Ole wako mwanadamu

Ole wako mwanadamu

Ninaanza kwa salamu kwani siku zote huwa ni jambo la hekima pale popote linapotamkwa(muhali gani), ingawa mimi ni mgeni katika JF ila nahisi umeongelea kitu ambacho moyo wangu umekuwa na shauku ya kuongezea chochote katika hili@Eiyer

Mda mwengine ufahamu mbaya juu ya mambo unaweza ukapelekea product mbaya ya mambo kwani kile ambacho kitakuwa kinaendelea kitakuwa asili yake ni kutokana na ule ufahamu uliobebwa.

Maana ya kuabudu ni kufanya kitu chochote kile chini ya sheria ya Mungu, nasiyo kuenda misikitini au makanisani tu, halafu ukitoka huko Mungu hayupo ni sawa na kuwa na mzazi halafu ukamwambia awe mzazi wako nyumbani tu halafu ukitoka nje hamjuani. Mungu baada ya kumumba binadamu hakumuacha tu aishi tu anavotaka yeye tu, kwasababu alijua kuwa matatizo ni jambo ambalo litakuwa haliepukiki kwake yeye. hivyo alimpa muongozo kupitia huo jinsi gani aishi, kwavile yeye ndiye aliye tuumba basi bila shaka anatujua zaidi kuliko sisi kwa sisi tunavojuana.

Matatizo yote ambayo hii leo dunia inakumbana nayo ni matokeo ya mifumo ya maisha ambayo binadamu waliojitungia wao wenyewe kutoka vichwani mwao nakupangiana sheria ambazo asili wamezitunga wao, huku wakisahau tabia za kimaumbile ambazo wao wanazo, za kuathiriwa na mazingira waliyonayo, kwa kawida binadamu anatabia ya ubinafsi, ambayo inapelekea kujivutia vitu kiupande wake, ndomana leo tunaona wamiliki wa mfumo wa ubepari ambao tunaenda nao leo hii duniani wa kiwa juu na kuwaonea walioko chini, pia wakiendelea kutuletea sheria mbalimbali ambazo kimsingi haziendani na maumbile ya binadamu ndo mana matatizo, amani na utulivu wa nafsi kwa binadamu ni jambo ambalo halipo.

"kwahakika binadamu amepewa elimu ndogo tu" AL Qur-an Karim
 
Nimependa thread yako na jinsi ulivyosisitiza kubadilika kwa mwanadamu katika ulimwengu wa sasa ambapo dunia imekua kijiji. Umekata tamaa mno katika maelezo yako juu ya mwanadam, kana kwamba hakuna wenye utashi na wanaoweza simama wenyewe. Huku ukikataa kua maisha hayajawa rahisi, mazuri na salama.

Nazingatia katika eneo la Rahisi, Mazuri na Salama

Haya mambo sio rahisi kiasi hicho, naomba utambue kwamba urahisi wa maisha sasa hivi ndo unaleta matatizo yoote hayo ambayo umeainisha katika thread yako kwa baadhi ya wanadamu.

Vitu vimerahisishwa mno mpaka wakati mwingine mtu ana lemaa kwa kila kitu, unashida na Fulani basi unampigia simu una haja ya kumfuata – wengine wanapigiana na wako wote nyumba moja wakati huo huo; msomi kapewa assignment katika level ya chuo hataki kusoma vitabu aelewe na kutafakari mwenyewe badala yake ana google kisha ana copy na kupaste.

Watoto saizi michezo badala ya kwenda kucheza mpira amebwagiwa playstation hapo na kila aina ya game unategemea hio product ya watu hao inakua aina gani?

Ni kweli hivyo vitu vinafaa lakini kwa kiwango, tusipoangalia tunaelekea siko. Hivyo tunapozungumzia urahisi nafikiri tusi egemee urahisi wa watu kuishi bali urahisi wa mambo mengi kurahisishwa na jinsi yanavyopelekea kuharibu maisha huo urahisi ukiendekezwa.


Tunapozungumzi uzuri kwa upande wangu ni ile hali ya kusema walau wengi tunajua nini kinaendelea duniani (utandawazi), jinsi gani tunaruhusu na tunakubali kunyonywa na pia jinsi gani tunamapungufu na madhaifu katika maamuzi na uendeshaji wa sekta muhimu hapa nchini.

Utashi wa kutatua matatizo utatoka wapi na hali viongozi wa jana ni wasomi wa juzi, viongozi wa leo ni wasomi wa jana, wasomi wa leo ni viongozi wa kesho… makundi yote hayo matatu yalikua yakililia haki ya kila raia wa Tanzania wakati wakiwa katika kundi la usomi.

Lakini hayo hayo makundi (wasomi) wanapopata nafasi ambayo wanaweza mtumikia mtanzania na kumbadilisha maisha yake anasahau machungu yake na anakua hapo kwa manufaa ya wachache pamoja na familia yake. Uzuri hapo unakuja kua tunajua yote haya - hapo kale wazazi walikua hawana bahati ya kuelewa nini kinaendelea ndani na nje.

Sisi tunajua NDIO lakini haina maana yoyote sababu ukweli unabaki palepale kua watanzania sisi sio wazalendo. Naangalia wapiga kelele humu nchini ni wale wenyewe hatuna kitu cha uhakika ili kuendesha maisha yetu haya ya kudimba.


Ninapozungumzia usalama sina haja ya kwenda mbali, tukiendelea hivi tulivyo sisi Watanzania, wanajamiii, wasomi, viongozi na kukosa uzalaendo kuna USALAMA KWELI?

AshaDii!

Nimependezwa sana na hoja yako .."Rahisi, Mazuri na Salama" ... Ulivyoifafanua nimeilewa lakini naona kama hukuitendea haki dhana nzima ya Rahisi,Mazuri na Salama! Mimi ninaona vyote ulivyojaribu kuonyesha kuwa ni Tatizo la urahisi uliojengwa na technologia na uzuri unaopatikana kutokea kwenye urahisi huo sio tatizo la msingi!

ILA

Tatizo la msingi liko kwenye UTASHI wa mwanadamu mwenyewe.

Kwa kuwa utashi ndio ASILI YETU YA MSINGI kama binadamu inapowekwa kando au kutupiliwa mbali matokeo yake ni kuharibika kwa kila jambo. Teknolojia yenyewe sio tatizo ..lakini ni pale inapotumika pasipo na utashi wa mwandamu.

Kama technolojia ingetumika kwenye utimilifu wa utashi wa mwandamu , uzuri na usalama vingechipua na pasipo na kasoro yeyote kwani Mwandamu hajaasi Utashi uliopia asili na utambulisho wake!

Bila utashi hakuna uzalendo!

Uzalendo ni muendelezo wa Utambulisho wa kweli wa mwadamu kwenye familia yake hadi kwneye jamii yake na hatimaye Taifa lake!

Swali? UTASHI unapatikana wapi? Na tunautunza na kuelea vipi ili usipotee kwenye familia na jamii yetu?
 
Back
Top Bottom