Ofisi za Maprofesa na Madaktari wa UDSM zinathibitisha namna Taifa lilivyofeli. Je, hata majumbani kwao wanaishi kwa dhiki hivi?

Ofisi za Maprofesa na Madaktari wa UDSM zinathibitisha namna Taifa lilivyofeli. Je, hata majumbani kwao wanaishi kwa dhiki hivi?

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Naomba niseme ukweli kwamba ukitembea vyuo vikubwa Duniani utabaini Ofisi za waalimu ( Tutorial/Dr/Prof) NI eneo ambalo mnaweza mkakaa nakufanya majadiliano mkiwa na facilities zote.

For the first time nimefika university of Dar es salaam kumwona rafiki yangu ambaye nilisoma naye Ila Kwa sasa ni mwajiriwa wa Chuo kikuu cha DSM. Niseme ukweli hata yeye nafsi ilimsuta kunikaribisha ofisini kwake lakini hakuwa na jinsi ikabidi anialike.

Mazingira niliyoyakuta pale yanatia huruma. Hata kama ndo mnasubiri serikali iwajengee Ofisi hapana Madaktari na Maprofesa badilikeni. Haiwezekani sehemu mnayokaa Kwa zaidi ya masaa nane Kwa iwe mbovu kiasi hicho, chumba kimoja kidogo mnajibana wawili au watatu... Mnatumia public toilet, hakuna TV, hakuna desktop, laptop zenyewe zimechoka. Bora nisingeyafahamu haya nikanyamaza lakini naamini nikiandika hapa ntawaamsha watu kwenda kuwatembelea waalimu wao na kuwapa zawadi za meza za kisasa, viti vya kisasa, TV NK.

Labda nimeover expect lakini prof anapaswa awe mtu anayejijali, anayepokea machapisho na kuaandaa machapisho, anayefanya consultation every time that means anapaswa kuwa na Ofisi ambayo inamsadia kutekeleza majukumu yake.

LABDA NITOE USHAURI
1. Pamoja na miundombinu finyu, chuo kila Prof awe na chumba chake chenye meza nzuri, milango mizuri, TV na desktop

2. Tengeni vyumba maalum ambapo watakaa wasaidizi wa Maprofesa. Kwa maana nyingine incase kuna mwanafunzi au MTU anakuwa na program mahususi na Prof basi awe na sehemu anapoweza kukaa na kufanya KAZI.

3. Wekeni bajeti ya chai angalau Kwa wazee na wasomi wetu hawa watulize ubongo na kuwaza mambo mazuri yakuishauri serikali.

4. Waunganisheni kwenye miradi ya serikali wakaome Ofisi na mandhari wanaoishi wahitimu wao.

5. Maprofesa na Madaktari mliotolewa jalalani please wasaidieni wenzenu kifikra waishi maisha ya KAZI yanayoendana na hadhi ya elimu waliyonayo.

6. Kwa kuwa serikali na Maprofesa wenzenu haitawatekelezea niliyoandika 1-5 basi tengeni bajeti mfanye maboresho ya Ofisi zenu kwani muda mwingi wa maisha yenu mnautumia chuoni na ofisini kuliko sehemu nyingine yoyote. Mkikosa Amani na Ofisi mnayokaa mtapata tatizo la kiafya ikiwemo afya ya akili. Kama ninyi niwaalimu wetu onyeshe uprofesa wenu kwenye mazingira yenu ya KAZI.

Hii nimeandika Kwa UDSM lakini naamini vyuo vingine hawa wasomi labda Wana Hali mbaya zaidi yakuishi mazingira Duni wakisubiri serikali na mwajiri afanye miujiza.

Rafiki yangu najua ujajua kwamba nimeumizwa na Ofisi zenu Ila tambua kubadilika kunaanza nawewe... Mnamiliki vipi maguorofa huku mkiishi kwenye Ofisi Duni? Maisha yako ya fahari unaweza unayatengeneza mwenyewe.

I'll be back kuona mmebadilika? Kabudi was right those days.
 
Kaushaa kaka wajomba zanguu wale kwao hata usipaongele dili na hukohuko ulikokuonaa hataree
 
Maprof wamekaa kugombeza wanafunzi tu utadhani siyo wasomi. Mpaka unawaonea huruma hao wanafunzi.

Kwa masaa sita niliyokaa pale nilibaini hata kazi za utafiti pale chuoni hazifanyiwi maboresho sahihi.Unasomaje andiko ya masters kwenye Ofisi zile? Yale mazingira ni Duni Sana.

Na hii Inapoelekea Maprofesa kujisifu Kwa kukaa na KAZI za wanafunzi miezi minne. Huyu ndugu yangu anaongea kabisa HAPA KWETU MWANAFUNZA ATOBOI KIRAHISI, WAKIJA KWA LENGO LA KUMALIZA CHUO WANAKOMA WENYEWE. WAKITAKA KUMALIZA CHUO WAENDE HUKO KWINGINE SIYO HAPA.

Huyu ni msomi mwenzetu anawaza wanafunzi wafeli na anaona kabisa yupo sahihi. Wakati huo yeye amesoma masters nakumaliza Bila kuzidisha siku katika vyuo ambavyo wenzetu wamewekeza na kujua umuhimu wa muda. Mwalimu anadai wao UDSM utafiti "partial fulfillment" unakaa examination miezi mitatu..80 pages unasahisha above 90 days?

Nimejifunza mengi Sana UDSm lakini fikra za wenye chuo zimechangia kudumaza wasomi wao na kuwafanya wawe Mungu MTU.

Just from discussion, they way wanafunzi wanavyokuwa kutreated, Madaktari wanavyojisikia na namna wanavyoishi hakuna ubora wa elimu. Panatakiwa reform , time management na environment ya utoaji elimu mpo nje kabisa ya Dunia.

Siku nyingine nawaambia nilichoona college ya engenering ; najua mwajua Ila tuwakimbushe may be watabadilika
 
Naomba niseme ukweli kwamba ukitembea vyuo vikubwa Duniani utabaini Ofisi za waalimu ( Tutorial/Dr/Prof) NI eneo ambalo mnaweza mkakaa nakufanya majadiliano mkiwa na facilities zote.
Chai tupu....,Hapo ulisema ...."HAPA HAWAMALIZI......BLA BLA "Inaconfirm kuwa wewe hukwenda kumtembelea rafikio bali ni mwanafunzi uliyefeli pale.Wasalimie kitaa, pitia njia nyingine.Acha kuchafua best brains.
 
Wewe unasema UDSM, UDOM wanapaka ukuta mavi baadhi ya wanafunzi, hawa si ndio ma professor wa siku za usoni
Kumbe ni baadhi ya wanafunzi, ....na sio kila anayefika university atakuwa Prof, wengine wamefika kwa bahati mbaya na huishia njiani...,huenda ndo hao unaowaonglea(if any).
 
Maprof wamekaa kugombeza wanafunzi tu utadhani siyo wasomi. Mpaka unawaonea huruma hao wanafunzi.

Kwa masaa sita niliyokaa pale nilibaini hata kazi za utafiti pale chuoni hazifanyiwi maboresho sahihi.Unasomaje andiko ya masters kwenye Ofisi zile? Yale mazingira ni Duni Sana.

Na hii Inapoelekea Maprofesa kujisifu Kwa kukaa na KAZI za wanafunzi miezi minne. Huyu ndugu yangu anaongea kabisa HAPA KWETU MWANAFUNZA ATOBOI KIRAHISI, WAKIJA KWA LENGO LA KUMALIZA CHUO WANAKOMA WENYEWE. WAKITAKA KUMALIZA CHUO WAENDE HUKO KWINGINE SIYO HAPA.

Huyu ni msomi mwenzetu anawaza wanafunzi wafeli na anaona kabisa yupo sahihi. Wakati huo yeye amesoma masters nakumaliza Bila kuzidisha siku katika vyuo ambavyo wenzetu wamewekeza na kujua umuhimu wa muda. Mwalimu anadai wao UDSM utafiti "partial fulfillment" unakaa examination miezi mitatu..80 pages unasahisha above 90 days?

Nimejifunza mengi Sana UDSm lakini fikra za wenye chuo zimechangia kudumaza wasomi wao na kuwafanya wawe Mungu MTU.

Just from discussion, they way wanafunzi wanavyokuwa kutreated, Madaktari wanavyojisikia na namna wanavyoishi hakuna ubora wa elimu. Panatakiwa reform , time management na environment ya utoaji elimu mpo nje kabisa ya Dunia.

Siku nyingine nawaambia nilichoona college ya engenering ; najua mwajua Ila tuwakimbushe may be watabadilika
"80 pages unasahihisha above 90 days?".

You have no idea!

Some cows exist in the form of human.
 
Chai tupu....,Hapo ulisema ...."HAPA HAWAMALIZI......BLA BLA "Inaconfirm kuwa wewe hukwenda kumtembelea rafikio bali ni mwanafunzi uliyefeli pale.Wasalimie kitaa, pitia njia nyingine.Acha kuchafua best brains.
Best brains 🤣 zimeshindwa hata kujitengenezea system ya maji safi kwenye community yao ya chuo, zile departments za Engineering sijui wanafundisha nini wakati hawawezi kujisaidia wenyewe mahitaji muhimu kama maji, chuo wana migawo ya maji kama manzese tuu ,ni aibu sana
 
Wewe naye! tangu lini majalala yakawa na mandhari ya kuvutia, mbona umemtaja Kabudi hivi hukumwamini alipomsifia JPM kwa kumtoa jalalani?
 
Baadhi ya vyuo vikongwe vinahitaji ukarabati maalum
 
Utu upo wapi, imani zimeenda wapi, picha za ofisi zipo wapi
 
Back
Top Bottom