Ombi kwako mwenye mtaji(fedha), tulime/tufuge: mimi nina Nguvu na maarifa

Ombi kwako mwenye mtaji(fedha), tulime/tufuge: mimi nina Nguvu na maarifa

pasikulola

New Member
Joined
Sep 4, 2015
Posts
3
Reaction score
0
Heshima kwenu,.
Kama kichwa kinavyosomeka, nina ombi kwa yeyote anayeweza kuguswa anisaidie mtaji kwa njia ya kufanya kazi ya pamoja kwenye kilimo au ufugaji, hasa nyanya na kuku, kipaumbele kikiwa ni mikoa ya dar es salaam, pwani na mtwara(maboresho yanaweza kufanywa ikibidi).
Binafsi nakosa fedha, lakini nina upenzi na kilimo cha nyanya(tomatoes) na ufugaji kuku. Nina nia, maarifa, afya, Nguvu na uzoefu.
Naamini mpo wenye fedha na hata ardhi katika maeneo niliyolenga ambao mnatamani kufanya shughuli nilizozitaja lakini huenda mnakosa mtu wa kutoa Nguvu zake na maarifa ili kufanikisha kazi tajwa au zinazohusiana na hizo.
Kama nia yako ni hiyo, naomba unisaidie upande wako, nami niwajibike upande wangu kwa kipindi tutakachokubaliana ili nami nipate mtaji kwa kadri ya makubaliano yatakayoafikiwa.
Kwa kifupi mimi ni mwanaume, 30+ yrs old.
Asanteni,....


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unapatikana maeneo gani mkuu...

Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Back
Top Bottom