Uchaguzi 2020 Ofisi za CCM wilaya ya Kinondoni watu wamepanga foleni ndefu wakisubiri kuchukua fomu

Niko hapa Kinondoni Mkwajuni aisee watu wameamua maana siyo kwa umati huu. Naambiwa watia nia wamefika hapa tangu saa 10 Alfajili kuwahi nafasi ili ofisi zikifunguliwa wawe wa mwanzo.
Mimi nimeona nikadhani ni wadhamini wa mgombea maarufu wamempenda, wanasubiri achukue fomu wamdhamini. Kumbe wanasubiri kuchukua fomu wawe wagombea!?
 
Bila picha jamani?????
 
Dah hizi siasa bhaana[emoji23][emoji23]
Mkuu siyo siasa,bali ni ugumu wa maisha,ajira hakuna.Unakumbuka miaka minne iliyopita,uhamiaji walitangaza nafasi za kazi 80 kama sijakosea,siku ya usaili wasailiwa walijitokeza zaidi ya 12,000/ ilibidi wafanyie uwanja wa Taifa.
 
Usisahau bahasha za milioni kumi kwa kila mbunge kupitisha miswaada yenye maslahi kwa wakubwa.
 
Mimi nimechukuwa Iringa mjini bwashee.

Jukumu langu la kwanza nililoombwa na wanyalu ni kuhakikisha Lipuli wana Paluhengo hawashuki daraja.
Kumbe bwashee wewe ndio Pierre Liquid? Ndio mana nyuzi zako nyingine hazieleweki.
 
Ubunge umefanywa sio uwakilishi tena ni sehemu ya kuongeza kipato

Wapi Rita Poulsen, Master J na wenzao? Kutia nia imekuwa Bongo Star Search nyingine.

Watu watu wanajitafutia umaarufu badala ya kujikita kwenye uzalishaji wa mali.

Hatuendi popote kama taifa kwa vimbwanga hivi.
 
Wewe punguza basi huo usukununu wako, unaleta habari inayohitaji kuwa na picha, lkn unashindwa kutuaminisha kwa hilo
 
Labda lipuli ya kongwa kwenu msiyo jua kuwa mwl JK Nyerere alisha fariki
Mimi nimechukuwa Iringa mjini bwashee.

Jukumu langu la kwanza nililoombwa na wanyalu ni kuhakikisha Lipuli wana Paluhengo hawashuki daraja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…