Ofisa Biashara United alalamika kupigwa na 'makomandoo' wa Yanga

Ofisa Biashara United alalamika kupigwa na 'makomandoo' wa Yanga

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Kabla ya mchezo wa Yanga dhidi ya Biashara United uliopigwa Jumanne Februari 15, 2022 kwenye Uwanja wa Mkapa, kulitokea mvurugani baina ya ofisa wa Biashara United na wale aliowaita makomandoo wa Yanga.

Huyu hapa ofisa huyo anaelezea kilichotokea kabla ya mchezo huo wa Azam Sports Federation Cup kuanza.

“Mimi naitwa Alphat Juma, asubuhi ya leo (jana) baada ya kikao cha pre-match pale Uwanja wa Karume, Kamisaa akaturuhusu kwenda Uwanja wa Mkapa kukagua vyumba.

“Tulipofika tukakuta kuna dada wa JKT, akanionyesha vyumba viwili, nikachagua kimoja na kusaini kisha nikaingia ndani.

Wakati nakagua, wakaja security wamezaa sare zao nyekundu wakanilazimisha nifungue mlango, nilipofungua wakanivamia na kaunza kunipiga.

“Walikuwa wengi ikabidi nitoke, nilimjulisha Team Manager kwa njia ya simu na baadaye tukamjulisha Kamisaa wa mchezo ambaye alikuwa msibani.

“Nawajua na nimewakariri, hata sasa nikiwaona nawajua, ni watu wa Yanga, kuna mmoja wao wakati nakabana naye nilimsikia wanamuita Kondo.

“Alikuja hadi bosi wao wa JKT akasema hawa watu si wa Yanga kwa nini wanaingia vyumba vya Biashara? Nimeumizwa sana na walichokifanya.

“Tumesharipoti kote ikiwemo kwa TFF. Na kulikuwa na semina ya waamuzi hapa wameona kila kitu.”

55.JPG
 
Tutafika tu..... wanakotaka tufike
 
Mwanaume unapata wapi nguvu ya kujitokeza kwenye camera na kujisifia eti umepigwa na wanaume wenzako? Alitakiwa apambane nao mpaka mwisho!

Aache kutafuta huruma. Au kama vipi akawashtaki. Si amekiri mwenyewe anawafahamu mpaka kwa majina yao?
 
Nikisema wapigwe tu nitakula ban na nikisema wasipigwe nitakula ban yaani hii nchi ngumu kama mfupa wa tembo mademu wazee,kazi ngumu,pombe kali,jf ban,kitanda kungunu juu mbu neti hazigawiwi ckuizi,barabara tope,mwenye nyumba anataka pango Kwa miezi 6,ajira hakuna, mbowe gaidi,demu japo mzee ila anaomba hela. Stephen aliuliwa kwa stress kama hizi huko na Jewish
 
kama alivyo sema mhanga 'walio mtandika walikuwa wamevaa nguo nyekundu', sasa apo si kesi imekwishaa??? tangu lini wananchhi wakavaa nguo nyekundu?? inavyo elekea hapo aliye piga na aliye pigwa wootee ni mikia hiyoooo
 
Mwanaume unapata wapi nguvu ya kujitokeza kwenye camera na kujisifia eti umepigwa na wanaume wenzako? Alitakiwa apambane nao mpaka mwisho!

Aache kutafuta huruma. Au kama vipi akawashtaki. Si amekiri mwenyewe anawafahamu mpaka kwa majina yao?
We lijinga tu, juzi hapo mashabiki wenu wa utopolo waliwamwagia mkojo mashabiki wa simba kwenye Mchezo wa Simba SC vs Asec Mimosas, walipotandikwa mkatoa kila aina ya lawama na malalamiko.

Unadhani kupigana na kundi la watu ni rahisi?

Tumia akili zako vizuri!
 
Hili tukio ni kweli kabisa limetokea huyu jamaa kapigwa haswaa!! Ila wachambuzi wa michongo hautawasikia wakiongea chochote.. wenyewe wanasubiri match za simba tu ndo pakukuzia brand zao na kuongeza followers kwenye page zao..
 
We lijinga tu, juzi hapo mashabiki wenu wa utopolo waliwamwagia mokojo mashabiki wa simba kwenye Mchezo wa Simba SC vs Asec Mimosas, walipotandikwa mkatoa kila aina ya lawama na malalamiko.

Unadhani kupigana na kundi la watu ni rahisi?

Tumia akili zako vizuri!
Utopolo + wandishi wao wa habari ni kama kuku wa kienyeji.. niwasahaulifu sana.... ndugu zao walivyopewa kipondo ma mashabiki wa simba juzi walihamasishana na wachambuzi wao wa michezo kulilia na kuilani simba sasahiv hazijapita hata siku tatu wanafanya tukio la aina ileile halafu wako kimya...
 
Nikisema wapigwe tu nitakula ban na nikisema wasipigwe nitakula ban yaani hii nchi ngumu kama mfupa wa tembo mademu wazee,kazi ngumu,pombe kali,jf ban,kitanda kungunu juu mbu neti hazigawiwi ckuizi,barabara tope,mwenye nyumba anataka pango Kwa miezi 6,ajira hakuna, mbowe gaidi,demu japo mzee ila anaomba hela. Stephen aliuliwa kwa stress kama hizi huko na Jewish
Mamantilie nao hawajazi vizuri sahani ya ukoko wa wali (zege) kama zamani. Kwenye netball wanavaa skintight kiasi kwamba hatuoni 'mambo' vizuri kama zamani, I hate modern netball. Nilikuwa natoa michango na sadaka kanisani vizuri tu, mambo yalipochachia kila mtu amenitenga, Katekista siku hizi hununui vocha?
 
We lijinga tu, juzi hapo mashabiki wenu wa utopolo waliwamwagia mokojo mashabiki wa simba kwenye Mchezo wa Simba SC vs Asec Mimosas, walipotandikwa mkatoa kila aina ya lawama na malalamiko.

Unadhani kupigana na kundi la watu ni rahisi?

Tumia akili zako vizuri!

Tatizo la nyinyi watoto wa siku hizi mayai mayai mengi! Halafu tangu lini hao makomandoo wa Yanga wakavaa nguo nyekundu?
 
Tatizo la nyinyi watoto wa siku hizi mayai mayai mengi! Halafu tangu lini hao makomandoo wa Yanga wakavaa nguo nyekundu?
Kwa akili yako finyu, kuvaa nguo nyekundu ndiyo kuwa siyo Yanga?

Mna akili fupi sana, walivaa vile ili washukiwa wawe Simba siyo? Mbinu ya kishamba hata mtoto anaing'amua.
 
Kwa akili yako finyu, kuvaa nguo nyekundu ndiyo kuwa siyo Yanga?

Mna akili fupi sana, walivaa vile ili washukiwa wawe Simba siyo? Mbinu ya kishamba hata mtoto anaing'amua.

Dogo huna ushahidi! Na uache kiherehere. Kama huyo jamaa yako anawafahamu hao wababe wake, si akashtaki?

Hivi ni kwa nini vijana wa siku hizi mnapenda sana kulia lia na kutaka kuonewa huruma, pasipo sababu za msingi?
 
Back
Top Bottom