Katiba mpya si mali ya chama chochote ni mali ya wananchi. Na katiba mpya si utashi wa chama kipi kitupatie ni takwa la wananchi kama wakiitaka lazima ipatikane."
"Ni makosa vyama vya siasa kuhodhi mchakato huo na kusema bila sisi katiba mpya haiwezi kupatikana. Hakuna chama chenye mamlaka ya kuamua katiba mpya iweje. Mamlaka hiyo ni ya wananchi."
"Tatizo viongozi wetu wa CCM wanaona bado watu wamelala kule kwenye miaka ya giza. Lazima watofautishe wananchi alioongoza Nyerere na wananchi wa sasa" Thadei Ole Mushi, Kada wa CCM.
ALIANDIKA THADEI OLE MUSHI ENZI ZA UHAI WAKE.
Chama changu ni CCM, sina maslahi yoyote na Upinzani wala chadema ila Nina maslahi na uhai wa mtu. Nasikia Ndugai kaufuta Ubunge wa Lisu kisa hayupo bungeni na wala hajui yupo wapi.
Nafikiria Risasi 16 zilizotoboa mwili wa Tundu Lisu, nafikiria uwezo wa Mungu ambaye aliamua kutuonyesha kuwa yeye ndiye mwenye uwezo wa kuchukua Roho ya Mtu awapo hapa Duniani kwa kuwe yeye ni muumba....
Si Rahisi mtu kupigwa risasi 16 bado akawa anapumua, ni mamilioni ya watu wangapi Duniani waliwahi kuuliwa kwa risasi moja? Kwa nn Lisu apigwe 16 na bado aendelee kupumua?
Ni kipi cha muhimu hapa uhai au Ubunge? Ukiwa hai unaweza kuwa mbunge lakini ukiwa mfu huwezi kuwa mbunge. Lisu licha ya matibabu ya hospital anahitaji matibabu ya kisaikolojia huyu bado hajawa sawa hata kodogo.
Niwatake watanzania wote kuendelea kumuombea Lisu kwa kila Dua unayoweza, huyu kwangu ni mpinzani kwa kuwa nipo CCM lakini bado itikadi haiwezi kutuondolea roho ya ubinadamu tuliyoumbiwa na Mwenyezi Mungu. Thamani ya Ubunge haiwezi kulingana na thamani ya uhai.
Lisu anapambania afya yake, mguu wake kila Siku anasogeza bolt na machuma ili ukae sawa, mwili wake una machuma kila mahali ndani na njee ya mwili.... Huo Ubunge unamsaidia nini?
Najiuliza Spika aliwahi kumtembelea Mara ngapi Lisu? Je kama baba wa wabunge wote aliwahi kumpigia hata Lisu Simu? Aliwahi hata kumuuliza anaendeleje? Kama baba kweli mwanao anapigwa Risasi 16 hutamfuata Hospital, hutamjulia hali yake? Hii ndio Tanzania aliyotuachia Nyerere? Kweli hatuwezi kuona bado Lisu ni mgonjwa? Mbona mnacheza na Mungu?
Tumshukuru Mungu kwa kila Pumzi tuivutayo, kuna Siku hutaweza kujivika madaraka, wala nguo tutakuvika sisi tulio hai. Kila ukipita njiani tunapishana na karakana zinazouza majeneza haya yote yanatusubiri sisi tulio hai, waliokufa walishachukua ya kwao. Ya nn kungangana na madaraka ya hii dunia?
Wote ipo Siku tutafunga midomo yetu na tutaoza kabisa. Mtendee mwenzako wema.....
Tuzidishe maombi kwa Lisu bila kujali itikadi zetu.
Ole Mushi.
JUN 28. 2019
THADEI OLE MUSHI
amefariki leo tarehe 4.1.2024