Nyumba ya msanii Batuli yaungua moto

Hivi hawa wasaniii hizi nyumba wanazitoa wapi na kazi hawana
 
Amekimbilia kucheka na JK na magufuli bila kuangalia usalama wa nyumba yake kwanza? maskini na JK muda wake ndio umekwisha aombe magufuli awe na nyota ya wasanii., kama ndie yule ajae.
 
Ccm hoyeeeeeee..... bado ya shoga angu sepetungaaaa
 
Nyumba yake au aliyopanga/pangishiwa? pole lakini.
 
Nyumba ya muigizaji wa filamu, Batuli imetekea kwa moto. Nyumba hiyo ipo maeneo ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam
“Nilikuwa saluni najiandaa ili niende kwenye fainali za TMT ndipo nilipopigiwa simu na majirani majira ya saa tatu usiku kuwa nyumba yangu inaungua na imeteketea yote kwa moto,” Batuli aliiambia Clouds FM.
“Iliniuma sana vitu vilivyonusurika ni magari yangu tu mawili,” alisema kwa uchungu.
Aliongeza kuwa majirani walihisi chanzo cha moto huo kinaweza kuwa ni umeme. Hata hivyo hakuna aliyejeruhiwa.
 
Hii nyumba alikuwa amepanga tuu!
 
Jana alikuwa zake fiestan jangwan anaselebuka sijui wamemuahidi kumjengea nyingine

Hahaha aitoe wapi hiyo nyumba....wanauza sura show off nyingi....
Kuwa baba mama mwenye nyumba kwa bongo movie naona ni mwiko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…