Nyumba za kupanga ni mateso sana

Nyumba za kupanga ni mateso sana

We fala umenichekesha sana ila acha uboya! Ongeza upange Apartment ni aghali ila kuna raha yake amini nakwambia. Jichange change tu ukae kwako ukiwa fully fledged ukiingia ndani kwako unakuwa unamaliza mambo yote yani kinachokutoa nje ni kuanika nguo tu.

Pia utakuwa unaishi na watu wenye class katika mazingira hayo sababu wambea wambea hawawezi ku afford kodi ya laki 2 au zaidi kwa mwezi [emoji23][emoji23][emoji23] labda wawe ni genge la wadangaji!

Nimeishi maisha yote ya kukaa nyumba ya mama mwenye nyumba njaa njaa na mkuda anakufatilia na kudai kodi before time na nyumba ambayo mmiliki ni Don hakai hapo! Raha ni kukaa kwenye nyumba ambayo mwenye nyumba ana mishe zake sio kutegemea kodi za nyumba na anakaa mbali na hapo!

Tafuta nyumba ya aina hio mzee utakuja kuniambia!
Aya bn
 
Daah pole sana fanya uondoke tu hapo.

Kuna nyumba niliwahi panga ilikuwa ni room za ndani miaka ya nyuma kidogo basi mwenyewe kutwa kusikiliza nyimbo za taifa nasauti anaweka ya juu hasa au ya afrika mashariki au ile tazama ramani.

Kuna siku nilimuomba apunguze sauti kidogo nilimindiwa sana kuwa mimi si mzalendo.
 
Mkuu kama anamtoto wa kike hata kama sio pisi kali mpelekee moto mkeka hautatandikwa karibu na choo niamini mimi
 
Back
Top Bottom