Ombi kwa TFF: Muda wa kuanza mechi za ligi kuu usogezwe mbele kwa mkoa wa Kigoma

Ombi kwa TFF: Muda wa kuanza mechi za ligi kuu usogezwe mbele kwa mkoa wa Kigoma

Phamarcist

JF-Expert Member
Joined
Apr 18, 2021
Posts
219
Reaction score
479
Habari za wakati wanamichezo wenzangu?

Nikiwa kama mkereketwa wa soka mwenye makazi ya muda ndani ya mkoa wa kigoma. Ninaliomba shirikisho la mpira wa miguu ( FF) liangalie muda wa kuanza kwa mechi za ligi kuu kwenye mkoa huu.

Mkoa wetu kigeografia upo tofauti na mikoa mingine kwenye suala la kuchomoza na kuzama kwa Jua, nini maana yangu! Kigoma mpaka saa moja na nusu jua bado linawaka, hivyo basi kitendo cha kuanza mechi saa kumi kinapelekea mashabiki kua kwenye jua kali ndani ya dakika zote tisini.

Ili kuzuia tatizo hili at least mechi zingeanza saa 11 kwani majukwaa yetu hayana kivuli kabisa ukiacha jukwaa la VIP ambalo ni dogo sana kua accommodate watu zaidi ya 50.

Najua changamoto hii wamekutana nayo wengi lakini wamekosa mahala pa kuisemea, mimi binafsi nimeona jukwaa hili linatosha pia kufikisha hoja hii.

Asanteni.
 
Muonekano wa uwanja wa lake Tanganyika.
images%20(12).jpg
 
  • Thanks
Reactions: K11
Habari za wakati wanamichezo wenzangu?

Nikiwa kama mkereketwa wa soka mwenye makazi ya muda ndani ya mkoa wa kigoma. Ninaliomba shirikisho la mpira wa miguu ( TFF ) liangalie muda wa kuanza kwa mechi za ligi kuu kwenye mkoa huu.

Mkoa wetu kigeografia upo tofauti na mikoa mingine kwenye suala la kuchomoza na kuzama kwa Jua, nini maana yangu! Kigoma mpaka saa moja na nusu jua bado linawaka, hivyo basi kitendo cha kuanza mechi saa kumi kinapelekea mashabiki kua kwenye jua kali ndani ya dakika zote tisini.

Ili kuzuia tatizo hili at least mechi zingeanza saa 11 kwani majukwaa yetu hayana kivuli kabisa ukiacha jukwaa la VIP ambalo ni dogo sana kua accommodate watu zaidi ya 50.

Najua changamoto hii wamekutana nayo wengi lakini wamekosa mahala pa kuisemea, mimi binafsi nimeona jukwaa hili linatosha pia kufikisha hoja hii.

Asanteni.
Kiuhalisia kigoma haipo kwenye GMT+3.Kigoma ni GMT+2 kama ilivyo nchi za afrika ya kati.Ombi lako ni sahihi.Saa kumi ya Dareslam,kwa kigoma ni saa Tisa.
 
Wasipokuja na utetezi wa "mdhamini"basi ombi lako litapita ila mashujaa nadhani safari yake kurudi alikotoka imewadia round two havuki
Kaka mashujaa tumesajili, nadhani hujauona ubora wetu kwakua tumekutana na timu mbili za madaraja ya juu kwa wakati mmoja. Ila watoto wa kariakoo wote wanaujua mziki wa masokwe wa lake Tanganyika.
 
Kiuhalisia kigoma haipo kwenye GMT+3.Kigoma ni GMT+2 kama ilivyo nchi za afrika ya kati.Ombi lako ni sahihi.Saa kumi ya Dareslam,kwa kigoma ni saa Tisa.
Ni kweli mkuu, yaani mpaka game inaisha basi kichwa kinauma.
 
  • Thanks
Reactions: K11
Yaa uko sahihi naamini wenye mamlaka watalifanyia kazi... Kigoma jua la saa 10 ni kama saa 8 mchana Dodoma
Sio kweli, nilishakaa Kigoma, tofauti ya muda wa kuzama jua kati ya Dar na Kigoma haizidi dk 40. Na Dar ipo Mashariki kuliko Dodoma

Hilo la jua kuzama saa moja na nusu nao ni uongo wa karne.... Kawaida ni 12:55, likichelewa sana haizidi saa moja na dk kumi
 
Sio kweli, nilishakaa Kigoma, tofauti ya muda wa kuzama jua kati ya Dar na Kigoma haizidi dk 40. Na Dar ipo Mashariki kuliko Dodoma

Hilo la jua kuzama saa moja na nusu nao ni uongo wa karne.... Kawaida ni 12:55, likichelewa sana haizidi saa moja na dk kumi
Hujakaa kigoma mkuu, uliza mtu yeyote akwambie huku mpaka saa moja na nusu jua bado halijazama. Usijaribu kubisha kitu ambacho huna uhakika nacho.
 
Yaani unasema jua linazama 12:55 wewe ni dhahiri hujakaa kigoma kabisa.
 
Sio kweli, nilishakaa Kigoma, tofauti ya muda wa kuzama jua kati ya Dar na Kigoma haizidi dk 40. Na Dar ipo Mashariki kuliko Dodoma

Hilo la jua kuzama saa moja na nusu nao ni uongo wa karne.... Kawaida ni 12:55, likichelewa sana haizidi saa moja na dk kumi
Kama mwanza sasa jua linazama saa 1:08 kwa kigoma jua kuzama saa 1:30 ni ukweli hakuna ubishi.
 
Ashhhh msitusumbue kwanza team yenu inarudi ilipotoka licha kusajili sana dirisha dogo.....asanteni kushiriki
 
Back
Top Bottom