Poleni sana, Kama kuna mwanasheria anaweza kutusaidia nilipata kusikia katika Power Breakfast ya Fina na Masoud walikuwa wanaongea na mwanasheria ambaye alikuwa akidadavua mantiki ya "Parking at owner's risk" kwamba haikubailiki kisheria.
Hata kama kuna kibao kinasomeka "Parking at owner's risk" bado mwenye eneo husika atawajibika kwa madhara yatakayo msibu mgeni wake, eneo lako, walinzi wako halafu mteja awajibike kwa uzembe wa mwenye hotel/Duka/Bar hii haijakaa vizuri.
Binafsi nilishaumia sana na wezi wa power window UDSM lakini walinzi wa chuo walifanikiwa kukamata wezi ambao nao wanakuja na gari na mnapaki pamoja, hiyo ya UDSM jamaa walitekeleza gari si unajua kuna mageti na ulinzi pale hata hivyo hatukujua mambo yaliishaje.
Please ukiibiwa usiende kununua spare za dili, ukinunua ujue unamuamishia maumivu mtu mwingine.