Ombi kwa Polisi: Nyinyi ni wenzetu, kwenye Maandamano yetu tafadhali msigeuke Gestapo au Makaburu!

Tulipongeze jeshi letu la polisi.
P
Kumbe jeshi hili liliundwa 1919? Ndio maana linatenda kikoloni namna hii? Angalia tofauti ya utendaji na JWTZ iliyoanza 1964 utauona waziwazi.
Policemkoloni ife ili ianzishwe Tanpol mpya haya maujinga yatakwisha.
 
Jeshi la Polisi ni wenzetu.
P
 
Hapa ulikuwa bado hujalamba asali
 
Ombi hili hatimaye limeanza kutelelezwa
Polisi ni wenzetu
Ombi hili ndio limeanza kutekelezwa juzi pale furahisha Jeshi la polisi likifanya vyema, lipongezwe, hongera FFU kusambaratisha maandamano bila virungu, mabomu ya machozi, risasi za moto, bila maafa!
P
 
Wanabodi,

Kazi Kuu ya Jeshi la Polisi ni kulinda raia na mali zao, katika kutimiza jukumu hilo, pia wanawajibu wa kutuliza ghasia na kuhakikisha kunakuwepo amani na utulivu kwa ustawi wa taifa hili.
Baada ya kupokea taarifa hii Asante sana kwa taarifa hii, tutashiriki kikamilifu.
Natoa pongezi zangu za dhati kwa Rais Samia, baada ya kuusoma ushauri huu Maandamano ni Haki ya Vyama vya Siasa, Serikali itoe kila ushirikiano kwa CHADEMA hata kama uelekeo ni Ikulu
Atakuwa amekubaliana na ushauri huu. Hivyo sasa wito wangu huu Kufuatia Umuhimu wa Maandamano ya UKUTA: Nimehamasika, Nitashiriki, Tujitokeze kwa Wingi! Ila...!
Uendelee,

Haya shime, tujitokeze kwa wingi kushiriki maandamano muhimu sana haya na hata kukitokea taarifa za kiinteligensia, maandamano yaendelee.

P
 
Kitendo alichofanyiwa huyu mzee wa Chadema ikithibitishwa ni polisi wetu, then ni uthibitisho polisi wetu ni zaidi ya gestapo!.
Nashauri kwa negligence iliyofanywa na Jeshi letu la polisi kuhusu kadhia hii ya kifo cha Mzee Ali Mohamed Kibao, Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA Taifa na Msaidizi wa Katibu Mkuu , kukutwa ameuwawa na mwili wake kutupwa eneo la Kunduchi Ununio,
watu wanne wawajibike!.
1. Waziri - kwa ajali kazini
2. IGP - kwa negligence ya RPC wake
3. RPC -DSM - negligence
4. OCD Kinondoni - negligence, na hawa wawili wa mwisho RPC na OCD wanaweza kufikishwa kwa Pilato!.

Ni wakati sasa Rais Samia kukasirika kama enzi za Nyerere!.
P
 
Naomba kuwaandaa watu kisaikolojia kuhusu siku ya Jumatatu ya tarehe 23 September


Mimi mwenzenu niliwahi kuwa mwanaheshi sio tuu kwa kupita JKT, bali nilikuwa JWTZ.

Naomba niwadondolee sifa za mtu kufanya kazi anayoipenda. Kuna aina tatu za askari jeshi, polisi magereza, FFU, Zimamoto, uhamiaji.
1. Ni wale watu wanaojiunga jeshi kwasababu wanalipenda, yaani yeye kuvaa kijeshi, kutembea kijeshi, kuvaa manyota anapenda anaona raha na kujisikia fahari sana. Hawa ni wanajeshi at heat, for the love of it, wanalipenda jeshi.
2. Ni wale wanajiunga jeshi kama ajira, fursa na opportunities, hawa ni askari for the needs, wanaweza walipende jeshi au wasilipende. Mfano sifa za kuajiriwa polisi ni Division 4 ya points 28-32. Hivyo uki score hivyo, hakuna chuo kingine chochote kinaweza kukupokea zaidi ya CCP!.
3. Wajeshi damu, siku zote kwa watoto wa kiume dad is their hero, their role modal, watoto wa kike. Mama zao. Hivyo mtoto tangu anakuwa anatamani kuwa kama baba au mama, hivyo wazazi wao wanawapa connection na kuwaingiza jeshini, hawa ni askari spoon fed babies.

Miongoni mwa mazoezi ya jeshi, kufanya drills mbalimbali
JWTZ drills yao kubwa ni vita
Polisi ni usalama wa raia na mali zao
FFU ni riot
Zimamoto ni fire drills

Sasa lile kundi la kwanza la askari at heart, wanatamani kweli actions, kule kufanya tuu drills kila uchwao but no actions, wanakuwa bored
Hivyo kuna wanajeshi wanatamani vita, zikija fursa za UN kulinda amani wanafurahi sana, kundi la kwanza kwasababu wana kiu ya action, kundi la pili na la tatu kwasababu ya maokoto.

Askari Zimamoto wanatamani moto kweli wauzime.
FFU wanatamani riot wawatulize,
Hivyo hizo ni picha za mazoezi tuu ya kawaida ya FFU, wakila drills, hivyo actions za mara ya mwisho ni enzi za JK, Enzo za Chuma JPM, kulikuwa hakuna fyoko fyoko, alifunga kila kitu na hakuna aliyekohoa!. Mama kaingia, kaachia, hivyo sasa kuna watu wanataka kumjaribu kwa kumpanda kichwani, hivyo hawa jamaa wana hamu nao sana kufanya action na sio kila siku drills.

Nimeziweka ili msije kusema hatukujua!.

Tafakari Chukua hatua,.

P
 
Neno mene mene tekel upharsin linaonekana katika Danieli 5, pamoja na tafsiri yake. Baadhi ya tafsiri hutamka upharsin kama parsin. Maneno hayo yalionekana ukutani katika jumba la mfalme Belshaza, kaimu mfalme wa Babeli. Anarejelewa kuwa “mwana wa Nebukadreza (Danieli 5:18, 22), ingawa hakuwa mrithi wa karibu wa Nebukadneza (Yeremia 52:31). Simulizi la Biblia la mwonekano wa kustaajabisha na wenye kuogopesha wa usemi mene mene tekel upharsin umetokeza usemi wa kisasa “mwandiko ukutani,” unaomaanisha “ishara au onyo la msiba usioepukika.”
 
Hili ni ombi kwa jeshi letu shupavu, kakamavu, makini na adilifu la polisi.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…