFASIRIKA KAMA UFALME WA WAFALME.
Sawa
Asante kwa mchango, kuna part nyingi sana nlizifupisha. Ili kuleta uzi usio mrefu.

Mungu akipenda nitaleta Alama ya Nyoka kwa Mtizamo wa Jamii za Kiafrika.
 
Ndotoni nyoka hutumika ili kumshtua mtu aamke.

Yaani kama umelala vibaya, damu haizunguki vizuri. Basi anakuja nyoka kwenye ndoto ili akutie presha kidogo moyo usukume damu izunguke mwili wote.

Lakini kama umejifunika gubigubi joto limezidi. Basi anakuja nyoka ndotoni akuvuruge ubiringike uliondoe blanketi.

Ikiwezekana basi hiyo adrenalini atakayokupiga itakuamsha ili urekebishe hali mbaya uendelee kuishi.

So wanaohusianisha nyoka na mizimu au majini basi waende mbele na kusema ni mizimu wazuri au majini wazuri wanaokutakia mema. Uishi wala usife.

Desperate needs, calls for desperate actions. Ikibidi kukuamsha na umelala fofofo na unazidi kuishiwa uhai pumzi........ basi inakuwa ndo muda wa kulileta 'bomu la maangamizi' (call in the big guns);

Linaletwa jinamizi ambalo ni mixer ya zimwi, jitu na joka kubwa. Utaaamka tu. Je jinamizi ndio malaika mlinzi!!!????👇
Okeyy
Shukraani kwa Mchango
 
NYOKA ,ALAMA YA UKOMBOZI (UUNGU) au USHETANI


SEHEMU YA II


Na Da Vinci XV





NYOKA KATIKA MAANDIKO MATAKATIFU


467ACA98-1B16-4CE1-8B51-C15D8E5BD4DF.jpeg



Kama nlivyopata kuelezea huko juu Mungu alimtumia nyoka katika kazi zake tofauti tofauti, ambazo ziliwakilishwa na nyoka

Maandiko ya Mwanzo kabisa ambayo yanamtaja nyoka ni katika kitabu cha (Mwanzo 3:1)

Hapo Bwana anajaribu kumuelezea Nyoka alivyo mwerevu na alivyofanikiwa kumrubuni Hawa na Mumewe kuvunja amri ya bwana Muumba wao.
Usisahau bwana anamzungumzia nyoka kiumbe mwerevu kupita kiumbe yoyote pale bustanini.

Sehemu ya pili ndio inaonyesha nyoka kama tulivyopata kuijadili huko juu Muungu anatumia nyoka kudhuru lakini vilevile Alama ya nyoka kama Tiba Tazama ( Hesabu 21: 4-9)


4 - Wakasafiri kutoka mlima wa Hori kwa njia ya Bahari ya Shamu; ili kuizunguka nchi ya Edomu, watu wakafa moyo kwa sababu ya ile njia.

5 - Watu wakamnung'unikia Mungu, na Musa, Mbona mmetupandisha huku kutoka nchi ya Misri, ili tufe jangwani? Maana hapana chakula, wala hapana maji, na roho zetu zinakinai chakula hiki dhaifu.

6 - Bwana akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma, watu wengi wakafa.

7 - Watu wakamwendea Musa, wakasema, Tumefanya dhambi kwa sababu tumemnung'unikia Mungu, na wewe; utuombee kwa Bwana, atuondolee nyoka hawa. Basi Musa akawaombea watu.

8 - Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi.

9 - Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi.



Naam, habari ya waisraeli na Musa nadhani wengi wetu tunaijua jinsi walivyokuwa wabishi juu ya Musa walishushiwa Chakula kutoka mbinguni na bado wakakikataa kifupi walikuwa na kashikashi kubwa sana na Musa na mungu wake vitimbi vya hali ya juu,

FF91CA8E-D896-4BE5-8AD7-D55E4226CA0A.jpeg


Andiko hilo linabainisha nyoka katika pande mbili kama Uponyaji na pande nyingine ni mwenye Kuleta madhara, Mungu aliwatumia waisraeli nyoka baada ya kumnenea vibaya Mungu na Musa ambae amewaokoa katika ardhi ya Utumwa na Kuwapeleka nchi ya Ahadi nyoka hao waliwauma na kusababisha vifo kwao lakini Baada ya Kugutuka Mungu akamwagizia dawa ya Nyoka hao ambayo ni sanamu ya Shaba ya Nyoka ambayo yoyote aitazamae ilimwokoa kutokana na Kifo. Hivyo hapa nyoka alitambulika kama Uponyaji.
Wakala wa madhara na Uponyaji ni nyoka, kifo na Uzima ni Nyoka. Lakini vyote hivi vilifanywa na Bwana Mungu Baba.


Naam
Sehemu ya Pili ni Musa alipoamriwa na mungu wake kwenda kwa Farao, kumpa elimu juu ya M/Mungu ili kuomukoa na kuwaokoa watu kutoka katika Upotofu , na ili somo liende sawasawa Mwenyezimungu alijaalia kwa Musa miujiza ambayo kwayo Huenda firauni angepata kutambua haki, Musa alitumia nyoka kama alama na Muujiza mbele ya Firauni na Wakati huo huo wachawi wa Firauni walitumia nyoka pia. Habari hii inapatikana katika biblia na Qur'an kwa Ujumla wake.



QUR'AN 20:17-


17 - Na nini hicho kilichomo mkononi mwako wa kulia, ewe Musa?

18 - Akasema (Musa) : Hii ni fimbo yangu; naiegemea na ninawaangushia majani kondoo na mbuzi wangu. Tena inanifaa kwa matumizi mengine.


19 - Akasema: Itupe, ewe Musa!


20 - (Musa) Akaitupa. Mara ikawa nyoka anaye kwenda mbio.



Hayo ni mazungumzo kati ya Nabii Musa na Mola Wake alipopewa dhima ya kwenda kumkabili Farao na Upotofu wake na habari ya Musa kwenye Qur'an ilianzia hapo badala ya M/mungu kumpa muujiza huu ambao kilichofwata Hadithi yake tunaijua Wachawi wa Firauni/farao walitupa nyoka zao kushindana na Musa ambaye nae kwa uwezo wa M/Mungu aliwavaa wote na kuwameza nyoka wote wa wachawi , kilichofuata hapo kwa Wachawi ni kufuata Mungu wa Musa na kumuamini Musa ukitaka kupata kisa hiki Endelea katika Aya za Mbele za Sura hii ya 20 ndani ya Qur'an tukufu (Surat Taha)


Na kwenye Biblia habari hii inapatikana katika Kitabu cha (KUTOKA 7:9-) kinaelezea vyema jinsi fimbo(Nyoka) ya Musa na Haruni ilivyomeza Nyoka wote wa wachawi wa Farao rejelea andiko hilo.

ACD563E8-9903-4EEE-8864-F1CA24F83EBE.jpeg


Hapo nyoka ametumika kama Uchawi (Wachawi wa Farao) na Pia ametumika katika Ukombozi(Nyoka wa Musa),mapambano mawili haya kati ya Upande Mungu na Upande wa Shetani na wote wakiwakilishwa na Nyoka.


Ukiachana nyoka kuonekana kama mkombozi lakini upande wa pili ndani vitabu hivi vitatifu vinamtaja nyoka kama Shetani na Ibilisi na Upotofu , Sehemu ya kwanza kabisa ni pale ambapo nyoka alifanikiwa kumrubuni Mama yetu Hawa na Kumhadaa akafanikiwa kuvunja alichoamriwa na Mungu wake. (MWANZO 3:4)

783C19F4-2720-4741-9FF0-BCDE9B6179BA.jpeg

Lakini pia Yohanna mtoto wa Zebedayo yule mwanafunzi wa Bwana Yesu, aliyetekwa na kupewa mateso katika kisiwa cha Patmo ili kumshurutisha aache kutangaza neno la M/mungu basi M/Mungu akamshushia ufunuo kumfunulia siri nyingi za dunia zijazo na zilizopita na zilizokuwepo wakati huo ili kumfariji Mwanafunzi huyu wa Bwana Yesu baada ya Kufikia hatua ya kukata tamaa juu ya mateso kutoka kwa Watesi wake.

Ufunuo wa Yohanna (12:9) inamtaja Nyoka kama Ibilisi /Shetani

(Ufunuo wa Yohana ) 12 : 9 - Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.

Ukirudi juu kidogo hadi mstari wa Tisa unajaribu kumuelezea Nyoka huyu Ibilisi anapojaribu , kupambana na Jeshi la M/Mungu na mwisho kutupwa na jeshi lake lote kushindwa.

BA1D088E-995E-43FC-B5DB-0013FB0C6C72.jpeg


Ili kujaribu kuhalalisha utambulisho wake wa uwongo kama mungu. Hii ndiyo sababu Shetani alichagua kutumia ishara ya nyoka kama njia bora zaidi ya kumdanganya Hawa na vilevile uzao wake kuanzia wakati huo na kuendelea.
Maandiko yanatusaidia kuona kwamba Shetani anaiga na kupotosha kila ukweli wa kimungu, kila dhana ya kimungu, kanuni, au utendaji, kila ishara nzuri na chanya, picha, ishara, na alama ili kudanganya na kuendesha roho za watu.
Na ndio sababu hii hata miungu , ya Watu wa kale na jamii za zamani zilitumia Ishara ya Nyoka kama njia ya kuyafikia mafanikio ya kiuungu na kama ujuavyo Mfumo na mwenendo wa miungu wengi ni mwenendo wa Shetani.
Kwa maana Nyoka mwanzo ilisimama kama Alama ya Kiungu na Uponyaji kutoka Mungu.






DaVinci XV
 
Nyoka ni alama ya Tiba na Uponyaji ndo maana taasisi nyingi za Tiba hutumia nemboya Nyoka. Hata Shirika la Afya Duniani WHO linaumia nembo ya nyoka, waganga wa jadi wanafuga nyoka wa kutosha, hata kwenye nembo ya hospitali ya Muhimbili kuna chata ya nyoka, Noti ya shilingi mia tano pia ilikua na picha ya nyoka ikimaanisha uchumi imara unahitaji watu wenye afya.

Nyoka ni kiumbe pekee mwenye uwezo wa kijivua gamba, tafsiri yake ni kwamba kujivua gamba ni kuleta uhai mpya (Mgonjwa Kupona). Lile gamba la nyoka ukikutana nalo barabarani linatoa nuksi, lishike tu uondoe nuksi za ile rambirambi uliyokula. Hata vidonge vimeundwa kwa mfano wa mayai ya nyoka kuvipa uponyaji. Kumbuka madaktari wanatibu, uponyaji anatoa Mungu.

Mussa alitengeneza nyoka wa shaba akamweka juu ya mti na kila aliyegongwa na nyoka alipona kwa kumwangalia nyoka yule. Uamuzi wa Mungu kuweka uponyaji kwenye nyoka wa shaba hadi mwana wa israeli kupona ndio umefanya taasisi nyingi za tiba duniani kutumia alama iyo ya nyoka.

Mara nyingi ipo getini ili mgonjwa anapoingia getini tu amwangalie nyoka apokee uponyaji. Wazee wa zamani wanakuambia nyoka anajua dawa zoe za mitishamba, nyoka akipata jeraha hujitibu au hutibiwa na wenzake hadi apone walitumia mitishamba, ndo mana wazee wa zamani wakikutana na hali iyo waliwafuatilia nyoka na kuangalia wanachuma dawa kwenye miti gani? na kutumia miti hiyo kama Tiba.

Marekani walianza kutumia alama ya nyoka baada ya kuja Afrika na kujifunza siri hii kutoka kwa wazee wetu, wakati jeshi lao lilioamua kutumia nembo ya nyoka kama alama ya kikosi cha Tiba cha jeshi ambalo awali lilitumia alama ya msalaba. Hii inarahisisha kazi ya madaktari kwa sababu wanatibu mtu mwenye uponyaji teyari. Ndugu zangu hii dunia ni kubwa mno unachotakiwa ni kujifunza kwa bidii sana ili usiishie kutukana tu ati nyoka ni ushirikina.

Nyoka ni kielelezo cha udadisi na umakini, utamaduni wa kuhoji badala ya kukubali kila kitu kirahisi. Kitendo cha nyoka kumwambia Eva ale tunda kina tafsiri mbili. Wapo wanaoona kitendo hicho kama uongo na wengine kama udadisi. Tafsiri ya makala hii ni tujifunze utamaduni wa kuhoji, tusikubali kila kitu kama mazuzu na wakati tuna akili za kutosha.

Robert Gren anasema, mwandishi wa kitabu cha THE 48 LAWS OF POWER anasema,"Hatuna budi kumshukuru nyoka, nyoka alikua mwalimu mkuu wa kwanza duniani, mtetezi wa kwanza wa udadisi na utafiti, adui wa kwanza wa ujinga, mnong'onezaji wa kwanza kwenye sikio la mwanadamu wa kwanza ili ajikomboe." Hii inaitwa Mental Liberation.

Usipotuliza akili ukaenda kiroho sana utasema Gren alimkufuru Mungu na wakati bibilia inasema, "Nyoka alikua mwelevu kuliko wanyama wote wa mwituni aliowafanya Bwana." Soma Mwanzo 3:1.

Kumbuka hata yesu mwenyewe amewahi kukiri kuwa nyoka ni mwelevu sana na akawatuma wanafunzi wake wawe na busara kama nyoka. Hili ni funzo kubwa sana kwamba kila kitu kina ubaya na uzuri na ukijua hilo huwezi kumuua mke wako kwa sababu amekudanganya mana hata wewe ni muongo tena kumzidi mkeo.

Kwanza uongo unasaidia sana maana kuna ndoa bila kudanganya zingesha kusambaratika siku nyingi. Bila kudanganya kuna watu walishafukuzwa kazi siku nyingi. Kuna watu bila kudanganya wasingepata wachumba na wengine wasingeoa bila uongo. Kuna watu uongo umewaokoa na kifo, tatizo la uongo ukigundulika ndo utakoma.

Nyoka ni ishara ya kujipa muda wa kufikiri kabla ya kutenda (Kuwa Makini) kwa asili nyoka ni mtulivu hafanyi jambo bila sababu. Ni hatari kwa viumbe wengine ana sumu kali, hafanyi jambo bila kufanya mchanganuo wa hasara na faida. Nyoka anapenda kukaa sehemu yenye utulivu, anaweza kuingia ndani ya nyumba na kusepa bila mtu yeyote kujua. Wengi tumelala na nyoka sana tu, wakati wa kiangazi wanakunywa maji ndani kabisa, sema kwa sababu ya mahesabu huwezi kuwaona. Nyoka wanacheza sana na watoto wako na hawafanyi kitu chochote kwa sababu wanajua watoto hawana roho mbaya.

Kupitia nyoka tunajifunza kutofanya mambo bila kuangalia madhara na faida kama mjinga anayepima kina cha maji kwa miguu miwili. Tusiwe kama yule mama mkwe aliyetumia hisia kujaji, kisa cha mama mkwe, "Bwana mmoja alikwenda kutembea ukweni kwake ilipofika usiku aliamka kwenda kujisaidia lakini kwa bahati mbaya taa zote zilikua zimezimwa, wakati anapapasa ili kuwasha taa aliparamia vyombo vya chakula jikoni. Kipindi anajaribu kuviweka vizuri mara taa ikawasha na mama mkwe akamuona yule bwana ameshika vyombo na kumwambia. Baba kama hukushiba ungesema.

Mama mkwe alitumia hisia kujaji hakujipa muda wa kufikiri. Shida ya hisia inakupa majibu ya haraka ambayo yanaweza kukuletea shida. Unadhani yule bwana aliendelea kukaa ukweni? Ndo yaleyale unakwenda kutembea sehemu unasikia sisi humu ndani hatujwahi kuibiwa kitu kabisa. Kichwa kisipofanya kazi vizuri ya kufikiri utakuwa mtu wa kuchafua hali ya hewa kila siku. Nyoka anatukumbusha kujipa muda wa kufikiri zaidi.

Kwaiyo unapokutana na nyoka mara kwa mara basi rejea hizi tafsiri hapa lakini unapokutana na nyoka ndotoni hizi hapa tafsiri kutoka kwa mtaalamu wa mambo ya asili.

1. Ukiota umegongwa na nyoka ina maana kwamba unatakiwa kuwa makini kwenye mambo yako vinginevyo utaumia. Umezoea kupiga hela acha, una tabia ya kula ada acha, una tabia ya kula michango ya harusi acha, unahonga hadi hela ya rambirambi acha mara moja, una tabia ya kuchepuka acha usikamatwe na mchepukaji mwezako akakunyonga.

Siku hizi wanaume wanaua sana na hiyo ndo maana ya ndoto ya nyoka. Wazungu wanasema if you have a dream of a snake chasing you, this might mean that you need to look at the relationship in your life and see if you have sweapt any issues underneath malizia kwa kugoogle huo msemo ........

2. Ukiota unamuona nyoka maana yake ni kwamba utadanganywa na mkeo au mumeo. jaribu kumkumbusha uaminifu katika ndoa, najua atawaka kwa sababu umemtachi lakini usikonde kwa sababu kinga ni bora kuliko Tiba ya mapenzi.

3. Ukiota unapigana na nyoka ni ishara ya kuwashinda adui zako, lakini ukiota unakimbizwa na nyoka jua adui zako wanakumaliza. Jipange, kazi kwako kupambana na hali yako. Kazi ya nyoka ni kukupa taarifa tu.

4. Ukiota unafuga nyoka au unamiliki nyoka au nyoka anakumeza hiyo ni ishara ya kupata madaraka makubwa ya uongozi. Kama ulipanga kutia nia we tia tu usiache.

5. Ukiota umemuona nyoka anauliwa barabarani hiyo ni ishara ya kutokea vita au magomvi. unaweza kuzichapa kazini, nyumbani au popote pale hivyo jitahidi kuwa makini.

6. Ukiota shamba lako limejaa nyoka ni ishara ya kwamba utapata mazao mengi msimu huo tunza shamba lako vizuri na unapomuota nyoka amekufa ni ishara umeepushwa na uadui na shari yake. pengine ulikuwa unapiwa hadi kutolewa meno.

7. Ukiota joka kubwa linajizongazonga mwilini mwako ni dalili ya jini aliyeingia mwilini anatafuta sehemu ya kujificha ndani yako. Piga sana maombi.

8. Ukiota una nyoka shingoni mwako ukamkatakata maana yake unakwenda kutoa talaka kwa mkeo.
Nyoka hufugwa ili kupata sumu yake inayotumika kwenye tiba kama ilivyo sumu ya nyuki, usiuwe nyoka.
 
Nyoka ni alama ya Tiba na Uponyaji ndo maana taasisi nyingi za Tiba hutumia nemboya Nyoka. Hata Shirika la Afya Duniani WHO linaumia nembo ya nyoka, waganga wa jadi wanafuga nyoka wa kutosha, hata kwenye nembo ya hospitali ya Muhimbili kuna chata ya nyoka, Noti ya shilingi mia tano pia ilikua na picha ya nyoka ikimaanisha uchumi imara unahitaji watu wenye afya.

Nyoka ni kiumbe pekee mwenye uwezo wa kijivua gamba, tafsiri yake ni kwamba kujivua gamba ni kuleta uhai mpya (Mgonjwa Kupona). Lile gamba la nyoka ukikutana nalo barabarani linatoa nuksi, lishike tu uondoe nuksi za ile rambirambi uliyokula. Hata vidonge vimeundwa kwa mfano wa mayai ya nyoka kuvipa uponyaji. Kumbuka madaktari wanatibu, uponyaji anatoa Mungu.

Mussa alitengeneza nyoka wa shaba akamweka juu ya mti na kila aliyegongwa na nyoka alipona kwa kumwangalia nyoka yule. Uamuzi wa Mungu kuweka uponyaji kwenye nyoka wa shaba hadi mwana wa israeli kupona ndio umefanya taasisi nyingi za tiba duniani kutumia alama iyo ya nyoka.

Mara nyingi ipo getini ili mgonjwa anapoingia getini tu amwangalie nyoka apokee uponyaji. Wazee wa zamani wanakuambia nyoka anajua dawa zoe za mitishamba, nyoka akipata jeraha hujitibu au hutibiwa na wenzake hadi apone walitumia mitishamba, ndo mana wazee wa zamani wakikutana na hali iyo waliwafuatilia nyoka na kuangalia wanachuma dawa kwenye miti gani? na kutumia miti hiyo kama Tiba.

Marekani walianza kutumia alama ya nyoka baada ya kuja Afrika na kujifunza siri hii kutoka kwa wazee wetu, wakati jeshi lao lilioamua kutumia nembo ya nyoka kama alama ya kikosi cha Tiba cha jeshi ambalo awali lilitumia alama ya msalaba. Hii inarahisisha kazi ya madaktari kwa sababu wanatibu mtu mwenye uponyaji teyari. Ndugu zangu hii dunia ni kubwa mno unachotakiwa ni kujifunza kwa bidii sana ili usiishie kutukana tu ati nyoka ni ushirikina.

Nyoka ni kielelezo cha udadisi na umakini, utamaduni wa kuhoji badala ya kukubali kila kitu kirahisi. Kitendo cha nyoka kumwambia Eva ale tunda kina tafsiri mbili. Wapo wanaoona kitendo hicho kama uongo na wengine kama udadisi. Tafsiri ya makala hii ni tujifunze utamaduni wa kuhoji, tusikubali kila kitu kama mazuzu na wakati tuna akili za kutosha.

Robert Gren anasema, mwandishi wa kitabu cha THE 48 LAWS OF POWER anasema,"Hatuna budi kumshukuru nyoka, nyoka alikua mwalimu mkuu wa kwanza duniani, mtetezi wa kwanza wa udadisi na utafiti, adui wa kwanza wa ujinga, mnong'onezaji wa kwanza kwenye sikio la mwanadamu wa kwanza ili ajikomboe." Hii inaitwa Mental Liberation.

Usipotuliza akili ukaenda kiroho sana utasema Gren alimkufuru Mungu na wakati bibilia inasema, "Nyoka alikua mwelevu kuliko wanyama wote wa mwituni aliowafanya Bwana." Soma Mwanzo 3:1.

Kumbuka hata yesu mwenyewe amewahi kukiri kuwa nyoka ni mwelevu sana na akawatuma wanafunzi wake wawe na busara kama nyoka. Hili ni funzo kubwa sana kwamba kila kitu kina ubaya na uzuri na ukijua hilo huwezi kumuua mke wako kwa sababu amekudanganya mana hata wewe ni muongo tena kumzidi mkeo.

Kwanza uongo unasaidia sana maana kuna ndoa bila kudanganya zingesha kusambaratika siku nyingi. Bila kudanganya kuna watu walishafukuzwa kazi siku nyingi. Kuna watu bila kudanganya wasingepata wachumba na wengine wasingeoa bila uongo. Kuna watu uongo umewaokoa na kifo, tatizo la uongo ukigundulika ndo utakoma.

Nyoka ni ishara ya kujipa muda wa kufikiri kabla ya kutenda (Kuwa Makini) kwa asili nyoka ni mtulivu hafanyi jambo bila sababu. Ni hatari kwa viumbe wengine ana sumu kali, hafanyi jambo bila kufanya mchanganuo wa hasara na faida. Nyoka anapenda kukaa sehemu yenye utulivu, anaweza kuingia ndani ya nyumba na kusepa bila mtu yeyote kujua. Wengi tumelala na nyoka sana tu, wakati wa kiangazi wanakunywa maji ndani kabisa, sema kwa sababu ya mahesabu huwezi kuwaona. Nyoka wanacheza sana na watoto wako na hawafanyi kitu chochote kwa sababu wanajua watoto hawana roho mbaya.

Kupitia nyoka tunajifunza kutofanya mambo bila kuangalia madhara na faida kama mjinga anayepima kina cha maji kwa miguu miwili. Tusiwe kama yule mama mkwe aliyetumia hisia kujaji, kisa cha mama mkwe, "Bwana mmoja alikwenda kutembea ukweni kwake ilipofika usiku aliamka kwenda kujisaidia lakini kwa bahati mbaya taa zote zilikua zimezimwa, wakati anapapasa ili kuwasha taa aliparamia vyombo vya chakula jikoni. Kipindi anajaribu kuviweka vizuri mara taa ikawasha na mama mkwe akamuona yule bwana ameshika vyombo na kumwambia. Baba kama hukushiba ungesema.

Mama mkwe alitumia hisia kujaji hakujipa muda wa kufikiri. Shida ya hisia inakupa majibu ya haraka ambayo yanaweza kukuletea shida. Unadhani yule bwana aliendelea kukaa ukweni? Ndo yaleyale unakwenda kutembea sehemu unasikia sisi humu ndani hatujwahi kuibiwa kitu kabisa. Kichwa kisipofanya kazi vizuri ya kufikiri utakuwa mtu wa kuchafua hali ya hewa kila siku. Nyoka anatukumbusha kujipa muda wa kufikiri zaidi.

Kwaiyo unapokutana na nyoka mara kwa mara basi rejea hizi tafsiri hapa lakini unapokutana na nyoka ndotoni hizi hapa tafsiri kutoka kwa mtaalamu wa mambo ya asili.

1. Ukiota umegongwa na nyoka ina maana kwamba unatakiwa kuwa makini kwenye mambo yako vinginevyo utaumia. Umezoea kupiga hela acha, una tabia ya kula ada acha, una tabia ya kula michango ya harusi acha, unahonga hadi hela ya rambirambi acha mara moja, una tabia ya kuchepuka acha usikamatwe na mchepukaji mwezako akakunyonga.

Siku hizi wanaume wanaua sana na hiyo ndo maana ya ndoto ya nyoka. Wazungu wanasema if you have a dream of a snake chasing you, this might mean that you need to look at the relationship in your life and see if you have sweapt any issues underneath malizia kwa kugoogle huo msemo ........

2. Ukiota unamuona nyoka maana yake ni kwamba utadanganywa na mkeo au mumeo. jaribu kumkumbusha uaminifu katika ndoa, najua atawaka kwa sababu umemtachi lakini usikonde kwa sababu kinga ni bora kuliko Tiba ya mapenzi.

3. Ukiota unapigana na nyoka ni ishara ya kuwashinda adui zako, lakini ukiota unakimbizwa na nyoka jua adui zako wanakumaliza. Jipange, kazi kwako kupambana na hali yako. Kazi ya nyoka ni kukupa taarifa tu.

4. Ukiota unafuga nyoka au unamiliki nyoka au nyoka anakumeza hiyo ni ishara ya kupata madaraka makubwa ya uongozi. Kama ulipanga kutia nia we tia tu usiache.

5. Ukiota umemuona nyoka anauliwa barabarani hiyo ni ishara ya kutokea vita au magomvi. unaweza kuzichapa kazini, nyumbani au popote pale hivyo jitahidi kuwa makini.

6. Ukiota shamba lako limejaa nyoka ni ishara ya kwamba utapata mazao mengi msimu huo tunza shamba lako vizuri na unapomuota nyoka amekufa ni ishara umeepushwa na uadui na shari yake. pengine ulikuwa unapiwa hadi kutolewa meno.

7. Ukiota joka kubwa linajizongazonga mwilini mwako ni dalili ya jini aliyeingia mwilini anatafuta sehemu ya kujificha ndani yako. Piga sana maombi.

8. Ukiota una nyoka shingoni mwako ukamkatakata maana yake unakwenda kutoa talaka kwa mkeo.
Tuko kwa Yesu sasa. Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo Hivyo Mwana wa Adamu (YESU) hana budi kuinuliwa.''yoh 3:14"'
 
Nyoka ni alama ya Tiba na Uponyaji ndo maana taasisi nyingi za Tiba hutumia nemboya Nyoka. Hata Shirika la Afya Duniani WHO linaumia nembo ya nyoka, waganga wa jadi wanafuga nyoka wa kutosha, hata kwenye nembo ya hospitali ya Muhimbili kuna chata ya nyoka, Noti ya shilingi mia tano pia ilikua na picha ya nyoka ikimaanisha uchumi imara unahitaji watu wenye afya.

Nyoka ni kiumbe pekee mwenye uwezo wa kijivua gamba, tafsiri yake ni kwamba kujivua gamba ni kuleta uhai mpya (Mgonjwa Kupona). Lile gamba la nyoka ukikutana nalo barabarani linatoa nuksi, lishike tu uondoe nuksi za ile rambirambi uliyokula. Hata vidonge vimeundwa kwa mfano wa mayai ya nyoka kuvipa uponyaji. Kumbuka madaktari wanatibu, uponyaji anatoa Mungu.

Mussa alitengeneza nyoka wa shaba akamweka juu ya mti na kila aliyegongwa na nyoka alipona kwa kumwangalia nyoka yule. Uamuzi wa Mungu kuweka uponyaji kwenye nyoka wa shaba hadi mwana wa israeli kupona ndio umefanya taasisi nyingi za tiba duniani kutumia alama iyo ya nyoka.

Mara nyingi ipo getini ili mgonjwa anapoingia getini tu amwangalie nyoka apokee uponyaji. Wazee wa zamani wanakuambia nyoka anajua dawa zoe za mitishamba, nyoka akipata jeraha hujitibu au hutibiwa na wenzake hadi apone walitumia mitishamba, ndo mana wazee wa zamani wakikutana na hali iyo waliwafuatilia nyoka na kuangalia wanachuma dawa kwenye miti gani? na kutumia miti hiyo kama Tiba.

Marekani walianza kutumia alama ya nyoka baada ya kuja Afrika na kujifunza siri hii kutoka kwa wazee wetu, wakati jeshi lao lilioamua kutumia nembo ya nyoka kama alama ya kikosi cha Tiba cha jeshi ambalo awali lilitumia alama ya msalaba. Hii inarahisisha kazi ya madaktari kwa sababu wanatibu mtu mwenye uponyaji teyari. Ndugu zangu hii dunia ni kubwa mno unachotakiwa ni kujifunza kwa bidii sana ili usiishie kutukana tu ati nyoka ni ushirikina.

Nyoka ni kielelezo cha udadisi na umakini, utamaduni wa kuhoji badala ya kukubali kila kitu kirahisi. Kitendo cha nyoka kumwambia Eva ale tunda kina tafsiri mbili. Wapo wanaoona kitendo hicho kama uongo na wengine kama udadisi. Tafsiri ya makala hii ni tujifunze utamaduni wa kuhoji, tusikubali kila kitu kama mazuzu na wakati tuna akili za kutosha.

Robert Gren anasema, mwandishi wa kitabu cha THE 48 LAWS OF POWER anasema,"Hatuna budi kumshukuru nyoka, nyoka alikua mwalimu mkuu wa kwanza duniani, mtetezi wa kwanza wa udadisi na utafiti, adui wa kwanza wa ujinga, mnong'onezaji wa kwanza kwenye sikio la mwanadamu wa kwanza ili ajikomboe." Hii inaitwa Mental Liberation.

Usipotuliza akili ukaenda kiroho sana utasema Gren alimkufuru Mungu na wakati bibilia inasema, "Nyoka alikua mwelevu kuliko wanyama wote wa mwituni aliowafanya Bwana." Soma Mwanzo 3:1.

Kumbuka hata yesu mwenyewe amewahi kukiri kuwa nyoka ni mwelevu sana na akawatuma wanafunzi wake wawe na busara kama nyoka. Hili ni funzo kubwa sana kwamba kila kitu kina ubaya na uzuri na ukijua hilo huwezi kumuua mke wako kwa sababu amekudanganya mana hata wewe ni muongo tena kumzidi mkeo.

Kwanza uongo unasaidia sana maana kuna ndoa bila kudanganya zingesha kusambaratika siku nyingi. Bila kudanganya kuna watu walishafukuzwa kazi siku nyingi. Kuna watu bila kudanganya wasingepata wachumba na wengine wasingeoa bila uongo. Kuna watu uongo umewaokoa na kifo, tatizo la uongo ukigundulika ndo utakoma.

Nyoka ni ishara ya kujipa muda wa kufikiri kabla ya kutenda (Kuwa Makini) kwa asili nyoka ni mtulivu hafanyi jambo bila sababu. Ni hatari kwa viumbe wengine ana sumu kali, hafanyi jambo bila kufanya mchanganuo wa hasara na faida. Nyoka anapenda kukaa sehemu yenye utulivu, anaweza kuingia ndani ya nyumba na kusepa bila mtu yeyote kujua. Wengi tumelala na nyoka sana tu, wakati wa kiangazi wanakunywa maji ndani kabisa, sema kwa sababu ya mahesabu huwezi kuwaona. Nyoka wanacheza sana na watoto wako na hawafanyi kitu chochote kwa sababu wanajua watoto hawana roho mbaya.

Kupitia nyoka tunajifunza kutofanya mambo bila kuangalia madhara na faida kama mjinga anayepima kina cha maji kwa miguu miwili. Tusiwe kama yule mama mkwe aliyetumia hisia kujaji, kisa cha mama mkwe, "Bwana mmoja alikwenda kutembea ukweni kwake ilipofika usiku aliamka kwenda kujisaidia lakini kwa bahati mbaya taa zote zilikua zimezimwa, wakati anapapasa ili kuwasha taa aliparamia vyombo vya chakula jikoni. Kipindi anajaribu kuviweka vizuri mara taa ikawasha na mama mkwe akamuona yule bwana ameshika vyombo na kumwambia. Baba kama hukushiba ungesema.

Mama mkwe alitumia hisia kujaji hakujipa muda wa kufikiri. Shida ya hisia inakupa majibu ya haraka ambayo yanaweza kukuletea shida. Unadhani yule bwana aliendelea kukaa ukweni? Ndo yaleyale unakwenda kutembea sehemu unasikia sisi humu ndani hatujwahi kuibiwa kitu kabisa. Kichwa kisipofanya kazi vizuri ya kufikiri utakuwa mtu wa kuchafua hali ya hewa kila siku. Nyoka anatukumbusha kujipa muda wa kufikiri zaidi.

Kwaiyo unapokutana na nyoka mara kwa mara basi rejea hizi tafsiri hapa lakini unapokutana na nyoka ndotoni hizi hapa tafsiri kutoka kwa mtaalamu wa mambo ya asili.

1. Ukiota umegongwa na nyoka ina maana kwamba unatakiwa kuwa makini kwenye mambo yako vinginevyo utaumia. Umezoea kupiga hela acha, una tabia ya kula ada acha, una tabia ya kula michango ya harusi acha, unahonga hadi hela ya rambirambi acha mara moja, una tabia ya kuchepuka acha usikamatwe na mchepukaji mwezako akakunyonga.

Siku hizi wanaume wanaua sana na hiyo ndo maana ya ndoto ya nyoka. Wazungu wanasema if you have a dream of a snake chasing you, this might mean that you need to look at the relationship in your life and see if you have sweapt any issues underneath malizia kwa kugoogle huo msemo ........

2. Ukiota unamuona nyoka maana yake ni kwamba utadanganywa na mkeo au mumeo. jaribu kumkumbusha uaminifu katika ndoa, najua atawaka kwa sababu umemtachi lakini usikonde kwa sababu kinga ni bora kuliko Tiba ya mapenzi.

3. Ukiota unapigana na nyoka ni ishara ya kuwashinda adui zako, lakini ukiota unakimbizwa na nyoka jua adui zako wanakumaliza. Jipange, kazi kwako kupambana na hali yako. Kazi ya nyoka ni kukupa taarifa tu.

4. Ukiota unafuga nyoka au unamiliki nyoka au nyoka anakumeza hiyo ni ishara ya kupata madaraka makubwa ya uongozi. Kama ulipanga kutia nia we tia tu usiache.

5. Ukiota umemuona nyoka anauliwa barabarani hiyo ni ishara ya kutokea vita au magomvi. unaweza kuzichapa kazini, nyumbani au popote pale hivyo jitahidi kuwa makini.

6. Ukiota shamba lako limejaa nyoka ni ishara ya kwamba utapata mazao mengi msimu huo tunza shamba lako vizuri na unapomuota nyoka amekufa ni ishara umeepushwa na uadui na shari yake. pengine ulikuwa unapiwa hadi kutolewa meno.

7. Ukiota joka kubwa linajizongazonga mwilini mwako ni dalili ya jini aliyeingia mwilini anatafuta sehemu ya kujificha ndani yako. Piga sana maombi.

8. Ukiota una nyoka shingoni mwako ukamkatakata maana yake unakwenda kutoa talaka kwa mkeo.
Tuko kwa Yesu sasa. Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo Hivyo Mwana wa Adamu (YESU) hana budi kuinuliwa.''yoh 3:14"'
 
Wakati Africa tumeaminishwa kuwa nyoka ni shetani Wazungu na waarabu wao wanamfuga nakuchezanaye kama mtoto mchanga.

Shirika la dawa duniani Yani mahospitalini wanatumia alama ya nyoka kama alama ya uponyaji, Vivyo ivyo kwa Imani za jadi nyoka wanamtumia kama uponyaji yani ukimuona nyoka kama hu mgonjwa basi umepona, kama usafarini basi safari yako ni ya mafanikio, kama hu mgonjwa wa macho yale mate yake ni dawa nk.

Pia nyoka utumiwa na matajiri wengi duniani japo Africa anatumiwa kisirisiri kuliko watu weupe wanavyomtumia bila kuficha, Bible inatuambia nyoka ndo kiumbe mwelevu kuliko wanyama wote, hiyo hiyo Bible inasema nyoka ni shetani, hiyo hiyo Bible inasema atakaye mtazama nyoka wa Musa ndiye atakaye okoka..

Swali Je Kuna siri gani juu ya nyoka iliyofichwa na wahenga na hizi dini batili tulizoletewa na wakoloni?
 
Back
Top Bottom