Nyumba na. 81 Aggrey street Dar es salaam 1955

Nyumba na. 81 Aggrey street Dar es salaam 1955

Asante sana kwa Historia iliyotukuka Mzee wetu. Tunaomba uendelee kuiweka humu kwa manufaa ya vizazi vijavyo. Asante sana.
Tusker...
Kila inapotokea nafasi In Shaallah nitajaribu kueleza kile ninachokifahamu.
 
Isambe,
Ahsante ndugu yangu.

Nimeshangazwa na ile chuki katika kauli zake.
Nimejiuliza kipi kimemghadhibisha huyu ndugu yangu?

Yawezekana katika ile ''post,'' lipo kosa nami sikuliona.

Ikiwa hivyo ndivyo ilikuwa yeye kunielekeza basi nami
nitoe jibu.

Lakini anakuja na ghadhabu na matusi pasi na sababu.
Watu sasa wanayao kila mtu ana ghadhabu zake,wala usiliweke moyoni,....wanasema ukubwa jalala.
 
Tusker...
Kila inapotokea nafasi In Shaallah nitajaribu kueleza kile ninachokifahamu.
Maalim wangu salaam aleykum, mi nilikutana na Juma Kubbe juzi msikiti wa Mwembe chai kwenye kisomo cha tahtim ya Marehemu Bi Tatu Mrisho mke wa Rahim Lumelezi aliyekuwa mchezaji wa Simba Sports Club basi Sheikh Thabit alimwita kwa jina lake la utani Jimmy Lover nilimuona Juma kubbe akitabasamu kama hulka yake ilivyo siku zote ni mtu wa kutabasamu na mas'hara sana.
 
Tusker...
Kila inapotokea nafasi In Shaallah nitajaribu kueleza kile ninachokifahamu.
Juma kubbe na mtaa Stanley Aggrey habanduki kwenda kukote alipisha ujenzi wa ghorofa uishe karudi hapo hapo mpaka leo! Nyumba yao ya miaka ya nyuma ilikuwa nyumba no.74 na Mzee wake marehemu Mzee Khamisi Kubbe Msukuma mjanja aliyekuwa akitengeneza vifaa kama ndoo za bati,sufuri,koroboi,machekeche na vinavyohusiana na mabati hapo nyumbani kwake kabla ya kuhamia Gerezani,nimemwita mjanja kwa sababu alikuwa na soko la kuuza vifaa hivyo mpaka Mwanza zama hizo za miaka ya sitini!.
 
Slim5,
Ahsante sana.

Kulikuwa na somo yako hapa Dar anaitwa Slim.
Alikuwa mtu wa mikasa kweli kweli.

In Shaallah iko siku nitaleta visa vyake hapa barzani.

Kama Dar ya 1970 kulikuwa na wajanja 10 na yeye
namba yake imo humo tena nafasi za matawini.
Allah akbar. Sheikh nasubiria kwa hamu hilo andiko.
 
Juma kubbe na mtaa Stanley Aggrey habanduki kwenda kukote alipisha ujenzi wa ghorofa uishe karudi hapo hapo mpaka leo! Nyumba yao ya miaka ya nyuma ilikuwa nyumba no.74 na Mzee wake marehemu Mzee Khamisi Kubbe Msukuma mjanja aliyekuwa akitengeneza vifaa kama ndoo za bati,sufuri,koroboi,machekeche na vinavyohusiana na mabati hapo nyumbani kwake kabla ya kuhamia Gerezani,nimemwita mjanja kwa sababu alikuwa na soko la kuuza vifaa hivyo mpaka Mwanza zama hizo za miaka ya sitini!.
Mtebetini,
Mzee Khube ni baba yangu.

Kama hivi namuona pale barazani kwake alipokuwa akifanya
shughuli zake kabla ya kuhamia Gerezani na kuwa na kiwanda
kikubwa katika miaka ya 1970.

Allah amrehemu mzee wetu.
 
Maalim wangu salaam aleykum, mi nilikutana na Juma Kubbe juzi msikiti wa Mwembe chai kwenye kisomo cha tahtim ya Marehemu Bi Tatu Mrisho mke wa Rahim Lumelezi aliyekuwa mchezaji wa Simba Sports Club basi Sheikh Thabit alimwita kwa jina lake la utani Jimmy Lover nilimuona Juma kubbe akitabasamu kama hulka yake ilivyo siku zote ni mtu wa kutabasamu na mas'hara sana.
Mtebetini,
Umenitajia Rahim Lumelezi nilicheza nae Congo United katika 1970s.

Majuzi nimekutana na dada yake Diana nilikuwa sijamuona miaka
mingi akanifahaisha kuwa alihamia Uingereza miaka mingi.

Wanamajlis tuwieni radhi kidogo kwani taarifa kama hizi ni nje kidogo
ya ukumbi.
 
Othiambo,
Hakika nyakati zile wazee wakituhimiza sana kuhusu adabu.
Walikuwa na neno lao wakituasa,''Usitutukanishe.''

Maana ikiwa mtoto atakosa adabu watu watajua mama yake
hakumfunza adabu na hili kwao lilikuwa tusi kubwa.

Ustaarabu bado ungalipo ni wajibu wetu kuwafunza wanetu
na hata hapa barzani ikiwa unahisi mtu hakupata malezi kwao
kwa njia ya utaratibu unamuelekeza kuwa huenda huko kwenu
si vibaya lakini haifai kufanya kadha wa kadha kwenye kadamnasi.
Ni kweli kabisa na kila mtu mzima alikuwa ni mzazi pia kwani aliweza kumuadibisha mtoto yoyote aliyekosa mahapa popote pale anapoona inafaa.
Na ikitokea baada ya hapo akamhadithia mzazi halisi basi kesi na adhabu huanza upya kabisa.
 
Ni kweli kabisa na kila mtu mzima alikuwa ni mzazi pia kwani aliweza kumuadibisha mtoto yoyote aliyekosa mahapa popote pale anapoona inafaa.
Na ikitokea baada ya hapo akamhadithia mzazi halisi basi kesi na adhabu huanza upya kabisa.
Abunuwasi,
Sisi tulikuwa tunakatazwa kwenda kuogelea pwani.

Wazee walikuwa wanahofu tusije tukazama.

Lakini tukienda kuogelea kwa siri sana na pale ilipo
ofisi ya Azam Marine kulikuwa na pipa la maji baridi.

Tukishatoka kuogelea tunakuja pale kuoga katika lile
pipa kuondoa chumvi ili nyumbani tusijulikane.

Kazi ilikuwa wakati wa kurudi tusikutana na mtu akenda
kusema katuona Uzunguni.

Kule kote kulikuwa kunaitwa, ''Uzunguni.''

Ikiwa tutamuona mtu anatufahamu kwa mbali tulikuwa
tunajificha.

Lakini kama ujuavyo siku za mwizi 40.

Tulipotimia umri wa kati tuko sekondari ''past time,'' kubwa
ilikuwa ''movies'' Empire Cinema mchana Jumamosi na Jumapili.

Tukiangalia, ''Westerns.''

Hii wazee wenyewe wakifurahi unapewa shilingi moja na senti
ya soda ila unakumbushwa kurudi nyumbani mapema.
 
Abunuwasi,
Sisi tulikuwa tunakatazwa kwenda kuogelea pwani.

Wazee walikuwa wanahofu tusije tukazama.

Lakini tukienda kuogelea kwa siri sana na pale ilipo
ofisi ya Azam Marine kulikuwa na pipa la maji baridi.

Tukishatoka kuogelea tunakuja pale kuoga katika lile
pipa kuondoa chumvi ili nyumbani tusijulikane.

Kazi ilikuwa wakati wa kurudi tusikutana na mtu akenda
kusema katuona Uzunguni.

Kule kote kulikuwa kunaitwa, ''Uzunguni.''

Ikiwa tutamuona mtu anatufahamu kwa mbali tulikuwa
tunajificha.

Lakini kama ujuavyo siku za mwizi 40.

Tulipotimia umri wa kati tuko sekondari ''past time,'' kubwa
ilikuwa ''movies'' Empire Cinema mchana Jumamosi na Jumapili.

Tukiangalia, ''Westerns.''

Hii wazee wenyewe wakifurahi unapewa shilingi moja na senti
ya soda ila unakumbushwa kurudi nyumbani mapema.
Clint Eastwood????
 
Clint Eastwood????
Abunuwasi,
''The Good, The Bad and The Ugly...'' my all time favourite Western.
Giuliano Gemma, Anthony Stefen, Ferdinando Sancho...

Umenipeleka mbali sana.
Hapa kwangu nina projext size ya mkono.

Usiku ''sitting room,'' yangu huwa ''theater'' nina ''classics,'' nyingi na sichoki
kuziangalia - ''Lawrence of Arabia,'' ''The Guns of Navarone,'' ''Blue Hawaii,''
Elvis huyu.

Hii movie niliiona siku ya Eid Fitr Empire 1964 nilikuwa na miaka 12.
Ndipo nilipoamua kujifunza kupiga guitar na kuimba.

Zingine nikiziangalia na marehemu baba yangu katika 1960s...

Huwa narudi nyuma sana utotoni niko kizani peke yangu najihisi niko
Empire.

Nikipenda pia kusoma ''comics'' nilipokuwa mtoto kisha novels nilipopata makamo.
 
Abunuwasi,
''The Good, The Bad and The Ugly...'' my all time favourite Western.
Giuliano Gemma, Anthony Stefen, Ferdinando Sancho...

Umenipeleka mbali sana.
Hapa kwangu nina projext size ya mkono.

Usiku ''sitting room,'' yangu huwa ''theater'' nina ''classics,'' nyingi na sichoki
kuziangalia - ''Lawrence of Arabia,'' ''The Guns of Navarone,'' ''Blue Hawaii,''
Elvis huyu.

Hii movie niliiona siku ya Eid Fitr Empire 1964 nilikuwa na miaka 12.
Ndipo nilipoamua kujifunza kupiga guitar na kuimba.

Zingine nikiziangalia na marehemu baba yangu katika 1960s...

Huwa narudi nyuma sana utotoni niko kizani peke yangu najihisi niko
Empire.

Nikipenda pia kusoma ''comics'' nilipokuwa mtoto kisha novels nilipopata makamo.
Maalim wangu umenifanya nimkumbuke marehemu Baba yangu kwa kuwataja hao wababe wa classic movies,kuna One Silver Dollar,Seven dollars to kill you. Mimi pamoja na kuwapenda hao kipenzi changu mwingine alikuwa Charles Bronson.
 
Maalim wangu umenifanya nimkumbuke marehemu Baba yangu kwa kuwataja hao wababe wa classic movies,kuna One Silver Dollar,Seven dollars to kill you. Mimi pamoja na kuwapenda hao kipenzi changu mwingine alikuwa Charles Bronson.
Mtebetini,
My all time favourite ya Charles Bronson ni ''Chatoo's Land.''
 
Bansen...
Utadhani ilikuwa jana tu.
Namshukuru Allah kwa kunileta wakati ule...

Those were the days we thought would never end...
You can say that Again and Again bro we were blessed to experience our childhood during that period. Unakumbuka ujanja wetu kwa wasichana uliishia kwenda kwenye buggy splendid new palace, anatoglo], movies,parties lakini hakukuwepo na pombe?? na mwisho wa yote tuliridhika kwa busu tu.
 
Ni kweli kabisa na kila mtu mzima alikuwa ni mzazi pia kwani aliweza kumuadibisha mtoto yoyote aliyekosa mahapa popote pale anapoona inafaa.
Na ikitokea baada ya hapo akamhadithia mzazi halisi basi kesi na adhabu huanza upya kabisa.
Hivi jamani mnamkumbuka mzee Mpangile pale kwenye makaburi ya kisutu ambaye wakati tukiwa wadogo tulikuwa tunakwenda kupopoe maembe maeneo yale naye alikuwa anatufurusha mbio ilikuwa kama mchezo wa paka na panya pale-
Mwenyezi mungu amlaze mahala pema babu yetu yule
 
You can say that Again and Again bro we were blessed to experience our childhood during that period. Unakumbuka ujanja wetu kwa wasichana uliishia kwenda kwenye buggy splendid new palace, anatoglo], movies,parties lakini hakukuwepo na pombe?? na mwisho wa yote tuliridhika kwa busu tu.
Abunuwas,
Mimi nina dairy zangu za kuanzia 1968 huwa nikisoma nachoka.
Huwa siwezi kwenda hata kurasa tatu nafunga.

Nidhamu yetu ilikuwa ya hali ya juu na tukipenda shule.
Tulijua wakati wa kucheza na wakati wa kufanya kazi.

Usinikumbushe party za December shule zikifungwa!
The roaring 60s.

Iko siku nilikuwa London Liverpool Coach Station nimekuja kupanda
basi kwenda Glasgow.

Kuna kijimkahawa kila nikifika pale huwa nakwenda kupata chai.
Nje ya hicho ki-cafe naona picha ya Helen Shapiro.

Nikumuusudu sana huyu dada uimbaji wake enzi za 1960s.
Nasoma ile ''poster,'' naona imeandikwa, ''Jesus for Jews.''

Helen Shapiro amekuwa ''Born Again,'' na tangazo linasema atakuwa
shamba gani sijui anafanya mahubiri.

Nilichoka.
Hakika siku zimekwenda.

Nikamkumbuka Helen Shapiro kwenye movie na Billy Fury, ''Play It Cool.''
''Skirt,'' yake iko magotini au juu kidogo.
 
Back
Top Bottom