Ofa (nusu bei) ya Shoprite imenipa mtaji wa kufungua duka reja reja

M24 Headquarters-Kigali

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2012
Posts
8,199
Reaction score
8,186
Juzi nikiwa mlimani city nikashangaa nyomi ya watu wakikimbilia Shoprite supermarket kuuliza kulikon nikaambiwa kuna ofa (nusu bei, 50% OFF) nami nikachoma ndani kuwahi ofa ile kuingia tu mbinde kufika ndani ikawa purukushani kwa kweli yaani ni vurugu tupu mi nikawahi mikuku almost friji Zima, konyagi, mi-whisky, mafuta ya kupikia (50 lts) sukari 250 kgs, sabuni za kuogea box 10, OMO kubwa 20. sasa jana nimedamka alajiri saa 11 kuwahi tena ofa nakutana na tangazo ofa imesitishwa. Daah but si mbaya nimepata pa kuanzia. Shikamoo SHOPRITE!!
 

Attachments

  • offa.jpg
    56.6 KB · Views: 1,087
  • ofe.jpg
    23.3 KB · Views: 913

Mkuu angalia usijetuwekea sokoni bidhaa iliyoisha muda wa matumizi!
 
Mimi nasikitika sana hawa jamaa kuondoka,Na hawa Wakenya ni balaa, wataweka hadi walinzi Wakenya,
 
Hata kama vime-expire NO PROBLEM nina muhuri wangu, nafuta expire date ya zamani na kupiga mpya. Tena ya tarehe za 2015
 
kihemuhemu chako kikiisha, tulia chini uanze kukagua bidhaa moja baada ya nyingine uone mwisho wa matumizi yake(expire date),,,kama zimezidi mwezi huu basi umeokota dodo kwenye shina la mbilimbi.
 
haka kauzi kamenikumbusha zile Bavaria za kariakoo,,,nilinunua carton nzima kumbe kesho yake ni mwisho wa matumizi,,,,daaah! hizi biashara za wahindi hizi, yaani muhindi yupo tayari akuuzie kitu cha elfu 10 kwa elfu 3 kuliko akupe bure bila kujali ubora wa hicho kitu.
 
Ile ofa ya Nakumat imekumbushia zama zile watani wa jadi walivyokuwa wakija na masabuni, dawa za meno, wanawarushia watanzania kabla ya kucheza mechi uwanja wa taifa kwenye michuano ya chalenji au ya klabu afrika afrika mashariki, kipindi hicho siyo kombe la Kagame.

Iikuwa kama enzi za maduka ya ugawaji watu walikuwa wanapigana vikumbo na kunyang'anyana bidhaa mikononi kama wapo kwenye njaa ya kutisha. Ilikuwa ni aibu aibu aibu kwa njaa walionesha watanzania mbele ya uwekwezaji wa majirani zetu wa karibu tu watani wa jadi. Laiti, habari hii ingetangazwa mapema na hizi habari kufika mpaka maeneo ya wale ya wananchi wa kawaida ingekuwa habari nyingine. Watu waliingia asubuhi na kulipa bill usiku sababu ya misululu ya foleni.
Watu walikula na kunywa pombe, na vinywaji baridi ndani ya Super market, na walikuwa wanakwimba nyimbo kama wapo PARADISO.

Ama kweli ilikuwa tafrani ya aina yake, na kielelezo cha Utanzania wetu kwenye mambo ya MDEBWEDO.
 

Yaani wewe ndiye uliyefungua ofisi tatu za bima Mbeya na kuanza kulaumu uchawi, leo unakimbilia bidhaa za nusu bei ambazo hata hujui zinaexpire lini?

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…