Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
- Thread starter
-
- #41
Abunuwasi,Hivi jamani mnamkumbuka mzee Mpangile pale kwenye makaburi ya kisutu ambaye wakati tukiwa wadogo tulikuwa tunakwenda kupopoe maembe maeneo yale naye alikuwa anatufurusha mbio ilikuwa kama mchezo wa paka na panya pale-
Mwenyezi mungu amlaze mahala pema babu yetu yule
Othiambo,
Hakika nyakati zile wazee wakituhimiza sana kuhusu adabu.
Walikuwa na neno lao wakituasa,''Usitutukanishe.''
Maana ikiwa mtoto atakosa adabu watu watajua mama yake
hakumfunza adabu na hili kwao lilikuwa tusi kubwa.
Ustaarabu bado ungalipo ni wajibu wetu kuwafunza wanetu
na hata hapa barzani ikiwa unahisi mtu hakupata malezi kwao
kwa njia ya utaratibu unamuelekeza kuwa huenda huko kwenu
si vibaya lakini haifai kufanya kadha wa kadha kwenye kadamnasi.
Mbetini,Maalim umenipeleka mbali sana wakati nasoma Mombasa Kenya 1974 niliona “The Mechanic”
Radika,Nimevutiwa na ustaarabu wako basi ntafurahi kuziona mada zako nyingi zina mafunzo hasa kwa namna unavyoandika lugha yetu ya kiswahili inavutia sana nakupongeza sana.
Radika,
Ahsante kaka.
Nimezaliwa na kukulia Dar es Salaam Kariakoo ya 1960s.
Sina ''vernacular,'' ninasema Kiswahili toka utoto.
Ingia: www.mohammedsaid.com
Radika,Nashukuru mkuu ngoja nicheki.
Radika,
Karibu.
Unaweza kufanya ''search,'' kwa majina na matukio.
Mathalan Julius Nyerere, Rashid Kawawa, TANU, Mapinduzi ya Zanzibar nk.
Ukiingia kwenye ''Gallery,'' kuna DVD na Audio nazungumza.
Bali...Asante maalim
Radika,Shukrani sana kwa ufafanuzi nitafanya hivyo.
Mkuu nakukubali sana,nataka nikitulia nitafute muda,nawe ukubali kunipa wasaa,nikutembelee unijuze ilimu,wajua sisi hatukubahatika kuwa karibu na watu wanoijua nchi hii ,hivyo kazi kwetu kuitafuta kwa wajuzi kama wewe ,maalimuBali...
Ahsante kaka.
Clint Eastwood????
Ni kweli kabisa na kila mtu mzima alikuwa ni mzazi pia kwani aliweza kumuadibisha mtoto yoyote aliyekosa mahapa popote pale anapoona inafaa.
Na ikitokea baada ya hapo akamhadithia mzazi halisi basi kesi na adhabu huanza upya kabisa.
Bro,Duh Abunwasi umenikumbusha mbali sana.
Juzi nilikuwa katika mikutano yangu ya biashara nikaulizwa nielezee nilikulia katika mazingira gani utotoni.Nilijibu Kama ulivyo elezea hapo juu Na nikaongezea Nilikuzwa na kulelewa Na mtaa mzima. Maana toka natoka nyumbani mpaka shule ninachungwa Na majirani bila ya kujijua.Nikigombana Au nikafanya utovu wa Nidhamu nitapigwa Au kukemewa Na wazee wa mtaani.Kwa kweli huwa namshukuru Mwenye-EZ-Mungu Kwa mapenzi ya majirani Na Watu wengi tu.Naongelea miaka ya 60s Na 70s
Maalim wangu salaam aleykum, mi nilikutana na Juma Kubbe juzi msikiti wa Mwembe chai kwenye kisomo cha tahtim ya Marehemu Bi Tatu Mrisho mke wa Rahim Lumelezi aliyekuwa mchezaji wa Simba Sports Club basi Sheikh Thabit alimwita kwa jina lake la utani Jimmy Lover nilimuona Juma kubbe akitabasamu kama hulka yake ilivyo siku zote ni mtu wa kutabasamu na mas'hara sana.
Lutayega,mzee@mohamed said makala zako huwa zinanivutia ila huwa sipati funzo lolote kwenye hizo habari. Naomba nisaidie lengo la visa vya kihistoria unavyotupatia ni kutusaidia kupata funzo gani. Mfano kisa hiki kinatufunza Nini, na je ulitaka DSM za enzi ya 1950 ibaki vilevile na ili iweje
Lutayega,
Sababu ya kuweka post hiyo ni kuonyesha Dar es Salaam ilikuwaje.
Hii ni katika kuhifadhi historia kwa vizazi vijazo.
Visa kama ulivyoita ninavyoweka ni kueleza mambo ambayo si wengi
wanayajua na kwa sababu ile ile ya kuhifadhi historia.
Kuhusu kupata funzo hiyo inategemea na inatofutiana kati ya mtu na
mtu.
Kuna wanaopata elimu mpya katika makala zangu na kuna wengine
wanatoka hawajaelewa kitu.
Sijui nini kimekufanya useme kuwa natamani Dar es Salaam ingebaki
kama ilivyokuwa.
asante kwa ufafanuzi, kilichonifanya kukuliza nimeona kwenye Maelezo yako kama unalalamika eneo ilipokuwapo hiyo nyumba kujengwa magorofa.Lutayega,
Sababu ya kuweka post hiyo ni kuonyesha Dar es Salaam ilikuwaje.
Hii ni katika kuhifadhi historia kwa vizazi vijazo.
Visa kama ulivyoita ninavyoweka ni kueleza mambo ambayo si wengi
wanayajua na kwa sababu ile ile ya kuhifadhi historia.
Kuhusu kupata funzo hiyo inategemea na inatofutiana kati ya mtu na
mtu.
Kuna wanaopata elimu mpya katika makala zangu na kuna wengine
wanatoka hawajaelewa kitu.
Sijui nini kimekufanya useme kuwa natamani Dar es Salaam ingebaki
kama ilivyokuwa.
Lutayega,asante kwa ufafanuzi, kilichonifanya kukuliza nimeona kwenye Maelezo yako kama unalalamika eneo ilipokuwapo hiyo nyumba kujengwa magorofa.