Obama: Huwezi kusema una Demokrasia ukashinda kwa 90% + huku upinzani umeufungia, uhuru wa habari hakuna

Obama: Huwezi kusema una Demokrasia ukashinda kwa 90% + huku upinzani umeufungia, uhuru wa habari hakuna

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2012
Posts
4,572
Reaction score
26,885


Alisema: huwezi kuwa na Demokrasia na ukashinda kwa zaidi ya 90+ huku mpinzani wako umemfunga, hakuna uhuru wa habari, hakuna uhuru wa vyama kukutana, kufanya mikutano, uhuruwa kukosoa serikali, hakunataasisi imara za check and balance ukasema kuna demokrasia.

Unafanya uchaguzi kujidanganya

----
ALIYEKUWA RAIS WA MAREKANI AKIZUNGUMZIA DEMOKRASIA
-
Tunatakiwa kuacha kujifanya kuwa, Nchi kufanya Uchaguzi wakati muda mwingine mshindi hupata zaidi ya asilimia 90 ya kura kimaajabu kwa sababu Wapinzani wote wamefungiwa, ni demokrasia.

Demokrasia inategemea Taasisi imara, inahusu haki ndogo ndogo, mfumo unaoangalia usawa bila watu au Taasisi fulani kuwa na nguvu kuliko nyingine, uhuru wa kutoa maoni, uhuru wa kujieleza, Uhuru wa Vyombo vya Habari, haki ya kuandamana, kuihoji Serikali, Mahakama huru na Kila mmoja kuofuata Sheria.
 
US wenyewe hawana democracy kabisa sababu wana kitu kinaitwa Selection of the Electors ambayo ndio yenye Sauti ya mwisho kuliko kura za wananchi wote.

The Electoral College process consists of the selection of the electors, the meeting of the electors where they vote for President and Vice President, and the counting of the electoral votes by Congress. The Electoral College consists of 538 electors.

Ikumbukwe Trump kaiba kura kwa msaada wa Russia na hakuna kilichofanyika
 
Hiyo Ndio demokrasia

Kama hujajipanga unajiandaa kwa wakati mwingine

TLP itatoa ushindani Sasa
 
Obama kwa amefanya uchumi wa Marekani uyumbe huyo ni dhaifu hana lolote hawezi kumfkia Mzalendo Magufuli
Kwa uchapa Kazi
 
Back
Top Bottom