Abdul-nasir
New Member
- Dec 25, 2011
- 4
- 0
Ninaanza kwa salamu kwani siku zote huwa ni jambo la hekima pale popote linapotamkwa(muhali gani), ingawa mimi ni mgeni katika JF ila nahisi umeongelea kitu ambacho moyo wangu umekuwa na shauku ya kuongezea chochote katika hili@Eiyer
Mda mwengine ufahamu mbaya juu ya mambo unaweza ukapelekea product mbaya ya mambo kwani kile ambacho kitakuwa kinaendelea kitakuwa asili yake ni kutokana na ule ufahamu uliobebwa.
Maana ya kuabudu ni kufanya kitu chochote kile chini ya sheria ya Mungu, nasiyo kuenda misikitini au makanisani tu, halafu ukitoka huko Mungu hayupo ni sawa na kuwa na mzazi halafu ukamwambia awe mzazi wako nyumbani tu halafu ukitoka nje hamjuani. Mungu baada ya kumumba binadamu hakumuacha tu aishi tu anavotaka yeye tu, kwasababu alijua kuwa matatizo ni jambo ambalo litakuwa haliepukiki kwake yeye. hivyo alimpa muongozo kupitia huo jinsi gani aishi, kwavile yeye ndiye aliye tuumba basi bila shaka anatujua zaidi kuliko sisi kwa sisi tunavojuana.
Matatizo yote ambayo hii leo dunia inakumbana nayo ni matokeo ya mifumo ya maisha ambayo binadamu waliojitungia wao wenyewe kutoka vichwani mwao nakupangiana sheria ambazo asili wamezitunga wao, huku wakisahau tabia za kimaumbile ambazo wao wanazo, za kuathiriwa na mazingira waliyonayo, kwa kawida binadamu anatabia ya ubinafsi, ambayo inapelekea kujivutia vitu kiupande wake, ndomana leo tunaona wamiliki wa mfumo wa ubepari ambao tunaenda nao leo hii duniani wa kiwa juu na kuwaonea walioko chini, pia wakiendelea kutuletea sheria mbalimbali ambazo kimsingi haziendani na maumbile ya binadamu ndo mana matatizo, amani na utulivu wa nafsi kwa binadamu ni jambo ambalo halipo.
"kwahakika binadamu amepewa elimu ndogo tu" AL Qur-an Karim
Mda mwengine ufahamu mbaya juu ya mambo unaweza ukapelekea product mbaya ya mambo kwani kile ambacho kitakuwa kinaendelea kitakuwa asili yake ni kutokana na ule ufahamu uliobebwa.
Maana ya kuabudu ni kufanya kitu chochote kile chini ya sheria ya Mungu, nasiyo kuenda misikitini au makanisani tu, halafu ukitoka huko Mungu hayupo ni sawa na kuwa na mzazi halafu ukamwambia awe mzazi wako nyumbani tu halafu ukitoka nje hamjuani. Mungu baada ya kumumba binadamu hakumuacha tu aishi tu anavotaka yeye tu, kwasababu alijua kuwa matatizo ni jambo ambalo litakuwa haliepukiki kwake yeye. hivyo alimpa muongozo kupitia huo jinsi gani aishi, kwavile yeye ndiye aliye tuumba basi bila shaka anatujua zaidi kuliko sisi kwa sisi tunavojuana.
Matatizo yote ambayo hii leo dunia inakumbana nayo ni matokeo ya mifumo ya maisha ambayo binadamu waliojitungia wao wenyewe kutoka vichwani mwao nakupangiana sheria ambazo asili wamezitunga wao, huku wakisahau tabia za kimaumbile ambazo wao wanazo, za kuathiriwa na mazingira waliyonayo, kwa kawida binadamu anatabia ya ubinafsi, ambayo inapelekea kujivutia vitu kiupande wake, ndomana leo tunaona wamiliki wa mfumo wa ubepari ambao tunaenda nao leo hii duniani wa kiwa juu na kuwaonea walioko chini, pia wakiendelea kutuletea sheria mbalimbali ambazo kimsingi haziendani na maumbile ya binadamu ndo mana matatizo, amani na utulivu wa nafsi kwa binadamu ni jambo ambalo halipo.
"kwahakika binadamu amepewa elimu ndogo tu" AL Qur-an Karim