Nyota zenu HAZIFANANI

Jamani huyo mwanamke yupo karne gani?ya kuamini huo upotovu?,mbona haiingii akilini?inaonyesha anatafuta sababu za kuachana ila kaona bora atafute visingizio hivyo. Ingawa yataka moyo ila piga moyo konde mpe nafasi kwa upande wake,mwache dunia imfunze,atakuja juta tu.
 
vumilieni tu kama sie wanawake tunavyovumiliana vimbwanga vyenu...
mie nashangaaga sana,utakuta mwanaume huyo huyo ashawahi kuwa na vimada kibao siku akisikia mkewe naye yupo upande huo huo wake anashindwa hadi kufanya kazi!!!!??!
wewe BUJIBUJI mwambie huyo kaka wanawake wapo kibao...principle ni kama ile kata mti panda mti,atafute mwanamke mwingine...baaasi,ila kabla hajaweka ndani ahakikishe anakuwa na check-list ya mwanamke anayemhitaji.sio anajizolea tu mwanamke na kuweka ndani.matokeo yake ndio hayo mtu anakupa sababu za kijinga kutaka kukuacha za you know jogoo kasuka mabutu-hazimake sense.
 
Nyota haziendani mbona wamebahatika kupata watoto?
Nyota haziendani mbona hakuna mtoto hata mmoja aliyefariki.
Nyota haziendani mbona wamesoma hadi chuo na wamehitimu
nyota haziendani mbona.......(atamalizia)
mwambie jamaa amuulize mambo yote mazuri waliyofanikiwa kufanya kwa hizo hizo nyota zao.
Amuulize sababu hasa. Habari za nyota haiingii akilini.
 
Nyota haziendani mbona wamebahatika kupata watoto?
Nyota haziendani mbona hakuna mtoto hata mmoja aliyefariki.
Nyota haziendani mbona wamesoma hadi chuo na wamehitimu
nyota haziendani mbona.......(atamalizia)
mwambie jamaa amuulize mambo yote mazuri waliyofanikiwa kufanya kwa hizo hizo nyota zao.
Amuulize sababu hasa. Habari za nyota haiingii akilini hapo kuna sababu nyngne.
 
ukimpenda mtu ni pamoja na kumpa nafasi kufanya yale anayoamini yanamfurahisha mwisho wa siku atapata majibu ya kila tendo alilolifanya,bila hata kuulizwa na mtu, najua inaumiza sana kuona umpendaye anakwenda kinyume na yale unayotarajia. mara nyingi wanawake hutembea na watu wanaowapenda sasa waeza kuta mkurugenzi anatoa huduma za ziada ambazo baba hafanyi mapenzi nayo upofu lakini nashindwa kuelewa jambo moja ukishazaa watoto wawili najua tunakomaa zaidi kiakili ivi mapenzi ya mpita njia na watoto yapi yana thamani mpe muda mkeo nakwambia atarudi na kilio ambacho atasahau maishani.

mapenzi yana stage huyu dada yupo stage ya kwanza ndo maana kaweza kumueleza mumewe huu upuuzi subiri ile stage ya pili igote mahali yake kama hakupiga ukunga wa kikwao mwambie kaka asimame kiume kupigania maisha ya wanawe kama dada anangangana na nyota ampe nafasi maana waeza kuta tayari mkewe kashaanza kusafiria ungo kushika penzi la kibosile bila wote kujua
 
Duuuh nampa pole yake. ila yaonekana mwanamke kesha pata tamu zaidi ndio maana ameanza jeuri unajua alisha zoea nyama ya ng'ombe sasa kajaribu ya nyati ya ng'ombe hataki tena huyo. cha msing kukomaanae ita mchukua time kubadilika but kama huna moyo wa kuvumilia achia ngazi. pili jamani lazma 2wewakweli jamani huenda bosi ka2mia ile dawa ya nasa usitoke. maana simchezo mambo mengine. jamaa atafute njia ya kumrejeza mkewe la sivyo atawatia watoto shida za bure. mwisho mwambie asiifikirie dunia kama anavyo iona but dunia imebadilika ikotofauti na anavyo iona. afungue macho na aachane na upofu. namtakia jitihada njema
 
<br />
<br />
Pumba hizi kila mahali.
Ingia hapa www.astrology.com
Ndio waganga wa kienyeji nao?
 
Mara zote huwa napenda kushauri baada ya kusikia pande zote mbili. Ila pia hata upande mmoja naweza shauri ila si kwa kiwango kinachoridhisha. KWANZA KABISA MUULIZE HUYO JAMAA YAKO WATOTO WANA UMRI GANI SASA. KAMA MWANAMKE KWELI AMETAMKA HAYO YA KUACHANA AMEMAANISHA LILILO MOYONI. kuna makabila ambayo kabla ya kumwoa unahitaji maombi ya kufunga siku saba ili kukata minyororo ya enzi na enzi ambayo wao hurithi. Kama hauko kwa mlengo wa kimaombi, Shirikisha wana ndugu hasa wa kwake including kaka zake wenye mlengo mzuri na usiwafiche la meneja kitambi. VINGINEVYO amesoma udhaifu wake ndo maana anamtesa. Maneno ya mzuri sana ndo maana anaonekana hajazaa ni kipuuzi...UZURI WA MWANAMKE SIYO UREMBO NI TABIA..Mwache akale urembo wake ambao utaisha punde na akirudi usimsamehe tena. Wapo wanawake wazuri sana ambao wanahitaji mume wa kweli hata kama ana watoto kumi. Fanya kazi kwa bidii..tumia muda wako na marafiki...chukua mwanamke umtakae kutimiza ngono bila kusahau condoms..hudhuria maeneo ya kukufurahisha...usikumbuke mlikotoka angalia unakokwenda...watoto kama wanaumri zaidi ya miaka saba waeleze wasome sana..waletee vinavyowajaza furaha...usimkaripie mama yao mbele yao..usikae naye meza ya mazungumzo tena...mkilala usiku usimguse hata kama anataka penzi na kama akilazimisha vaa condom maana atakuuwa mtuachie yatima....vitendo hivyo vitamfanya aumie sana na ataanza kuchange. Rafiki yake wa karibu kama anao wachape nao wote...watembezee mwili waziwazi..then kama mhudumiaji watoto yuko mmoja leta wa pili mrembo kuliko yeye ILA KAMWE USIJARIBU KUTEMBEA NA HUYO HOUSEGIRL
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…