LGE2024 Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi yafungwa Songwe, Wanachama CHADEMA walia kufanyiwa rafu

LGE2024 Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi yafungwa Songwe, Wanachama CHADEMA walia kufanyiwa rafu

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

SAUTIYANGU

New Member
Joined
Oct 23, 2024
Posts
4
Reaction score
2

WhatsApp Image 2024-10-31 at 13.53.19_b96a8f24.jpg

Ofisi ya msimamizi wa Uchaguzi kata ya Sogea Mjini Tunduma imefungwa kwa muda usiojulikana katika kipindi hiki cha Uchukuaji na urejeshaji wa Fomu za wagombea huku chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)kikilalamikia kunyimwa nakala ya Fomu walizorejesha kwaajili ya uteuzi wa wagombea.

Wakizungumzia changamoto hiyo viongozi wa CHADEMA pamoja na wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Serikali za mitaa katika kata hiyo wamedai mnamo tarehe 26 Mwezi huu walichukua na kurejesha fomu lakini walipoanza kufuatilia nakala ya Fomu waliyotakiwa kupewa kwa Mujibu wa Utaratibu kila wanapofuatilia wanakuta ofisi hiyo imefungwa.

Kwa upande wake Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Tunduma Bi Mariam Chaurembo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Mji Tunduma amekiri kuwepo kwa Changamoto hiyo na kuwasihi wanachadema kuwa warulivu wakati wanashughulikia changamoto hiyo kwani fomu zao zimepokelewa na kufungiwa katika chumba ambacho hawawezi kuzichambua kwa sasa mpaka itakapofika hatua ya Uteuzi.
WhatsApp Image 2024-10-31 at 13.54.37_f60bfc12.jpg

WhatsApp Image 2024-10-31 at 13.54.35_86b9ed5e.jpg
 
Back
Top Bottom